Navigation Menu



Ni nini maana ya Talaka katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.

Maana ya Talaka
Talaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili. Baada ya kuvunja mkataba huu kwa kufuata sharia ya Kiislamu, mwanamke aliyetalakiwa huwa huru kuolewa na mume mwingine.

 


Talaka katika Uislamu
Talaka katika Uislamu si jambo Ia kupendeza. Kwa hiyo mume na mke wanatakiwa wajitahidi kusuluhishana na kuvumiliana iii hatua ya kupeana talaka isifikiwe.


Talaka ni jambo Ia halali hub ruhusiwa inapokuwa hapana budi na wala Si jambo Ia kuhifanyia mas-khara kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:

 


Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: "Katika halali inayochukiza mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) ni talaka ". (Abu Daud).

 


Kwa upande mwingine, kama Mwenyezi Mungu (s.w) angahiharamisha talaka, hali ya maisha ingahikuwaje katika famihia zile ambazo mume na mke wamekosana kiasi cha kila mmoja kutotaka kumuona mwenziwe! Kwa hiyo, mume au mke atakapofanya kosa au makosa makubwa yasiyovumihika kwa mwenziwe, Mwenyezi Mungu (s.w) ametoa ruhusa wapeane talaka na kuachana kwa wema na mapenzi kama inavyosisitizwa katika Qur-an:

 

Talaka (za kuweza kurejeana) ni mara mbili. Kisha ni kumuweka kwa wema au kumwacha kwa ihsani ... ". (2:229). Na mtakapowapa wanawake talaka nao wakafikia kumaliza eda yao, basi warejeeni kwa wema au tokaneni nao kwa wema... (2:231). Basi wanapofikia muda wao, ima warejeeni kwa wema, au farikianeni nao kwa wema... (65:2).

 


Kwakuwa ndoa ni mkataba waliowekeana mume na mke wa kuishi kwa wema na kuachana kwa wema ikibidi kuachana, hapana sababu kabisa ya kujenga chuki na uhasama kati ya wawili hawa kwa sababu tu eti wanashindwa kuuendeleza mkataba wao. Katika aya hizi tunaamrishwa kuvunja mkataba huu kwa wema kwa kufuata utaratibu aliouweka Mwenyezi Mungu (s.w) na baada ya hapo kila mmoja kuwa huru.

 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1544


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Usimamizi wa Haki na haki za binadamu Katika Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...

Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili
Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake. Soma Zaidi...

Je inafaha kuingizwa eda na kutolewa?
Kuingizwa au Kutolewa EdaKatika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh. Soma Zaidi...

NAMNA YA KUSWALI: NIA YA SWWALA, NA KUPIGA TAKBIRA (yaani kusema Allah akbar)
Mtume (s. Soma Zaidi...

Nguzo za swala.
Kipengele hiki kinaelezea nguzo mbalimbali za kuswali. Soma Zaidi...

Ni kwa nini lengo la Funga na swaumu halifikiwi na wafungaji?
Kwa nini Lengo la Funga halifikiwi na Wafungaji Wengi? Soma Zaidi...

Faida za kuswali swala za sunnah
Posti hii inakwenda kukufundisha kuhush swala za sunnah. Soma Zaidi...

Swala ya maiti, namna ya kuiswali, nguzo zake, sharti zake na suna zake, hatua kwa hatua
Soma Zaidi...

Siku ya idi al-fitir na namna ya kusherekea idi
Soma Zaidi...

Kwa nini imefaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani
Unaweza kijiuliza ni kwa nini hasa kimepelekea kufaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani. Soma Zaidi...