kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii

kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii

11.

Download Post hii hapa

kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii

11. Kuwa na Kauli Njema


Muislamu anatakiwa kila mara azungumze mambo ya maana na ya kheri. Ulimi utumike kusema ukweli, kuamrisha mema, kukataza maovu, kuwashauri wengine juu ya mambo ya kheri, kupatanisha waliogombana, kumsabihi Allah, kutoa elimu yenye kunufaisha watu na katika mazungumzo mengine ya kheri.


“Na ni nani asemaye kauli bora kuliko (yule) aitaye (watu) kwa Allah na (mwenyewe) akafanya vitendo vizuri na kusema (kwa maneno yake na vitendo vyake): “Hakika mimi ni miongoni mw a Waislamu ”. (41:33).
Allah (s.w) anatuamrisha kusema maneno mazuri katika aya ifu atayo:

“Na waambie waja wangu waseme daima maneno yaliyo mazuri. Maana Shetani huchochea ugomvi baina yao. Hakika shetani kwa wanaadamu ni adui aliye dhahiri”. (17:53)
Hivyo Muislamu hana budi kuzungumza na watu kwa maneno mazuri ya heshima. Maneno mazuri ya heshima yanajenga na kuzidisha upendo kati ya watu. Maneno mazuri ya heshima ni ngao ya kumzuilia shetani asiingilie kati na kuleta migongano na kutoelewana. Ni katika msingi huu tunaamrishwa tuulinganie Uislamu kwa hekima na kwa mawaidha mazuri:

“Walinganie (watu) katika njia ya Mola wako kwa hekima na mawaidha m em a, na ujadiliane nao kw a namna iliyo bora. Hakika Mola w ako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake naye ndiye anayewajua walioongoka ”. (16:125).
Kauli njema ni yenye kumuongoza mja kwenda Peponi na kauli mbaya humuongoza mja kwenda Motoni kama tunavyojifunza katika Hadithi zifuatazo:
Sahl bin Sa ’d(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Atakayeweza kuchunga kilichopo kati kati ya taya zake (ulimi) na kilichopo katikati ya miguu yake miwili (utupu) ninaw eza kumhakikishia Pepo.” (Bukhari).

Abu Hurairah(r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Mja atatamka neno lenye kumfurahisha Allah bila ya kuona uzito wake, bado Allah (s.w) humlipa malipo makubwa kutokana na neno hilo. Na mja atatamka neno lenye kumuudhi Allah bila ya kuona uzito wake, na bado linakuw a ndio mw anzo w a kumuingiza Motoni. (Bukhari).



                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1373

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Maana ya Hadith al Quds na Hadith an-Nabawiy
Maana ya Hadith al Quds na Hadith an-Nabawiy

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya hadithi al Quds na Hadith an-Nabawiy

Soma Zaidi...
Uandishi wa hadithi wakati wa Matabii tabiina (tabiitabiina)
Uandishi wa hadithi wakati wa Matabii tabiina (tabiitabiina)

Hii ni historia ya uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina. Yaani wafuasi wa wale wafuasi wa Masahaba

Soma Zaidi...
DUA ZA WAKATI WA SHIDA
DUA ZA WAKATI WA SHIDA

DUA ZA WAKATI WA SHIDA 1.

Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w
Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w

Hii ni historia ya Imamu Bukhary pamoja na kitabu chake cha sahihul Bukhari.

Soma Zaidi...
Dua za kumuomba Allah wakati wa shida na tabu ama matatizo
Dua za kumuomba Allah wakati wa shida na tabu ama matatizo

Post hii inakwenda kukufundisha dua ambazo ni muhimu kuzisoma wakayi wa shida na taabu.

Soma Zaidi...