Ni zipi siku ambazo ni haramu kufunga? na ni kwa nini hairuhusiwi kufunga katika siku hizo

Ni zipi siku ambazo ni haramu kufunga? na ni kwa nini hairuhusiwi kufunga katika siku hizo

Siku Zilizoharamishwa Kufunga Sunnah



(i)Siku kuu za Iddil-Fitri na Iddil-Hajj



Imeharamishwa kufunga katika siku hizi kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:
Abu Sayyid al-Khudri (r.a) ameeleza kwamba Mtume (s.a.w) amesema: Hakuna funga katika siku mbili - siku ya (Iddil) Fitr na siku ya (Idd ya) kuchinja.” (Bukhari na Muslim).



(ii)Siku za Tashriq
Siku za Tashriq ni mwezi 11 hadi 13 Dhul-Hijjah. Ni haram kufunga
katika siku hizi kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatayo:
Ibn Al-Hazali(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Siku za Tashriqu ni siku za kula na kunywa na kumkumbuka Allah (s.w) (kwa Takbira). (Muslim).



(iii)Siku ya Shaka
Siku ya Shaka ni siku moja kabla ya Ramadhani. Yaani mwezi 30 Shaabani ambapo inawezekana ikawa ni siku ya kufunga. Mtume (s.a.w) amekataza kufunga sunnah katika siku hii ya mashaka ila kwa yule mwenye ada ya kufunga. Kwa mfano mtu mwenye ada ya kufunga Jumatatu ameruhusiwa kufunga endapo siku hiyo itaangukia Jumatatu. Hadith ifuatayo inabainisha makatazo haya:



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuw a Mtume wa Allah amesema: “Usifunge siku moja au mbili kabla ya Ramadhani ila kwa mtu yule mwenye ada ya kufunga funga fulani (k.m. funga ya Alhamisi), yeye anaruhusiwa kufunga ” (Muslim).



Inatakiwa siku moja au mbili kabla ya Ramadhani tusifunge ili tuweze kuukabili tukiwa na nguvu mpya na ili tutofautishe funga ya Ramadhani na funga za Sunnah.



(iv) Siku ya Ijumaa
Mtume (s.a.w) amekataza funga ya Sunnah katika siku ya Ijumaa tu, lakini kama mtu ana tabia ya kufunga sunnah, ikatokea siku ya Ijumaa ni miongoni mwa siku anazofunga, basi hapana ubaya. Tunajifunza haya katika Hadith zifuatazo:



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Na asifunge siku ya Ijumaa yeyote miongoni mwenu; ila tu akiwa ameanza kufunga kabla yake au ameendelea kufunga baada yake”. (Muslim).



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Usiuchopoe usiku kabla ya Ijumaa ukafanya usiku pekee kwa kusimama kwa swala na usiichague siku ya Ijumaa pekee kati ya siku za wiki kuwa ndio siku ya kufunga, ila kama mmoja wenu ana tabia ya kufunga sunnah na ikatokea siku ya Ijumaa imeangukia katika tarehe anayopaswa kufunga. ” (Muslim).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2626

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Ni nini maana ya Talaka katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.

Soma Zaidi...
Kujitwaharisha kutokana na najisi

Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl

Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl

Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria.

Soma Zaidi...
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.

Soma Zaidi...
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.

Soma Zaidi...
Kutoa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...