Nini maana ya protini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya protini

NINI MAANA YA PROTINI

 

Protini ni chembechembe zinazotokea kwa njia ya asili (bila ya kutengenezwa) na zimetokana na asidi za amono (amino acid) zilizounganishwa kwa kutupia bondi za peptide. Neno protini asili yake ni lugha ya Kigiriki ”proteios” likiwa na maana ya kuwa ni kitu kinachopewa nafasi ya kwanza. Yaani protini ni viinilishe “nutrients” ambazo ni muhimu sana mwilini kuliko viinilishe vingine. Neno hili limeanzaka kutumiwa karne ya 19 mwaka 1838 na Mkemia kutoka Swedih Jöns Jacob Berzelius.

 

Protini huweza kutofautiana namna zilivyo kutoka kiumbe kimoja na chingine, pia protini huweza kutofautiana kutoka kiungo kimoja kwenda kingine. Kwa mfano protini za kwenye macho ni tofauti na zile za kwenye moyo, ini na figo. Kila kiumbe hai kina protini, na pia protini huhusika katika michakato tata kwenye miili ya viumbe hai, kwa mfano protini huhusika katika kutengeneza antibodies ambazo hutengeneza kinga na kupambana na maradhi na wadudu shambulizi kama bakteria na virusi. Protini hutengeneza enxymes ambazo ndizo hutumika katika kumeng’enya chakula. Pia protini hutengeneza homoni (hormones)

 

Baada ya kukila chakula chenye protini chakula kinaanza kumengenywa kinapofika kwenye tumbo na utumbo, kisha hufyonzwa kwenye utumbo mdogo na kuingia kwenye mirija ya damu. Pindi chembechembe za protini zinapoingia kwenye damu, damu huanza kusafirisha protini kwenda maeneo mbalimbali ya mwili yanayohitajia protini. Huko protini zitaingia kwenye seli za mwili. Ndani ya seli mchakato kwa kuvunjwa vunjwa protini ili kutumiwa zaidi hufanyika. Ndani ya seli mchakato huu jhufanyka kwenye sehemu inayotambulika kitaalamu kama ribosomes

 

Miili ya wanyama haina uwezo wa kuhifadhi protini kwa matumizi ya baadaye. Hivyo kama mtu atakula protini nyingi, mwili utaibadili protini kuwa fati na baadaye kutumika kutengeneza nishati ndani ya mwili. Na endapo mtu hataweza kupata protini za kutosha mwili utaanda kuangalia maeneo yenye protini ndingi kama misuli, kisha mwili utaanza kuvunja protini iliyomo mule na kuipeleka maeneo mengine na hapa mtua ataanza kukonda na kupoteza nyama na hatimaye kufariki kama hatapata chakula chenye protini.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-03     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2081

Post zifazofanana:-

Ugonjwa wa kuharisha na sababu zake.
Kuharisha ni Hali ya kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisicho na damu Soma Zaidi...

Faida za kula tikiti
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula tikiti Soma Zaidi...

Timu ya simba ina miaka 87 sasa toka kuanzishwa
Kutokea kuitwa Sunderland mpaka Simba, timu hii ilianzishwa mwaka 1936 Soma Zaidi...

Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu
Ni zipo njia wanazotumia Allah katika kuwasiliana na kuwafundisha wanadamu? (EDK form 1: Dhana ya elimu katika Uislamu). Soma Zaidi...

Walio kwenye hatari ya kupata UTI
Posti hii inahusu zaidi watu walio kwenye hatari ya kupata UTI, ni watu ambao wako kwenye hatari ya kupata ugonjwa wa UTI kwa sababu ya mazingira mbalimbali kama ifuayavyo. Soma Zaidi...

Sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa
Post hii inahusu zaidi sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa,ni sababu ambazo uweza kuchangia kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa. Soma Zaidi...

Dalili za Ugonjwa wa Ebola.
Virusi vya Ebola ni virusi vinavyohusiana vinavyosababisha Homa za'hemorrhagic magonjwa yanayoambatana na kutokwa na damu nyingi (kuvuja damu), viungo kushindwa kufanya kazi na, mara nyingi, kifo. Virusi vya Ebola na virusi huishi kwa wanyama, na wanad Soma Zaidi...

Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)
Nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Dalili za mimba inayotishi kutoka
Posti hii inahusu zaidi dalili za mimba inayotaka kutoka yenyewe, Kuna wakati mwingine mama anabeba mimba na mimba hiyo I atishia kutoka na huwa inaonyesha dalili mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni dalili za mimba kutaka kutoka yenyewe. Soma Zaidi...

Fahamu Ugonjwa wa hepatitis A
Hepatitis A ni ugonjwa wa kuambukiza wa ini unaosababishwa na virusi vya Hepatitis A. Virusi ni mojawapo ya aina kadhaa za virusi vya Hepatitis vinavyosababisha kuvimba na kuathiri uwezo wa ini wako kufanya kazi. Soma Zaidi...

Sanda ya mwanaume na namna ya kumkafini
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Namna ya kugundua mtu mwenye kaswende.
Post hii inahusu zaidi njia za kumgundua mgonjwa wa kaswende, njia hizi utumika baada ya kuongea na mgonjwa kuhusu maisha yake hasa kujamiiana na watu mbalimbali. Soma Zaidi...