picha

Nguzo za swala.

Kipengele hiki kinaelezea nguzo mbalimbali za kuswali.

- Ni vile vipengele vinavyokamilisha swala kama ifuatavyo;

  1. Nia (dhamira moyoni).
  2. takbiira ya kuhirimia
  3. kusoma suratul-Fatihah
  4. kurukuu
  5. kujituliza katika rukuu
  6. kuitidali
  7. kujituliza katika itidali
  8. kusujudu
  9. kujituliza katika Sijda
  10. kukaa kati ya Sijda mbili
  11. kujituliza katika kikao kati ya sijda mbili
  12. kusujudu mara ya pili
  13. kujituliza katika sijda ya pili
  14. kukaa Tahiyyatu
  15. kusoma Tahiyyatu
  16. kumswalia au kumtakia rehema na amani Mtume (s.a.w) na waislamu
  17. kutoa salaam
  18. kufuata utaratibu huu (1-17) kwa mfuatano
  1. Nia.
  2. Nguzo za matamshi (visomo)
  3. Takbiira ya kuhirimia swala
  4. Kusoma Suratul-Fatihah
  5. Kusoma Tahiyyatu
  6. Kumswalia Mtume (s.a.w)
  7. Kutoa Salaam
  8. Nguzo za vitendo

-    Ukiondoa nguzo ya ‘Nia’ na ‘kufuata utaratibu’ zilizobaki ni nguzo za vitendo.

.Kufuata utaratibu

-     Ni yale mambo akiyafanya mwenye kuswali, hupandisha daraja ya swala yake

  1. Kuinua viganja vya mikono usawa wa mabega
  2. Kusoma dua baada ya Takbiira ya kuhirimia
  3. Kuanza kwa “Audhubillah” kabla ya kusoma Suratul-fatihah
  4. Kuitikia “Aamin” baada ya kumaliza kusoma Suratul-Fatihah
  5. Kusoma aya za Qur’an baada ya kusoma suratul-Fatihah rakaa mbili za mwanzo
  6. Kusoma Tasbih, Tahmid na dua katika rukuu, itidali, sijda, n.k.
  7. Kukaa na kusoma Tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili.
  8. Kusoma dua baada ya kumswalia Mtume (s.a.w).

Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 100-110

Aya za sijda ndani ya Qur’an ziko 15. 

(7:206), (13:15), (16:50), (17:109), (19:58), (22:18), (22:77), (25:60), (27:26), (32:15), (38:24), (41:38), (53:62), (84:21) na (96:19).

 

 

  1. Kutoelekea Qibla bila dharura (udhuru) wowote kisheria.
  2. Kupatikana na hadathi kubwa (hedhi/nifasi), ndogo (kutengukwa udhu) au ya kati na kati (janaba).
  3. Kufikwa na najisi mwilini, nguoni au mahali pa kuswalia.
  4. Kuvukwa na nguo ukawa uchi – mgongoni, kiunoni, kitovuni, n.k. (tahadhari kuvaa mashati mafupi, madogo kwa wanaume).
  5. Kusema au kutamka makusudi walau herufi moja isiyo na mahusiano na ibada ya swala.
  6. Kula au kunywa chochote hata kwa kusahau.
  7. Kufanya kitendo/jambo lisilohusiana na swala mfululizo mara tatu.
  8. Kuacha nguzo yeyote ya swala.
  9.  Kuzidisha nguzo yeyote ya swala makusudi.
  10. Kumtangulia imamu au kumchelewa (ukiwa maamuma) kwa nguzo mbili za kimatendo mfululizo na makusudi.
  11. Kutia nia ya kuikata swala au kujishauri moyoni uikate swala au usiikate.
  12. Kuwa na shaka kuwa umetimiza au haujatimiza sharti au nguzo yeyote ya swala.
  13. Kupotewa na akili au kulala ndani ya swala.
  14. Kutoa salaam makusudi kabla ya kuisha swala.
  15. Kuswalishwa kwa asiyekuwa muislamu.
  16. Kukhalifu (kutofuata) utaratibu wa Nguzo za swala katika mpangilio wake.
  17. Kuleta dua ya kuomba kitu cha haramu au muhali.
  18. Kumshirikisha Allah (s.w) kwa kuleta dua au maombi.

 

Ni jambo la tatu katika kusimamisha swala

 

Maana ya Khushui – Ni kujituliza kimwili na kifikra na kuzingatia yale mja   anayotenda na kusema katika swala.

-     Utulivu wa mwili hupatikana kwa kutojipapasa papasa, kutochezesha viungo na kuangalia pale tu unaposujudia.

 

2.Kuzituliza fikra (moyo)

-     Fikra hutulia kwa kurejesha na kubakisha mawazo yote ndani ya swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.

 

3.Kuwa na mazingatio

-  Mazingatio hupatikana kwa kujua maana pamoja na kuwa makini na kile unachokisema au unachokitenda ndani ya swala.       

 

-     Ni kutekeleza sharti zote za Swala kikamilifu kabla ya kuanza kuswali.

-     Ni kutekeleza kikamilifu nguzo zote za swala kuanzia mwanzo hadi mwisho wa swala.

      Rejea Qur’an (29:45), (20:14), (7:205), (107:4-6).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3340

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 web hosting    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Mali zinazojuzu kutolewa zaka, nisaab yake na viwango vyake

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kumuandaa maiti baada ya kufa

Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.

Soma Zaidi...
Adhabu ya mzinifu katika jamii ya kiislamu

(iii) Adhabu ya UzinifuKatika Sheria ya Kiislamu mtu haadhibiwi mpaka atende kwa uwazi matendo yenye kuvuruga utaratibu na amani ya jamii.

Soma Zaidi...
Hawa ndio wanaoruhusiwa kurithi

Hii ni orodha ya watu ambao wanaweza kurithi malibya marehrmu.

Soma Zaidi...
Hadhi na Haki za Mwanamke katika jamii mbalimbali hapo zamani

Utangulizi:Uislamu unamuelekeza mwanaadamu namna nzuri ya kuendesha maisha yake katika kila kipengele cha maisha akiwa binafsi, katika familia na katika jamii.

Soma Zaidi...
Hijjah

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Fiqh.

Kipengele hichi tutajifunza chimbuko la fiqh na maana ya figh.

Soma Zaidi...