image

Ni Ipi Elimu yenye manufaa

Elimu inaweza kugawanyika katika makundibmrngine mawili ambayo ni elimu yenye manufaa na elimubisiyi na manufaa

Elimu yenye Manufaa

Elimu yenye manufaa ni ile ambayo: Kwanza, humuwezesha mja kufikia lengo la kuumbwa kwake. Tumeona kuwa elimu imekuwa faradhi ya kwanza kwa waumini kwa kuwa elimu ndio nyenzo kuu ya kuwawezesha binaadamu kufikia lengo la kuumbwa kwao ambalo ni kumuabudu Allah (s.w), ipasavyo

 

katika kila kipengele cha maisha yao. (Qur-an 51:56). Pia elimu ndio nyenzo kuu ya kuwawezesha waumini kuwa viongozi wa jamii (makhalifa wa Allah) katika ardhi. (Qur-an 2:30 - 31).

 

Elimu itakayotafutwa kinyume na kumuwezesha mtu kumuabudu Mola wake ipasavyo na kusimamisha ukhalifa wa Allah (s.w) katika ardhi itakuwa si elimu yenye manufaa bali elimu yenye kuhasirisha kama tunavyojifunza katika hadithi zifuatazo:

 


Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w)
amesema: “Anayetafuta elimu isiyokuwa kwa ajili ya
kutafuta radhi za Allah (s.w), hasomi kwa lengo lolote
lile ila la kupata maslahi ya hapa duniani tu. Huyo
siku ya kiyama hatapata hata harufu ya Pepo.”
(Ahmad, Abu Daud, Ibn Majah).

 


Pia Mtume (s.a.w) ametuasa kuwa mwenye kutafuta elimu ili awazidi wasomi wengine au ili kuitumia katika biashara za kijahili au ili kujionesha kwa watu kuwa naye ni msomi, Mwenyezi Mungu atamuingiza motoni. (Tirmidh).

 


Pili, elimu yenye manufaa kwa binaadamu hapa ulimwenguni na huko akhera ni ile ambayo pamoja na mtu binafsi kuitumia katika kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo katika maisha yake ya kila siku, huifundisha au huifikisha kwa wengine pia kwa ajili ya kutafuta radhi za Allah (s.w).

 

Ni vibaya mno mbele ya Allah (s.w) mtu kukataa au kuacha kufikisha kwa wengine kila anachokijua kama tunavyojifunza katika hadithi ifu atayo:
“Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Atakayeulizwa juu ya jambo alilojifunza kisha akaficha (akakataa kutoa elimu ile) atavalishwa mshipi wa moto katika siku ya Kiyama”. (Ahmad, Ibn Majah, Tirmidh na Abu Daud).

 


Katika hadith nyingine iliyosimuliwa na Abu Hurairah Mtume (s.a.w) amesema:
“Mfano wa elimu isiyonufaisha ni sawa na mfano wa mali iliyokusanywa bila ya kutumiwa katika njia ya Allah ”. (Ahmad, Darini).

 

Kutokana na hadith hizi tunajifunza kuwa elimu yenye kunufaisha ni ile iliyofundishwa kwa wengine kinadharia na kiutendaji. Kwa kufundisha watu unachokijua bila ya wewe mwenyewe kutenda ni mfano mbaya mno kwa wale wanaofundisha na chukizo kubwa mno mbele ya Allah (s.a.w):

 

“Enyi mlioamini mbona mnasema msiyoyatenda?) Ni chukizo kubwa mbele ya Allah (s.w) kusema msiyoyatenda.” (61:2-3)





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1044


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Maswali juu ya mtazamo wa uislamu kuhusu dini
Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Humtegemea Mwenyezi Mungu peke yake
Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu. Soma Zaidi...

Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu
Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafundisho ya Mitume
Mafundisho ya mitume ni eneo lingine linalo thibitisha kuwepo Allah (s. Soma Zaidi...

Kwanini Uislamu umeipa Elimu nafasi ya kwanza?
Soma Zaidi...

Ni nini maana ya Ilhamu katika uislamu?
Ilhamu ni moja katika njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu na kuwafundisha mambo mablimbali. Soma Zaidi...

KUAMINI SIKU YA MALIPO
Soma Zaidi...

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini kutokana na vipawa alivyooewa na Allah
Je ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya kuwa na dini?. Vipawa alivyopewa na Allahni jibu tosha juu ya swali jilo Soma Zaidi...

Nafsi ya mwanadamu inavyothinitisha uwepo wa Allah
Mwanadamu ukifikiria vyema. Kuhusu nafsi yako, hakika utapatabfikra yabuwepp wa Mwenyezi Mungu Soma Zaidi...

Nafasi ya Elimu katika uislamu
Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu. Soma Zaidi...

ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ... Soma Zaidi...

Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)
"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu Soma Zaidi...