Zifahamu njia za kutwaharisha, aina za maji, udongo na Namna ya kujitwaharisha

Zifahamu njia za kutwaharisha, aina za maji, udongo na Namna ya kujitwaharisha

Download Post hii hapa

Zifahamu njia za kutwaharisha, aina za maji, udongo na Namna ya kujitwaharisha

Chakujitwah aris hia



Nafsi ya mtu hutwaharika kwa mtu huyo kumuamini Allah (s.w) ipasavyo na kufuata mwongozo wake katika kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na kijamii.
Muislamu atatwaharika kutokana na Najisi na Hadath kwa kutumia maji safi au udongo safi kwa kufuata masharti na maelekezo ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake.



Sifa za Maji Safi
Maji safi kwa mtazamo wa twahara ni yale yanayofaa kujitwaharishia yaliyogawanyika katika makundi yafuatayo:

(a)Maji Mutlak (maji asili)
Maji yoyote katika hali yake ya asili ni maji safi yanayofaa kujitwaharishia. Maji asili (natural water) ni maji ya mvua, chem chem, visima, mito, maziwa na maji ya bahari.



(b)Maji mengi:



Maji mengi ni maji yaliyokusanywa au yaliyokusanyika pamoja na kuwa na ujazo wa mabirika (qullatain) au ujazo usiopungua madebe 12. Mfano wa maji mengi yaliyokusanywa ni maji ya mapipa yenye ujazo wa lita 240, maji ya mabirika (matangi) maalum yaliyojengwa kuhifadhia maji msikitini na nyumbani. Mfano wa maji mengi yaliyojikusanya ni yale ya madimbwi makubwa yanayojikusanya wakati wa mvua.



Maji mengi hayahabiriki upesi. Hayaharibiki kwa kujitwaharishia ndani ya chombo kilichoyakusanya au ndani ya mkusanyiko huo wa maji. Pia maji mengi hayaharibiki kwa kuingiwa na najisi. Bali maji mengi yatakuwa hayafai kujitwaharishia iwapo yatabadilika asili yake katika rangi au utamu (ladha) au harufu.



(c)Maji machache:



Maji machache ni yale yaliyokusanywa katika chombo au yaliyojikusanya katika ardhi yakiwa na ujazo chini ya Qullatain* au chini ya ujazo wa pipa lenye ujazo wa madebe 12 au chini ya ujazo wa lita 224. Mfano wa maji machache ni ya ndoo, maji ya mtungi na maji yaliyojikusanya kwenye vidimbwi vidogo vidogo wakati wa mvua.



Maji machache hayatafaa kujitwaharishia iwapo



(i)yataingiwa na najisi japo kidogo sana.
(ii)Iwapo yatakuwa yametumika katika kujitwaharishia humo humo kwa kuondoa najisi au Hadath.
(iii)Iwapo yatakuwa yametumika kwa kufulia au kuoshea vyombo au kuogea humo humo.
(iv)Iwapo yataingiwa na kitu kikayabadilisha asili yake katika rangi, harufu au tamu(ladha).



Kutokana na haya tunajifunza kuwa, tunapokuwa na maji machache hatuna budi kuwa waangalifu wakati wa kuyatumia ili tusiyaharibu. Tusijitwaharishe ndani ya vyombo vilivyohifadhia maji hayo, bali tuyateke na kujitwaharisha mbali nayo. Kwa mfano tunakoga kwa kutumia kata na tunatawadha kwa kutumia kopo au birika.



(d)Maji makombo



Maji makombo ni maji yaliyonywewa na binaadamu au mnyama yakabakishwa.Maji makombo yanafaa kujitwaharishia ila yale yaliyonywewa na kubakishwa na mbwa au nguruwe.



Udongo safi



Udongo safi ni ule ulioepukana na najisi na ukabakia katika asili yake na kutochanganyika na kitu kama vile unga, majivu au vumbi la mkaa, vumbi la mbao (saw dust) n.k. kwa kawaida udongo wote katika ardhi ni safi.


                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1712

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Wafundisheni kuswali watoto wenu
Wafundisheni kuswali watoto wenu

Mtume amemfundisha kuwa watoto wafundishwe kuswali wakiwa na miaka saba na waadhibiwe wakiacha wakiwa na miaka 10

Soma Zaidi...
Maana ya kusimamisha swala
Maana ya kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili
Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili

Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake.

Soma Zaidi...
Utaijuwaje kama swala yako imekubalika
Utaijuwaje kama swala yako imekubalika

Hapa tunakwenda kuona jinsi ya kuzitathmini swala zetu.

Soma Zaidi...
Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda
Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala vitani
Jinsi ya kuswali swala vitani

Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swala ya haja
Jinsi ya kiswali swala ya haja

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya haja na jisi ya kuiswali.

Soma Zaidi...