Njia za kuzuia mimba zisiharibike.
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuzuia mimba zisiharibike, kwa sababu kila mama anayebeba mimba anategemea kupata mtoto kwa hiyo na sisi hamu yetu ni kuhakikisha kwamba mtoto anazaliwa kwa kuzuia mimba kuharibik
Njia za kuzuia mimba zisiharibike
1. Njia ya kwanza ni kuepuka matumizi ya pombe, dawa za kulevya na kuvuta sigara.
Hizi ndizo njia ambazo Usababisha mimba kutoka kwa sababu baadhi ya vilevi ni vikali na kuwepo kwa nicotine usababisha kuharibika kwa mimba.
2. Fanya mazoezi mepesi mepesi.
Kwa kufanya mazoezi hayo usababisha ukuaji mzuri wa kichanga ila mazoezi makubwa makubwa achana nayo hasa kufanyanya kazi nzito ambazo Usababisha mimba kutoka unapaswa kuepukana nayo ili kuweza kuepuka na matatizo ya kutoka mimba.
3. Jikinge na Maambukizi mbalimbali hasa kwenye via vya uzazi.
Wakati wa ujauzito ni vizuri kabisa kujikinga na kuwepo kwa magonjwa kwenye via vya uzazi kwa sababu yanaweza kusababisha maambukizi.na kusababisha mimba kutoka kwa hiyo na siku zote epuka kujamiiana na wanaume wengi au mbalimbali wakati wa ujauzito ili kupunguza magonjwa.
4. Na pia wakati wa ujauzito ni vizuri kuepuka kutumia sabuni za kunukia kusafisha uke daima tumia sabuni ya kawaida kwa sababu kuna hatari ya kuua bakteria wazuri wa kulinda uke na kusababisha Maambukizi kwenye via vya uzazi na kusababisha mimba kutoka.
5. Punguza matumizi ya vyakula visivyofaa.
Kwa kawaida kuna vyakula ambavyo havifai wakati wa ujauzito ni pamoja na vyakula vyenye kiwango kikubwa cha caffeine kwa mfano kahawa na matumizi ya mara kwa mara ya soda .
6. Tumia mlo kamili wakati wa ujauzito.
Kwa kawaida mlo kamili unatakiwa wakati wa ujauzito ni pamoja na vyakula na mboga mboga za majani na pia matumizi ya vyakula vyenye madini ya chuma kwa wingi kwa kufanya hivyo tunaweza kupunguza kiwango cha mimba kuharibika.fs
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 web hosting 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?
Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?
Soma Zaidi...Fahamu Ute unaotoka wakati wa ujauzito
Posti hii inahusu zaidi Ute unaotoka wakati wa ujauzito, kwa kawaida wakati wa ujauzito Kuna Ute ambao utoka na ni tofauti na kawaida pale mwanamke akiwa Hana mimba.
Soma Zaidi...Dalili za mimba kutoka.
Post hii inahusu zaidi dalili za mimba kutoka, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mimba zote ambazo utaka kutoka kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Dalili za kupata uvimbe kwenye kizazi (fibroid)
Post hii inaenda kufundisha kuhusiana na uvimbe wa kizazi kwa wanawake. Uvimbe wa kizazi no uvimbe ambao hutokea kwenye tumbo la kizazi ambao unaweza kuwa ndan ya kizazi uvimbe huu ndan ya mwanamke hujulikana kama (uterine myoma au fibroid). Uvi
Soma Zaidi...Samahani nauliza mjamzito akiwa na presha140/90 Kuna madhara?
Presha ya kupanda hypertension huweza kuzumbuwa watu kwa jinsia zote, na umri wote. Wajawazito pia wamekuwa wakisumbuliwa na presha hii mara kwa mara.
Soma Zaidi...