image

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Kuingizwa au Kutolewa Eda

Katika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh. Kizuka huanza eda baada tu ya kufariki mumewe na eda yake huisha mara tu baada ya muda wa miezi mine na siku kumi kuisha. Wala hapana vazi maalum Ia kukalia eda. Si nguo nyeupe, wala nyeusi, wala kuvaa matambara kama baadhi ya watu wanavyoitakidi. Mwanamke mfiwa atabakia nyumbani kwa mumewe au kwa warithi wa mumewe katika sitara kama kawaida anavyotakiwa awe mwanamke yeyote wa Kiislamu na ataendelea kufanya shughuli zake za nyumbani na nje ya nyumbani zilizo katika mipaka ya sheria ya Kiislamu. Wala hapana sheria yoyote ya kukaa nyumbani kivivu-vivu kama wanavyoitakidi watu wengine.
 
 
 
 
Hekima kubwa ya kuamrishwa kizuka kukaa eda, pamoja na haja ya kuangaliwa uwezekano wa kuachwa na mimba, kunampa kizuka nafasi ya kutulizana na kuliwazika baada ya kupatwa na msiba mkubwa kiasi hicho. Pamoja na kuwa mwanamke baada ya kipindi cha eda huwa huru kutoka nyumbani kwa mumewe marehemu na kuolewa na mume mwingine, akitaka kubakia katika nyumba ya mumewe pamoja na watoto wake, ana haki kisheria kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:
 
 
 
Na wale waliofishwa miongoni mwenu na wakawacha wake, wawausie (warithi wao) kwa ajili ya wake zao kupata matumizi ya mwaka mmoja bila ya kutolewa (katika nyumba za waume zao). Na kama wanawake wenyewe wakiondoka, basi si kosa juu yenu kwa yale waliyoyafanya kwa nafsi zao
 
 
 
 
wenyewe yanayofuata sharia. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu, mwenye hi/dma. (2:240).
Katika baadhi ya jamii za kijahili pamekuwa na mtindo wa kuwarithi wanawake waliofiwa na waume zao kama mali inavyorithiwa na jamaa wa marehemu. labia hii ya kumdhalilisha mwanamke na kumnyima uhuru wake wa kuolewa na mwanamume ampendaye imepigwa marufuku katika sheria ya Kiislamu kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:
 
 
 
Enyi mlioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa jeuri. Wala msiwazulie (kuolewa na waume wengine) iii mpate kuwanyang 'anya baadhi ya vile mlivyowapa (katika urithi wa waume zao...) (4:19)
 
 
 
 
Ama mwanamke mjane mwenyewe akiridhika kuolewa na ndugu au jamaa wa marehemu mumewe, ili aweze kubakia pale na watoto wake hapana ubaya ili mradi tu wafunge ndoa kama ilivyo katika sheria.
 
 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 8323


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Hali ya kuzuiliana kurithi katika uislamu
KuzuilianaTumeona kuwa wanaume wenye kurithi ni 15 na wanawake wanaorithi ni 10. Soma Zaidi...

Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani
Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku. Soma Zaidi...

Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini
Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Swala za sunnah na faida zake
Soma Zaidi...

Yanayofaa kwa maamuma katika kumfata imamu kwenye swala ya jamaa
Soma Zaidi...

Eda ya kufiwa na hukumu zake
Soma Zaidi...

walioruhusiwa kufungua (kula) mwezi wa ramadhani
Soma Zaidi...

Mambo yasiyoharibu Swaumu na Kufunguza mwenye kufunga
Soma Zaidi...

namna ya kuswali
11. Soma Zaidi...

nini maana ya hadathi na ni zipi aina za hadathi na uchafu katika uislamu
Soma Zaidi...

sadaka
Soma Zaidi...

familia
Soma Zaidi...