picha

Epuka kuwa muoga na yajue madhara ya uwoga

36.

Epuka kuwa muoga na yajue madhara ya uwoga

36. Kuepukana na Woga



Kinapokosekana kipengele hiki cha “kumtegemea Mwenyezi Mungu katika kila hali” katika tabia au mwendo wa mja nafasi yake inajazwa na kipengele cha “woga”. Woga na khofu juu ya matukio mbali mbali ya maisha ya hapa ulimwenguni husababishwa na uhaba wa imani


juu ya Allah (s.w) na sifa zake. Mtu asiyemtegemea Mwenyezi Mungu hudhania kuwa mafanikio yote ya maisha hupatikana kwa uwezo wa mwanaadamu na kuwa ni mwanaadamu pekee mwenye uwezo wa kujikinga na shari zote zinazomkabili.Dhana hii humtia mtu katika wasi wasi na woga atakapohisi kuwa tatizo au dhara fulani linalomkabili litamshinda nguvu kwa kuwa hana uwezo au msaada wa mwanaadamu wa kumuwezesha kupambana nalo.



Muislamu wa kweli hapaswi kuwa mwoga wa chochote kwa sababu hapana chochote kinachoweza kumdhuru, ila awe amekadiria hivyo Mwenyezi Mungu (s.w) na hapana mja awezaye kuepa ajali yake aliyoandikiwa na Mwenyezi Mungu. Muislamu anatakiwa awe imara katika kusimamisha Dini ya Allah katika kila kipengele cha maisha yake, bila ya kuhofu chochote kwani yeye daima yuko chini ya ulinzi na uangalizi wa Mwenyezi Mungu (s.w), na halitamsibu ila lile alilomuandikia Mwenyezi Mungu (s.w).


“Sema; halitatusibu ila alilotuandikia Mwenyezi Mungu, yeye ni Mola wetu. Basi Wa is lamu na wamtegemee Mwenyezi Mungu tu ”(9:51).
Pia Allah (s.w) ametukataza kuwaogopa makafiri:


“ Leo makafiri wamekata tamaa na dini yenu basi msiwaogope, bali
n iogop en i mimi ”(5:3).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 1807

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 ai web app    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Elimu

Uwanja wa elimu na maarifa

Soma Zaidi...
Kwanini Ni muhimu kusimamisha uislamu katika jamii

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Zoezi la 3

Kipengele hichi kina maswali mbalimbali kuhusiana na dini na mitazamo mbalimbali.

Soma Zaidi...
Kitabu Cha Dua 120

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
KULA HALALI NA ZILICHO KIZURI NI AMRI KATIKA UISLAMU

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم "إنَّ اللَّهَ طَيِّبٌ لَا يَقْبَلُ إلَّا طَي...

Soma Zaidi...
Zoezi

Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira.

Soma Zaidi...