picha

NIMLAUMU NANI part 1

Post hii inahusu hadithi Moja ya kijana maaalufu aliyeitwa Frank, ni kijana aliyekuwa mwaminifu ila amekumbana na wasichana wengi wanamasaliti ukizingatia Frank alikuwa kijana mstaalabu na mwaminifu sana ila anafikia kufanya maamuzi magumu kufuatana na ku

"NIMLAUMU NANI"

1. Ni asubuhi Moja nzuri iliyokuwa na upepo kidogo na jua kuanza kujitokeza huku ndege wakiimba nyimbo nzuri na watu wakijiandaa kwenda makazini, ila kwa sababu Frank siku hiyo hakuwa na picha atatokea wapi kwa sababu yeye kupata kazi kwa siku ilikuwa ni majaliwa ya mwenyezi Mungu kwa sababu alitegemea vibarua Ili mkono uweze kuingia kinywani kwa hiyo siku hiyo alikuwa Hana picha na hata hajapata mtu wa kumwita kumpatia kibarua. Frank aliendelea kuvuta shuka ghafla akasikia simu ikiitia kupokea anasikia maneno makali kutoka kwa mpenzi wake Amina, ni maneno ya kusikitisha yakisema.

 

 

 

 

2. "Wewe ni mpenzi gani maskini naona huwezi kunitunza kwa hiyo chukua zako hamsini na mimi nichukue zangu hamsini kwa sababu siwezi kuishi na mvulana maskini Kama wewe" maneno haya yalimchoma sana Frank na yalimfanya ahamke kutoka usingizi na kukimbia kwenda dukani kutafuta vocha kwa ajili ya kuongea na mpenzi wake Amina, lakini Amina alimjibu hivi, " yaani wewe maskini hujanielewa sikutaki na usinifatilie na koma kwa sababu mimi sio wa kiwango chako, baada ya Frank kusikia maneno kama hayo aliumia sana na kuwa na uchungu sana kwa sababu alitegemea sana Amina kama faraja kwake, alifikilia sana akajipigapiga kichwa ,akajishauri na akaamua kwenda kwa rafiki yake James kuomba ushauri Ili kumbembeleza Amina kuendelea kuwa karibu na frank.

 

 

 

 

 

3 Basi frank aliamua kujiandaa vizuri kwenda kwa rafiki yake James kumwambia yaliyo moyoni, ingawa  Frank alikuwa na uchungu aliamua kuwa mkakamavu Ili asiweze kuonyesha uchungu kwa watu aliokutana nao kwa sababu ilimpasa kupanda daladala kwa sababu Kuna mwendo kama saa moja  hivi, Frank alikuwa kwenye kituo cha daladala anmesubiri daladala ghafla akaja gari linaendeshwa na msichana mlembo sana yule msichana akamwambia frank aingie kwenye gari ampe lift akihaidi kumfikisha pale anapoenda basi frank akakubali akapanda lile gari na alifurahi kwa sababu na nauli kwake  ilikuwa ni shida.

 

 

 

 

4. Basi frank alipokuwa kwenye gari alikuwa na uzuni, ila yule msichana aliamua kusimamisha gari Ili kujua yaliyompata Frank, basi frank akapaswa kumwambia msichana yaliyompata yule msichana akaumia sana akaamua kumpa Frank moyo na kumpatia frank number za simu Ili waje kuongea baadae basi frank akafikishwa kwa rafiki yake wakaagana na yule msichana wakapeana number za simu  basi frank alipofika kwake na James akabisha hodi hakufunguliwa akazunguka nyuma ya nyumba hakuona mtu baadae aliamua kuingia ndani mpaka chumbani kwa James ndipo aliposhutuka kuwakuta James na Amina wako kitandani wamekumbatiana.

 

Itaendelea.

 

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/10/27/Thursday - 09:45:57 pm Topic: Jamvini Main: Burudani File: Download PDF Views 2061

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

SAFARI YA MUUJIZA sehemu ya tatu

Post hii inahusu Zaidi hadithi ya safari ya muujiza ambapo ya Mungu mengi anaenda kwao na kuomba kufahamu history yake ili afahamu kuhusu wazazi weo walipo na ndugu zao walipo.

Soma Zaidi...
WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 1

Post hii inahusu zaidi hadithi mpya na nzuri inayoitwa wakati wa Kufumbuka, ni hadithi inayohusu maisha ya kawaida ambapo watu ushindwa kudhamini watu wa karibu nao na kuona watu wa mbali ndio wenye maana ila shida zikifika ndipo wanaona umuhimu wao.

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA ( SEHEMU YA PILI)

Post hii ni mwendelezo wa hadithi ya safari yenye muujiza ,ni pale mtoto ya Mungu mengi anafika kwenye kituo Cha ntonga na kuona yake mazingira na kufahamu njia ya kwenda kule.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili

Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine.

Soma Zaidi...
SAFARI YA MUUJIZA

Post hii inahusu hadithi moja iliyotokea Kwa mama mmoja mwenye familia ya watoto watano.ambapo mama aliolewa na mwanaume mwenye maambukizi ya virus vya ukimwi na kupata watoto bila maambukizi kusambaa kutoka Kwa baba kwenda Kwa mama.

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano, baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kuona udhaifu wake kwamba anapenda sana mali.

Soma Zaidi...
WAKATI WA KUFUMBUKA

Post hii ni mwendelezo wa hadithi inayohusu Kufumbuka ambapo , John anaonekana kama sio mtoto wa Mzee maganga kwa sababu na miungu imekili kwa sababu chakula chote kimeliwa na kuisha.

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya kwanza)

Post hii inahusu zaidi vijana wawili ambao ni msichana na mvulana walioingia kwenye mahusiano wakiwa sekondari na wakahaidiana kuoana ila kwa sababu mbalimbali walizokutana nazo kwenye safari yao ya mahusiano mmoja akamsaliti mwingine na kusababisha kupo

Soma Zaidi...
Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme (sehemu ya nne)

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.

Soma Zaidi...
USALITI (sehemu ya tatu)

Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya ukweli ambayo imetokea siku sio nyingi jinsi Moses alipoacha kumwoa Rhoda naye akachanganyikiwa takribani miaka kama mitano hivi.

Soma Zaidi...