Nguzo za Imani kwa mujibu wa mafunzo ya kiislami.

Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu nguzo sita za imani katika Uislamu.

NGUZO ZA IMANI

Tunajifunza katika Qur-an na hadithi sahihi kuwa Imani ya Kiislamu imejengwa juu ya nguzo sita zifuatazo:

1 Kumuamini Allah (s.w).

2 Kuamini Malaika wake.

3 Kuamini Vitabu vyake.

4 Kuamini Mitume wake.

5 Kuamini Siku ya mwisho.

6 Kuamini Qadar yake.

 

Hawi Muumini wa Kiislam yule ambaye amekanusha angalau moja ya nguzo hizi kama inavyobainika katika Qur-an:

 

“... Na mwenye kumkanusha Allah (s.w) na Ma la ika wake na Vitabu vyake na Mitume wake na siku ya mwisho., basi bila shaka amepotea upotofu ulio mbali (kabisa)” (4:136)Mtu hatakuwa Muumini kwa kutamka tu hizi nguzo sita, bali pale atakapozijua kwa undani na kuendesha maisha yake yote kwa misingi ya nguzo hizi.

 

Tunazifahamu nguzo hizi sita kutokana na Hadith ya Mtume (s.a.w) iliyosimuliwa na Umar (r.a) kama ifuatavyo:Siku moja tulipokuwa tumeketi pamoja na Mtume (s.aw.) alitutokea mtu mmoja ambaye nguo zake zilikuwa nyeupe kama theluji na nywele zake nyeusi sana, hakuwa na dalili zozote za msafiri, ingawa alikuwa mgeni kwetu sote.

 

Halafu alikaa mbele ya Mtume (s.a.w) hali magoti yake yakikabiliana na yale ya Mtume na akaweka mikono yake katika mapaja ya Mtume na akasema:”Ewe Muhammad nifahamishe juu ya Uislamu ” na Mtume akasema ; “Ni kushuhudia ya kuwa hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allah, Kusimamisha swalaa, kutoa Zakat, Kufunga Mwezi wa Ramadhani, Kuhiji Makkat kwa mwenye kuweza” Halafu yule mgeni akasema “umesema kweli”. Tukastaajabu kwa nini aliuliza halafu akasadikisha.

 

Halafu akasema; “Nifa ham ishe juu ya Iman ”. Mtume akasema : “Ni kumuamini Mwenyezimungu na, Ma la ika wake , Vitabu vyake, Mitume wake, Siku ya Mwisho na Qadar, Kheri na shari yake.

 

Kisha akasema nifahamishe juu ya Ihsaan” Akasema “Ni Kumuabudu Allah kama kwamba unamuona, ikiwa wewe humuoni yeye anakuona ” Halafu akasema nifahamishe juu ya Kiyama ” Akasema: “Hajui mwenye kuulizwa juu ya hilo zaidi ya mwenye kuuliza.

 

Akasema “Nifahamishe dalili zake. Mtume akasema: “Ni wakati ambapo mjakazi atamzaa bibi yake, na utakapowaona wachungaji masikini wanaposhindana kujenga maghorofa. “Yule mgeni alipoondoka, Mtume alikaa kimya kwa muda kisha akasema: “eweUmar, unamfahamu muulizaji?’ Sote tukamjibu kuwa Allah na Mtume wake wanajua zaidi. Mtume akasema “Huyo ni Jibriil amekuja kuwafundisheni dini yenu” (MUSLIM) 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2435

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Mazingatio kabla ya kuosha maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W)

Zifuatazo ni njia nyingi za kumjua Mwenyezi Mungu (EDK form 2:dhana ya elimu katika uislamu)

Soma Zaidi...
Vipi Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia njia ya maandishi

Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi.

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Kujiepusha na Shirk

Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo

Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na nini? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo)

Soma Zaidi...