image

Njia za kumsafisha Mama aliyetoa mimba.

Post hii inahusu njia safi za kumsafisha Mama ambaye ametoa mimba au mtoto amefia tumboni.

Njia  za kumsafisha Mama ambaye ametoa mimba au mtoto amefia tumboni.

1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni kwamba njia hii utumika kumsafisha Mama kwa kutumia vyuma kawaida mimba ikiwa chini ya miezi minne au wiki kumi na mbili njia hii I aweza kutumika na pia wanaopaswa kuitumia ni wataalamu wa afya sio wake wanaotoa mimba ki magendo ni dhambi kwa Mungu na taifa pia .

 

2. Kwanza kabisa unapaswa kuandaa vifaa muhimu ambavyo vitaweza kutumika na pia viwe vimepitishwa kwenye usafishwaji wajoto la hali ya juu Ili kuweza kuondoa wadudu ambao wanaweza kuleta madhara baada ya kumsafisha vifaa hivi vinapaswa kutumiwa na wataalamu wa afya tu na sio wale wanaotoa mimba kinyume na utaratibu wa sheria za serikali na ki maadili.

 

3. Pia mwelezee mama kitu kinachopaswa kufanyika kama ni kumsafisha kwa sababu ya mimba inayotaka kutoka au ni kwa sababu ya kutoa mtoto aliyefia tumboni, pia mama naye anapaswa kukupatia ruhusa ya kufanya hivyo na pia familia inapaswa kuelezea kila kitu kinachoendelea na kuweza kushirikiana nawe kwenye kazi hiyo.na pia pakitokea shida yoyote unapaswa kuwaeleza familia na ndugu wa mama na mama mwenyewe.

 

4. Kabla ya kuanza kazi unapaswa kufunua sehemu muhimu ambazo unapaswa kufanyia kazi sio kumfunua mama mzima  hapo unakuwa umekosea maadili ya kazi, pia mama anapaswa kufunikwa vizuri na vitambaa maalum ambavyo kwa kitaalamu huitwa drape, hivi vitambaa Vimo kila kituo cha afya na pia kwenye hospitali kubwa vipo kabisa.pia wakati wa kazi ikitokea vikachafuka ni vizuri kabisa kuviweka sehemu maalumu na kuweza kumwekea mama vitambaa vingine na kazi inaendelea.

 

 

5. Hakikisha kwamba vifaa vyako ambayo unataka kuviweka kwenye uke ili kuweza kutoa kichanga unaviweka vizuri ili kuweza kuepukana na uharibifu kwenye sehemu mbalimbali za via vya uzazi, hakikisha unaviweka sawa pia wakati wa kutoa mimba iliyoharibika ni vizuri kumpiga mama sindano ya ganzi kwa sababu maumivu ni makubwa mno, kwa hiyo namna ya kuweka vifaa inapaswa kuwa sawa ili kuweza kuepukana na uharibifu wowote wa via vya uzazi.

 

 

6. Pia unapaswa kusafisha sehemu zote za via vya uzazi kuanzia kwenye sehemu za uke zote kwa kuua bakteria ambao wakiingia ndani wanaweza kuingiza maambukizi, pia na msafishaji anapaswa kuwa makini kwa kuvaa sterile gloves ambazo zinazuia kuingiza uchafu kwenye mwili wa mama na kuzuia magonjwa ambayo yanaweza kutoka kwa mama kwenda kwa mtoa huduma, magonjwa sugu ambayo yanaweza kusambaa ni homa ya nini pamoja na maambukizi ya Ukimwi.

 

 

7. Baada ya kusafisha na kuweka vyuma kwenye sehemu husika unapaswa kuvuta uchafu wote kutoka kwa Mama na hakikisha uchafu wote unaisha kabisa na kuhakikisha na damu yote inaisha na pia kama mama ana maumivu unapaswa kumpatia dawa ya maumivu ili aweze kutulia.

 

 

8. Baada ya hapo unapaswa kumshauri Mama na kumwambia mda mzuri wa kubeba mimba ili kuweza kuepukana na matatizo ya mimba kutoka mara kwa mara na kama mimba imetoka zaidi ya mara moja ni vizuri kabisa kutafuta sababu ya kutoka kwa mimba.

 

 

9. Pia ndugu jamaa na marafiki wote wanapaswa kuwa pamoja na mama ili kuweza kumtunza mama katika kipindi chote mpaka atakapofikia wakati wa kubeba mimba nyingine, na pia jamii inapaswa kuacha mila mbaya na desturi za kuona kwamba kutoa mimba ni mkosi kwa jamii.

 

 

10. Kwa hiyo mama baada ya kutoka kwa mimba anapaswa kwenda hospitali ikiwa amepata shida yoyote ya kiafya hata kama hana mtoto kwa sababu changamoto anazozipata Mama baada ya kujifungua na aliyetoa mimba anaweza kupata hizo hizo.

 

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1203


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Fahamu matatizo yanayowapata watoto waliozaliwa kabla ya wakati au mapema (premature)
Kuzaa kabla ya wakati ni kuzaliwa ambayo hufanyika zaidi ya wiki tatu kabla ya kuzaliwa kwa mtoto au kuzaliwa mapema ni moja ambayo hutokea kabla ya mwanzo wa wiki ya 37 ya ujauzito. Kawaida, ujauzito hudumu kama wiki 40. Soma Zaidi...

Malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama.
Posti huu inahusu zaidi malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama, ni huduma muhimu ambazo zimetolewa kwa akina Mama ili kuweza kuepuka hatari mbalimbali zinazowakumba akina Mama wakati wa ujauzito, kujifu na malezi ya watoto chini ya miaka mitano. Soma Zaidi...

Samahani naomba kuhuliza je unaweza kutokwa na maji maji ambayoa ayana rangi Wala harufu Ni dalili gani kwa mimba ya mwezi mmoja
ukiwa na ujauzito unaweza kuona mabadiliko mengi katika mwili wako yakiwemo kutokwa na majimaji. je majimaji haya yana dalili gani kwenye ujauzito? Soma Zaidi...

Magonjwa madogo madogo kwa Mama wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi magonjwa madogo madogo kwa akina Mama wajawazito, ni magonjwa ambayo hayawezi kupelekea kupoteza maisha kwa Mama mjamzito, magonjwa haya upotea ikiwa Mama atajifungua. Soma Zaidi...

Dalili za mimba ya mtoto wa kiume ama mtoto wa kike
Posti hii inakwenda kukueleza jinsi ya kuwjuwa kama mtoto ni wa kike ama wa kiume. Soma Zaidi...

Sifa za siku za kupata mimba
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya sifa za siku za kupata mimba Soma Zaidi...

Nguzo kuu za umama katika umri wa kupata watoto na kulea watoto
Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k Soma Zaidi...

Nna mimba ya miez miezi mitano 5 naruhusiwa kula papai kwa wing
Miongoni mwa matunda yenye virutubisho vingi ni pamoja na papai, nanasi, tikiti, palachichi, pera, karoti, hindi na boga. Lakini katika matunda haya yapo ambayo kwa mimba changa anatakiwa awe makini, kama papai na nanasi. Sasa vipi kuhusu mimba ya Soma Zaidi...

UTARATIBU WA KULEA MIMBA
Soma Zaidi...

Niharisha siku ya pili baada ya tendo. Jana hadi leo sijapata choo inawezakua nimeshika ujauzito?
Hivi unadhani kuharisha ni katika dalili za mimba, vipi kuhusu kutopata choo pia inaweza kuwa ni ujauzito? Soma Zaidi...

Je, mwanamke anapataje Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi PID?
Posti hii inaelezea namna mwanamke anavyoweza kupata Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi. Soma Zaidi...

Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa?
Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa. Soma Zaidi...