image

Nguzo za uislamu

Katika kipengele hiki tutajifunza nguzo za uislamu.aina tano za nguzo za uislamu,dhana ya nguzo za uislamu,lengo na umuhimu wa nguzo za uislamu

6.NGUZO ZA UISLAMU.

6.1.Dhana ya Nguzo za Uislamu.

Rejea Hadith ifuatayo:

Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:

“Uislamu umejengwa juu ya nguzo tano; Kushuhudia kuwa hapana Mola ila Allah na kushuhudia kuwa Muhammad ni Mtume wa Allah, Kusimamisha Swala, Kutoa Zaka, Kufunga Ramadhani na Kuhiji Makkah kwa mwenye uwezo.” (Bukhari na Muslim).

 

Kutokana na Hadith hii, nguzo za Uislamu ni:

  1. Kutoa Shahada mbili, kwa kushuhudia kuwa hapana Mola ila Allah na kushuhudia kuwa Muhammad ni Mtume wa Allah.
  2. Kusimamisha Swala.
  3. Kutoa Zakat.
  4. Kufunga mwezi wa Ramadhani.
  5. Kuhiji Makkah kwa mwenye uwezo.

 

Hadith hii inatufahamisha kuwa “Uislamu umejengwa juu ya nguzo tano” na sio “Uislamu ni nguzo tano”.

 

Hii ina maana kuwa misingi ya kusimama Uislamu ni nguzo tano lakini Uislamu hauwezi kukamilika (kusimama) kwa kusimamisha nguzo tano tu.

 

-     Nguzo tano ni nyenzo za kumuandaa muislamu kuweza kumuabudu Mola wake katika kila kipengele cha maisha yake ya kila siku.

 

-     Nguzo za Uislamu ni sehemu ndogo sana katika ibada ya muislamu ya maisha yake ya kila siku, mfano; shahada ni wastani wa 0% ya umri, swala ni 7% ya muda wa siku, zaka ni 2½ % ya mali yote ya tajiri, funga ni 5% ya saa za funga kwa mwaka na hija ni 0% ya umri wa mtu.

 

-     Jumla ya ibada ya nguzo 5 za Uislamu katika maisha ya muislamu ni wastani wa 3% tu na 97% ni nje ya ibada. 

 

-     Hivyo kutekeleza nguzo tano tu ni sawa na kufanya ibada 3% ya maisha na 97% ni nje ya ibada ambalo ndio lengo la kuumbwa mwanaadamu.

 

-     Kila nguzo ya Uislamu ina lengo maalumu na umuhimu wake katika kumuandaa mja kuweza kumuabudu na kumtumikia Mola wake ipasavyo.

 

 

 

Nguzo za Uislamu zina umuhimu na malengo maalumu kama ifuatavyo:

  1. Shahada mbili.

-     Ni kiingilio (kitambulisho) cha muislamu kwa ummah wa Kiislamu anayoitoa muislamu mbele ya ummah.

 

-     Ni kutoa ahadi ya kumtii Allah (s.w) ipasavyo katika kukiendea kipengele cha maisha ya kila siku saa 24.

 

2.Kusimamisha Swala.

-     Ni nguzo ya pili na ni nguzo kuu ya Uislamu na ni amri ya Allah (s.w) kwa waislamu wote katika kuitekeleza.

 

-     Lengo kuu la kusimamisha swala ni kumtakasa mja kutokana na mambo maovu na machafu.

      Rejea Qur’an (29:45).

 

3.Zakat.

-     Ni nguzo ya tatu ya Uislamu na ni amri ya Allah (s.w) kwa waislamu matajiri kuitekeleza.

 

-     Zaka ina lengo la utakaso (kuitakasa):

         Rejea Qur’an (9:103).

 

4.Swaumu.

-     Ni nguzo ya nne ya Uislamu na ni amri ya Allah (s.w) kwa waislamu kufunga mwezi wa Ramadhani.

 

-     Swaumu ina lengo la kumuandaa mja kuwa Mcha-Mungu atakaye mtii Allah (s.w) ipasavyo katika maamrisho na makatazo yake.

Rejea Qur’an (2:183).

 

5.Hija.

-     Ni nguzo ya tano ya Uislamu na ni amri ya Mwenyezi Mungu (s.w) kwa waislamu wenye uwezo wa mali na afya.

 

-     Hija ina lengo la kumtayarisha mja kumpenda Allah (s.w) kuliko kitu chochote hata nafsi yake.

 

-     Inamuandaa mja kuwa askari aliyetayari kutumia mali na nafsi yake katika kupigania dini yake.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 3745


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Taratibu za mahari katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu. Soma Zaidi...

Kumuandaa maiti punde baada ya kufariki dunia
Soma Zaidi...

NGUZO ZA UISLAMU: SWALA NA SHAHADA NA FAIDA ZAKE
NGUZO ZA UISLAMU. Soma Zaidi...

Mgawanyo wa mirathi kutoka kwenye Quran
Quran imegawanya mirathi katika haki. Mgawanyo huu ndio unaotakiwa utumike na si vinhinevyo. Soma Zaidi...

Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu
Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili. Soma Zaidi...

Uzuri wa Benki za kiislamu
Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine? Soma Zaidi...

Haki, wajibu na majukumu katika familia ya kiislamu na majirani zake
Soma Zaidi...

Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya
Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu. Soma Zaidi...

Maana ya uadilifu na usawa na tofauti zao
Posti hii itakwenda kukufunza utofauti kati ya uadilifu na usawa Soma Zaidi...

Funga ya ramadhan na nyinginezo
Nguzo za uislamu (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kutoa vilivyo halali
Nguzo za uislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...