Kafara kwa mwenye kuvunja masharti ya Ihram
Allah (s.w) kwa Urehemevu wake, ametoa nafuu kwa wale watakaovunja masharti ya Ihram kwa kutoa fidia isipokuwa kwa kosa la jimai.Tunafahamishwa katika Qur-an:
'... Na atakayekuwa mgonjwa katika nyinyi au ana vya kumuudhi kichw ani mw ake (akafanya yaliyokatazw a, kama vile kunyoa), basi atoe fidia kwa kufunga au (kwa kutoa) sadaqat au kuchinja mnyama ...' (2:196)
Katika Hadith tunafahamishwa:
Ka'ab bin Ajra (r.a) ameeleza: 'Nilipokuwa katika (hali ya) Ihram kwa ajili ya 'Umra nilisumbuliwa sana na chawa kichwani mwangu. Mtume wa Allah (s.a.w) akaniambia ninyoe kisha nifunge siku tatu au nichinje mbuzi wa sadaqat au niwalishe maskini sita. (Bukhari, Muslim, Abu Da ud).
Kwa hiyo kwa Muharim atakayevunja sharti lolote la Ihram atalazimika kutoa kafara kwa ama
(i) kufunga siku 3 au
(ii) kumchinja mbuzi na kuitoa nyama yake sadaqat au
(iii) kulisha maskini sita.
Kumwingilia mke ni kosa lisilosameheka kwa kutoa kafara bali hubatilisha Hija au 'Umra moja kwa moja. Ama kwa mume aliyefanya mapenzi na mkewe kwa kubusiana na kumkumbatia bila ya kufanya kitendo cha ndoa, atatoa kafara ya ngamia (au thamani yake) kama atatokwa na manii na kama hatatokwa na manii, atatoa kafara ya mbuzi.
Kafara kwa mwenye kuwinda au kuonyesha windo akiwa katika Ihram ni mbuzi iwapo mnyama huyo ana ukubwa wa mbuzi, au mdogo zaidi kuliko hivyo; vinginevyo atatoa kafara ya mnyama aliye sawa na huyo aliyemuwinda au atatoa thamani yake anunue vibaba vya chakula kinacholiwa sana katika sehemu hiyo, na kumlisha kila maskini kwa vibaba vitakavyopatikana. Hivi ndivyo tunavyoagizwa katika Qur-an:
Enyi mlioamini! Msiue mawindo na hali ya kuwa mmo katika Hija au 'Umra. Na miongoni mwenu atakayemuua makusudi basi malipo yake yatakuwa kwa (kuchinja) kilicho sawa na alichokiua katika wanyama wanaofugwa kama watavyohukumu waadilifu wawili miongoni mwenu.Mnyama huyo apelekwe ilipo Ka 'aba (akachinjwe na kutolewa sadaqat huko) au badala ya hayo ni kufunga, ili aonje ubaya wa jambo lake (hili). Mw enyezi Mungu ameyafuta yaliyopita; lakini atakayefanya tena Mw enyezi Mungu atam uadhibu. Na Mw enyezi Mungu ndiye Mw enye Nguvu na Mwenye kuadhibu. (5:95).
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa
Mwandhishi Tarehe 2018-08-01 Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 166
Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani
👉2 Kitau cha Fiqh
👉3 Kitabu cha Afya
👉4 kitabu cha Simulizi
Hukumu na taratibu za mirathi na kurithi katika uislamu
Soma Zaidi...
Sababu za mdomo kuwa mchungu
Hapa utajifunza sababu zinzopelekea mdomo kubadilika ladha na kuwa mchungu, ama mchachu. Soma Zaidi...
Kumkafini maiti namna ya kushona sanda ya maiti na utaratibu wa kumvisha sanda maiti
2. Soma Zaidi...
Hukumu ya zakat Al-Fitir na namna ya kuitoa zaka ya fitir
Soma Zaidi...
Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii
Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s. Soma Zaidi...
Kuwafanyia Wema Wazazi
Allah (s. Soma Zaidi...
nmna ya kufanya istikhara na kuswali swala ya Istikhara
Soma Zaidi...
(ii)Hum cha Allah (s.w) kwa kutekeleza amri zake
Anapotajwa Mwenyezi Mungu au wanapokumbushwa juu ya maamrisho na makatazo ya Mwenyezi Mungu, nyoyo zao hunyenyekea na kufuata kama walivyokumbushwa. Soma Zaidi...
Epuka kuwa muoga na yajue madhara ya uwoga
36. Soma Zaidi...
Chanzo cha vita vya Siffin na matokeo yake: Vita vya Ally na Muawia
Soma Zaidi...