Njia za jumla za kujikinga na magonjwa mbalimbali
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona
Njia za kujikinga na magonjwa.
1. Njia ya kwanza ni kufanya usafi wa mazingira,kufanya usafi wa binafsi yaani kuoga, kufua nguo, kukata kucha, kusafisha meno, kunywa maji safi na salama na mambo hayo ya kuhakikisha mwili unakaa kwenye hali ya usafi kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa,na pia kwa upande wa mazingira, kukata nyasi zilizozunguka makazi , kumchoma takataka,kutunza uchafu sehemu Moja na kutoruhusu kuishi sehemu Moja na wanyama, yaani kuwatengea wanyama sehemu yao kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa.
2. Kupata kinga ya mwili.
Kwa upande wa kupata kinga ya mwili ni pamoja na kupata chanjo zote zinazohitajika mwilini hasa hasa kwa watoto kwa kufanya hivyo tunazuia magonjwa ambayo yanaweza kutokea hapo mbeleni,kwa mfano kupata chanjo ya kifua kikuuu, kupata chanjo ya kuzuia kupooza, kupata chanjo ya kuzuia kuharisha kupata chanjo ya pepo punda na chanjo zote za lazima kwa mtoto na kwa mabinti wanaotegemea kubeba mimba kupata chanjo zinazohitajika Ili kuepuka magonjwa mbeleni. Kwa kuweka mwili katika hali ya kinga ni vigumu kupata magonjwa.
3. Kula mlo kamili.
Kuna msemo usemao kwamba chakula Bora ni dawa, kwa sababu mlo ukiwa kamili na kutosha ni vigumu sana kupata magonjwa, kwa mfano aina zote za vyakula zikiwa sawia ni vigumu kupata magonjwa kwa mfano matumizi mazuri ya vyakula vya wanga, protein, mafuta kidogo na mboga za majani za kutosha na kunywa maji kulingana na uzito wako kwa kufanya hivyo ni vigumu kupata magonjwa, lakini Kuna tabia ambayo watu wanapendelea aina Moja ya vyakula hasa vyakula vya madukani vilivyojaa kemikali na mafuta kwa wingi sukari wakitegemea kupata afya njema kwa kufanya hivyo matokeo yake ni kinenepeana na kuwa na vitambi hatimaye magonjwa ya presha na mengine mengi tu. Kwa hiyo kula mlo kamili ni kujikinga na magonjwa.
4. Kuangalia afya Yako mara kwa mara.
Kitendo cha kuangalia afya mara kwa mara nayo ni hatua Moja kubwa kwa sababu unaweza kukuta Kuna ugonjwa upo na ujautibu au kwa wakati mwingine ukikutwa na presha labda inaelekea kuwa juu unarekebisha mtindo wa maisha au ukikuta sukari ni kubwa unapunguza kiwango cha sukari kwa kufanya hivyo ni vizuri kabisa kuepuka na magonjwa au kwa vijana ni vizuri kabisa kupima maambukizi na magonjwa ya zinaa ikitokea kuna ugonjwa ni kuanza dawa mapema Ili kuweza kuepukana na matatizo mbalimbali ambayo ni pamoja na ugumba kama Kuna zinnia Kali au kuepuka kinga ya mwili kushuka kama Kuna maambukizi ya virus vya ukimwi.
5. Elimu kutolewa kila mara.
Kwa kupitia watu mbalimbali kwa lengo la kutoa elimu ni jambo zuri na la busara kwa sababu pengine Kuna mlipuko Fulani wa magonjwa jamii ikijulishwa mapema na kuweza kujikinga na kufuata mashart au tiba kama ipo ni vigumu kupata magonjwa kwa hiyo viongozi wa jamii wawe tayari kutoa elimu kwa waliowazunguka Ili kuzuia kuongezeka kwa magonjwa.
6. Kutibu magonjwa kama yapo.
Njia nyingine ya kupunguza magonjwa ni pamoja na tiba kama Kuna ugonjwa Fulani kwenye jamii ni vizuri kutibu ugonjwa huo Ili kuepuka kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa sababu Kuna watu wenye kinga ya hali ya juu ana ugonjwa ila haoneshi dalili ni vizuri kutoa ushauri na kuhakikisha kuwa ugonjwa unatibika kwa watu wenye hali ya hivyo.
7. Kutumia dawa endapo Kuna maambukizi.
Ni vizuri kabisa na jambo zuri kutumia dawa ikiwa umefanya vipimo na kugundulika una maambukizi kwa mfano watu wenye maambukizi ya virus vya ukimwi ni vizuri kabisa kutumia dawa na wasione aibu kabisa kwa sababu wasipotumia dawa wanaweza kuwa na magonjwa nyemelezi yanayosababisha afya zao kuyumba.
8. Kwa hiyo kuzuia kupatwa na magonjwa ni kazi inayoweza kufanikiwa zaidi kwa kuhakikisha mazalia ya wadudu wanaosambaza magonjwa kuharibiwa kwa mfano kujaribu mazalia ya mbu, nzi na wadudu wote ambao tnajua kazi zao ni kusambaza magonjwa tunaweza kutumia njia zozote pamoja na kutumia dawa za madukani za kuua wadudu.
9. Kwa hiyo kwa kufanya hayo yaliyojadiliwa magonjwa yanaweza kupungua au yasiwepo kabisa kwa sababu magonjwa yanakuwepo kwenye jamii kwa sababu ya kutozingatia tuliyoyajadili ambayo ni kutokula mlo kamili, tabia ya kutoangalia afya zetu, kushindwa kutumia dawa baada ya vipimo,kutofanya usafi kwenye mazingira yetu,kuishi na wadudu wanaosababisha ugonjwa na mambo mengine kama hayo, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuziangatia hayo Ili tuwe mbali na magonjwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 web hosting 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Mabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo za mimba
Wiki za kwanza za ujauzito ni kipindi cha mabadiliko makubwa ya ndani na nje ya mwili wa mwanamke. Makala hii inafafanua mabadiliko hayo ili kumsaidia mama kuelewa kinachoendelea na jinsi ya kukabiliana na hali hiyo kwa usalama.UtanguliziWakati mwingine, mabadiliko ya mwili huanza kujitokeza hata kabla hujapima na kupata majibu chanya ya mimba. Hii inatokana na msukosuko wa homoni unaolenga kutengeneza mazingira rafiki kwa ukuaji wa kiumbe kilichotungwa. Kuelewa dalili hizi ni muhimu ili uweze kujijali na kumpa mtoto wako nafasi nzuri zaidi ya ukuaji kuanzia siku ya kwanza.Maudhui: Mabadiliko ya Mwili katika Wiki za MwanzoKatika kipindi hiki, mwili wako unafanya kazi kubwa kurekebisha mfumo wake:Mabadiliko ya Homoni: Kiwango cha homoni za estrogen na progesterone hupanda kwa kasi ili kusaidia ujauzito, hali inayoweza kubadili hisia zako (mood swings).Mabadiliko katika Matiti: Matiti yanaweza kuwa makubwa, mazito, na yenye maumivu mepesi kutokana na kuongezeka kwa mtiririko wa damu na kujiandaa kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa.Mabadiliko ya Mfumo wa Chakula: Unaweza kuhisi kichefuchefu, hasa asubuhi, au kupata mabadiliko ya ladha (kuchukia vyakula fulani ulivyokuwa unapenda awali).Uchovu: Mwili hutumia nishati nyingi katika wiki za mwanzo kuunda mfumo wa kondo la nyuma (placenta), hali inayokufanya uhisi uchovu na usingizi wa mara kwa mara.Kukojoa Mara kwa Mara: Uterasi inapoanza kukua na shinikizo la damu kuongezeka, kibofu cha mkojo hupata shinikizo zaidi, jambo linalokufanya utake kwenda chooni mara kwa mara.Fact Check: Je, mabadiliko haya ni hatari?Ukweli: Mabadiliko mengi unayoyahisi ni ya kawaida kabisa na ni ishara kuwa mwili wako unakubali ujauzito. Hata hivyo, si kila mwanamke anapata dalili hizi zote.Tahadhari: Ikiwa utapata dalili hizi, unapaswa kuonana na daktari mara moja:Maumivu makali ya tumbo (upande mmoja au sehemu ya chini).Kutokwa na damu nyingi ukeni (vaginal bleeding).Homa kali au maumivu wakati wa kukojoa.Kutapika sana kiasi cha kushindwa kuhifadhi maji mwilini.HitimishoMabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo ni ishara ya maajabu ya kimaumbile yanayotokea ndani yako. Ingawa baadhi ya hali hizi zinaweza kuwa kero, kumbuka kuwa ni za muda mfupi. Kula mlo kamili, kunywa maji ya kutosha, na kupumzika ipasavyo kutakusaidia kupitia kipindi hiki kwa urahisi zaidi. Usisahau kuhudhuria kliniki mapema ili kupata ushauri wa kitaalamu na ufuatiliaji wa ukuaji wa mtoto wako
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kitovuni
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya tumbo kitovuni
Soma Zaidi...Matibabu ya mba na fangasi za ngozi kwa kutumia dawa za hospitali.
Fangasi za ngozi ni changamoto ya kiafya inayomkabili mtu yeyote, ikijidhihirisha kwa njia ya mba (tinea versicolor) au maambukizi mengine ya ngozi. Makala haya yanatoa uchambuzi wa kitaalamu kuhusu dawa za kisasa zinazotolewa hospitalini, umuhimu wa utambuzi sahihi, na jinsi ya kufuata itifaki ya matibabu ili kupata matokeo ya kudumu na kuepuka usugu wa vimelea.
Soma Zaidi...Sababu za wanawake kuwa na maumivu kwenye kiuno
Posti hii inahusu zaidi sababu za wanawake kuwa na maumivu kwenye viungo, ni ugonjwa unaowapata na wanaume ila kwa wanaweza unaowapata sana ukilinganisha na wanaume.
Soma Zaidi...Dalili za UTI upande wa wanawake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanawake
Soma Zaidi...Dalili za Mimba Baada ya Ovulation
Kipindi cha baada ya yai kupevuka (ovulation) na kabla ya siku zako za hedhi kutarajiwa (drip-wait period) ni kipindi cha kusisimua kwa mwanamke anayetafuta mtoto. Makala hii inaelezea dalili za mapema ambazo mwili unaweza kuzionyesha mara baada ya yai kurutubishwa na kupandikizwa kwenye mji wa mimba, yakikusaidia kuelewa mabadiliko ya kibaolojia yanayoendelea.
Soma Zaidi...