Maana ya Kusimamisha Swala
        Kusimamisha swala ni tofauti na kuswali. Kuswali ni kufanya vitendo vya swala kama vile kusimama, kurukuu, kuitidali, kusujudu, n.k. Kusimamisha swala ni kuitekeleza swala kwa kuchunga na kutekeleza kwa ukamilifu yafuatayo:
        (i)Sharti zote za swala.
        (ii)Nguzo zote za swala.
        (iii)Kuwa na khushui (unyenyekevu) wakati wote wa kutekeleza sharti na nguzo za swala.
        Mtu akiswali bila ya kuzingatia na kutekeleza kwa ukamilifu mambo haya matatu, ataonekana kuwa kaswali, lakini atakuwa hajasimamisha swala na atastahiki kuadhibiwa vikali na Mola wake kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:
        โBasi adhabu kali itawathibitikia wanaoswali, ambao wanapuuza swala zao (kwa kutozisimamisha), ambao hufanya ria โ. (107:4-6)
        Kupuuza swala ni pamoja na kutotekeleza ipasavyo sharti za swala, nguzo za swala, na kutokuwa na unyenyekevu wakati wa kutekeleza sharti na nguzo za swala.
        Hivyo, swala inayokubalika mbele ya Allah (s.w) ni ile iliyosimamishwa kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:
โHakika wamefuzu w aumini ambao katika swala zao ni wanyenyekevu โ. (23:1-2)
        โNa ambao swala zao w anazihifadhiโ . (23:9)
        Kuhifadhi swala ni kutekeleza kwa ukamilifu sharti na nguzo zote za swala.
Umeionaje Makala hii.. ?
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukujuza kuhusu swala za qabliya, baadiya na tahiyatul masjid.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi
Soma Zaidi...Katika post hii utakwenda kujifunza mambo ambayo ni haramu kwa mwanamke aliye na hedhi na nifasi
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...