Nguzo za swala.

Kipengele hiki kinaelezea nguzo mbalimbali za kuswali.

- Ni vile vipengele vinavyokamilisha swala kama ifuatavyo;

  1. Nia (dhamira moyoni).
  2. takbiira ya kuhirimia
  3. kusoma suratul-Fatihah
  4. kurukuu
  5. kujituliza katika rukuu
  6. kuitidali
  7. kujituliza katika itidali
  8. kusujudu
  9. kujituliza katika Sijda
  10. kukaa kati ya Sijda mbili
  11. kujituliza katika kikao kati ya sijda mbili
  12. kusujudu mara ya pili
  13. kujituliza katika sijda ya pili
  14. kukaa Tahiyyatu
  15. kusoma Tahiyyatu
  16. kumswalia au kumtakia rehema na amani Mtume (s.a.w) na waislamu
  17. kutoa salaam
  18. kufuata utaratibu huu (1-17) kwa mfuatano
  1. Nia.
  2. Nguzo za matamshi (visomo)
  3. Takbiira ya kuhirimia swala
  4. Kusoma Suratul-Fatihah
  5. Kusoma Tahiyyatu
  6. Kumswalia Mtume (s.a.w)
  7. Kutoa Salaam
  8. Nguzo za vitendo

-    Ukiondoa nguzo ya ‘Nia’ na ‘kufuata utaratibu’ zilizobaki ni nguzo za vitendo.

.Kufuata utaratibu

-     Ni yale mambo akiyafanya mwenye kuswali, hupandisha daraja ya swala yake

  1. Kuinua viganja vya mikono usawa wa mabega
  2. Kusoma dua baada ya Takbiira ya kuhirimia
  3. Kuanza kwa “Audhubillah” kabla ya kusoma Suratul-fatihah
  4. Kuitikia “Aamin” baada ya kumaliza kusoma Suratul-Fatihah
  5. Kusoma aya za Qur’an baada ya kusoma suratul-Fatihah rakaa mbili za mwanzo
  6. Kusoma Tasbih, Tahmid na dua katika rukuu, itidali, sijda, n.k.
  7. Kukaa na kusoma Tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili.
  8. Kusoma dua baada ya kumswalia Mtume (s.a.w).

Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 100-110

Aya za sijda ndani ya Qur’an ziko 15. 

(7:206), (13:15), (16:50), (17:109), (19:58), (22:18), (22:77), (25:60), (27:26), (32:15), (38:24), (41:38), (53:62), (84:21) na (96:19).

 

 

  1. Kutoelekea Qibla bila dharura (udhuru) wowote kisheria.
  2. Kupatikana na hadathi kubwa (hedhi/nifasi), ndogo (kutengukwa udhu) au ya kati na kati (janaba).
  3. Kufikwa na najisi mwilini, nguoni au mahali pa kuswalia.
  4. Kuvukwa na nguo ukawa uchi – mgongoni, kiunoni, kitovuni, n.k. (tahadhari kuvaa mashati mafupi, madogo kwa wanaume).
  5. Kusema au kutamka makusudi walau herufi moja isiyo na mahusiano na ibada ya swala.
  6. Kula au kunywa chochote hata kwa kusahau.
  7. Kufanya kitendo/jambo lisilohusiana na swala mfululizo mara tatu.
  8. Kuacha nguzo yeyote ya swala.
  9.  Kuzidisha nguzo yeyote ya swala makusudi.
  10. Kumtangulia imamu au kumchelewa (ukiwa maamuma) kwa nguzo mbili za kimatendo mfululizo na makusudi.
  11. Kutia nia ya kuikata swala au kujishauri moyoni uikate swala au usiikate.
  12. Kuwa na shaka kuwa umetimiza au haujatimiza sharti au nguzo yeyote ya swala.
  13. Kupotewa na akili au kulala ndani ya swala.
  14. Kutoa salaam makusudi kabla ya kuisha swala.
  15. Kuswalishwa kwa asiyekuwa muislamu.
  16. Kukhalifu (kutofuata) utaratibu wa Nguzo za swala katika mpangilio wake.
  17. Kuleta dua ya kuomba kitu cha haramu au muhali.
  18. Kumshirikisha Allah (s.w) kwa kuleta dua au maombi.

 

Ni jambo la tatu katika kusimamisha swala

 

Maana ya Khushui – Ni kujituliza kimwili na kifikra na kuzingatia yale mja   anayotenda na kusema katika swala.

-     Utulivu wa mwili hupatikana kwa kutojipapasa papasa, kutochezesha viungo na kuangalia pale tu unaposujudia.

 

2.Kuzituliza fikra (moyo)

-     Fikra hutulia kwa kurejesha na kubakisha mawazo yote ndani ya swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.

 

3.Kuwa na mazingatio

-  Mazingatio hupatikana kwa kujua maana pamoja na kuwa makini na kile unachokisema au unachokitenda ndani ya swala.       

 

-     Ni kutekeleza sharti zote za Swala kikamilifu kabla ya kuanza kuswali.

-     Ni kutekeleza kikamilifu nguzo zote za swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.

      Rejea Qur’an (29:45), (20:14), (7:205), (107:4-6).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3231

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Mambo yanayoweza kutoa udhu wako

Post hii itakufundisha mambo ambayo yanabatilisha udhu.

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo mtu anazuiliwa kurithi mali ya marehemu

Endapo mtu yupp katika orodha ya wanaotakiwa kutithi, anaweza kuzuiliwa kurithi kwa kuzingatia haya.

Soma Zaidi...
Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu

Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.

Soma Zaidi...
Aina au migawanyo mbalimbali ya haki katika uislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...
Sifa za imamu wa swala ya jamaa

Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.

Soma Zaidi...