Sunnah za Swala
        Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi. Ama mwenye kuswali akiacha kipengele chochote katika vipengele vya sunnah, swala yake itakamilika iwapo atatekeleza vipengele vyote vya nguzo. Katika Hadith tumeona kuwa Mtume (s.a.w) katika swala yake pana vipengele vya ziada ya nguzo kama ifuatavyo:
        1.Kuinua viganja vya mikono mkabala na mabega, usawa wa vigingi vya masikio wakati wa kuhirimia swala, kwenda kwenye rukuu, baada ya rukuu na baada ya kutoka kwenye Tahiyyatu ya kwanza.
        2.Kusoma dua baada ya takbira ya kuhirimia.
        3.Kuanza na a ’udhubillaah (kumlaani Shetani) kabla ya kuanza kusoma suratul-Fatiha.
        4.Kuitikia “Aamin”baada ya kumaliza Suratul Fatiha.
        5.Kusoma aya za Qur-an baada ya Suratul-Fatiha katika rakaa mbili za mwanzo.
        6.Kuleta Tasbih, Tahmid na dua katika rukuu, itidali na s ijda.
        7.Kutoa takbira katika kubadilisha kitendo kimoja kuendea kingine isipokuwa tu kutoka kwenye rukuu kwenda kwenye itidali ndipo tunaposema: “Sami’Allahu liman hamidah - Rabbanaa lakal-hamdu”.
        8.Kukaa na kusoma Tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili, kwa swala zenye rakaa zaidi ya mbili.
        9.Kusoma dua baada ya kumswalia Mtume na kabla ya kutoa S a la am.
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inakwendabkukujiulisha maana ya twahara na jinsi ya kujitwaharisha.
Soma Zaidi...Kutawadha ni katika ibada muhimu za mwanzo kutakiwa kuzijuwa na ni lazima. Swala yako haitaweza kutimia bila ya kujuwa udhu. Inakupasa kujuwa nguzo za udhu, yanayoharibu udhu na namna ya kutawadha kifasaha. Hapa utajifunza hatuwa za kutawadha
Soma Zaidi...Tofauti na maradhi yaliyotajwa hapo juu pia tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwepo kwa maradhi mengine hatari yanayosambazwa na mbu, kama vile ngirimaji pamoja na matende.
Soma Zaidi...Atika uislamu swala la kupanga uzazi linaruhusiwa endapo kutakuwa na sababu maalumu za kisheria.
Soma Zaidi...Kuzika Kuzika ni kitendo cha nne cha faradh tunacho lazimika kumfanyia ndugu yetu aliyetutangulia kufa.
Soma Zaidi...