Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuz

Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito.

1.Kuwapatia wajawazito neti pindi wanapoanza mahudhurio ya kliniki.

Hii ni mojawapo ya njia ambayo inafanya kila mahali nchini ambapo kila mwanamke mwenye mimba akija kuanza mahudhurio ya kliniki anapewa neti ili aweze kulala ndani yake wakati wa usiku na kuzuia mbu wanaoeneza Malaria wasimpate akilala ndani ya neti, kw hiyo akina Mama wale wazembe wa kuhudhuria kliniki mnapaswa kwenda ili kuepukana na Ugonjwa wa Malaria.

 

2.Pia kuna watu wenye mila potofu wakipewa neti badala ya kuitumia wakati wa kulala wanaitumia kufugia kuku na kufunika mazao ili yasiliwe na wadudu kwa hiyo elimu ni ya msingi kwa jamii ili kuepuka vitu vya namna hivyo na wanaofanya mambo kama haya wanapaswa kuchukuliwa na sheria kwa sababu hizi neti ni bajeti ya serikali.

 

3.Na njia nyingine ni kutoa dawa za SP kila mwezi pale ambapo Mama anakuja kwenye mahudhurio ya kliniki. Kila mwezi kwenye vituo vyote akina Mama upewa dawa za SP lengo ni kuzuia wadudu wanasababisha malaria kutofikia mtoto, maana dawa hizi ukaa karibu na plasenta ikitokea mdudu amefika uweza kuuawa na hawezi kupata Malaria, kwa hiyo akina Mama wanaoanza kliniki wakiwa na miezi sita hawapati dawa hizi kwa wakati kwa hiyo wanaweza kuwa katika hatari ya kupata Maambukizi.

 

4.Kuna baadhi ya mila na desturi za watu wakipewa dawa hizo uleta visingizio wakidai watatumia wakiwa njiani eti zinawasumbua na wakienda nyumbani hawatumii wanatumia madawa ya kienyeji hali hii usababisha mama kujifungua mtoto mfu au mimba kutoka, kwa hiyo hakina Mama jaribu kujali maisha yenu na watoto pia nenda kliniki kwa wakati, tumia kila dawa ipasavyo na nakuhakikishia utajifungua salama achana na mila na desturi za zamani maisha yamebadilika kuna magonjwa mengi na vitu vingi kwa hiyo okoa maisha yako na mtoto wako.

 

5.Njia nyingine ni kupima Malaria kwa wajawazito pindi tu wanapoanza mahudhurio ya kliniki, hii inatumika kila sehemu ambapo wanawake wanapoanza kliniki kati ya vipimo vinavyopikwa na Malaria nayo imo kwa kuft hivyo ni kutafuta njia ili kutokomeza ugonjwa huu. Kwa hiyo akina Mama wale wazembe wa kuhudhuria kliniki Malaria ipo na inaweza kumshika mjamzito na kusababisha madhara makubwa kama vile mimba kutoka na kuzaa mtoto mfu, kwa hiyo acha uvivu nenda kliniki



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/02/08/Tuesday - 09:59:27 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 642


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Endapo nina dalili za mimba na nikipima sina mimba, je, tatizo ni nini?
dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba. Soma Zaidi...

Samahani nauliza mjamzito akiwa na presha140/90 Kuna madhara?
Presha ya kupanda hypertension huweza kuzumbuwa watu kwa jinsia zote, na umri wote. Wajawazito pia wamekuwa wakisumbuliwa na presha hii mara kwa mara. Soma Zaidi...

Maji ya Amniotic
Posti hii inahusu zaidi maji ya Amniotic ni maji ambayo uzunguka mtoto na kufanya kazi mbalimbali kama ifuayavyo. Soma Zaidi...

Faida za Uzazi wa mpango
Posti hii inazungumzia Faida za Uzazi wa mpango kwa watoto, mama, wanandoa, na jamii au JUMUIYA. Soma Zaidi...

Dalili na sababu za Kukosa hedhi
Post hii inaongelea kuhusiana na Kukosa hedhi ambapo kitaalamu hujulikana Kama Amenorrhea ni kutokuwepo kwa hedhi - hedhi moja au zaidi ya kukosa. Wanawake ambao wamekosa angalau hedhi tatu mfululizo wana amenorrhea, kama vile wasichana ambao hawajaanz Soma Zaidi...

Namna ya kumtunza mtoto aliyezaliwa
Post hii inahusu zaidi namna ya kumtunza mtoto mchanga aliyezaliwa, ni njia zitoleeazo na wakunga Ili kumtunza mtoto mchanga aliyezaliwa. Soma Zaidi...

Je inaweza ukaingia period wakati unaujauzito?
Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi? Soma Zaidi...

Njia za uzazi wa mpango kwa akina Mama kuanzia miezi sita baada ya kujifungua mpaka mwaka mmoja
Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango kwa mama aliyejifungua kuanzia miezi sita mpaka mwaka mmoja. Soma Zaidi...

Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.
Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h Soma Zaidi...

Sababu za kutoka kwa mimba na dalili zake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kutoka kwa mimba na dalili zake Soma Zaidi...

Nahitaji kufaham siku ya kumpatia mimba make wangu, yeye hedhi yake ilianza talehe22
Je na wewe ni moja kati ya wake ambao wanahitajivkujuwa siku za kupata mimba. Ama siku za competes mwanamke mimba. Post hii ni kwa ajili yako. Soma Zaidi...

Je matiti kujaa na chuchu kuuma inakua ni dalili za hedhi?
Kuunda na kujaa kwa matiti ni miongoni mwa dalili za ujauzito lakini pia ni dalili za kukaribia hedhi kwa baadhi ya wanawake. Posti hii itakwenda kufafanuabutofauti wa dalili hizi na kipi ni sahihibkatibya hedhi ama ujauzito. Soma Zaidi...