picha

NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W)

Zifuatazo ni njia nyingi za kumjua Mwenyezi Mungu (EDK form 2:dhana ya elimu katika uislamu)

 NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W).

Njia za Kumtambua Mwenyezi Mungu (s.w).

Nafasi ya Fitrah (maumbile).

- Kila Mwanaadamu amepandikizwa hisia za kimaumbile zinazomtambua Mungu kupitia ujuzi wa kutambua mema na maovu.

 

- Mwanaadamu akipatwa na raha au misukosuko na huzuni hukiri uwepo wa Mwenyezi Mungu (s.w).

Rejea Quran (17:67), (30:30) na (91:7-8).

 

Vipaji vya Binaadamu.

- Vipaji vya akili na milango ya fahamu na fani zingine za elimu ni nyenzo pekee zikitumiwa vilivyo humuwezesha mtu kumjua Mola wake.

Rejea Quran (3:190-191), (35:28).

 

Nafsi ya mwanaadamu.

- Mfumo mzima wa mwili wa mwanaadamu na utendaji wake wa kazi wa ajabu wa viunge mbali mbali vya mwili kama kuyeyusha chakula tumboni, msukumo wa damu mwilini, n.k. ni ishara tosha juu ya uwepo wa Mwenyezi Mungu (s.w).

Rejea Quran (51:20-21) 

 

Mazingira.

- Utegemezi na uhusiano wa kimahitaji ya kutumia rasilimali ya kuishi kati ya mimea, wanyama na binaadamu (ecological balance).

 

- Maumbile mengine kama mbingu, ardhi na yote yanayoonekana na yasiyooneka katika mazingira yanayotunguka.

Rejea Quran (3:190).

 

Wahyi (Ufunuo).

- Wahyi ndio nyenzo kuu ya kumwezesha mwanaadamu kumtambua Mwenyezi Mungu (s.w) kwa usahihi unaotakikana.

 

- Elimu, vipaji na ujuzi au sayansi pekee haviwezi kumwezesha mwanaadamu kumtambua Mungu kwa baadhi ya maeneo, mfano nguzo za imani, n.k.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 3238

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 web hosting    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Ni Ipi Elimu yenye manufaa

Elimu inaweza kugawanyika katika makundibmrngine mawili ambayo ni elimu yenye manufaa na elimubisiyi na manufaa

Soma Zaidi...
Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah

Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio.

Soma Zaidi...
Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu

Mahusiano kati ya elimu ya mwongizo na elimu ya mazingira katika uislamu.

Soma Zaidi...
Mwanadamu hawezi kuishi bila dini kutokana na vipawa alivyooewa na Allah

Je ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya kuwa na dini?. Vipawa alivyopewa na Allahni jibu tosha juu ya swali jilo

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotaja katika surat An-Nisaa (4:60-63, 88, 138-145)

Huwaoni wale wanaodai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako?

Soma Zaidi...
Maana ya muislamu.

Kwenye kipengele hichi tutajifunza ni nani muislamu.

Soma Zaidi...