picha

Njia za kuzuia mimba zisiharibike.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuzuia mimba zisiharibike, kwa sababu kila mama anayebeba mimba anategemea kupata mtoto kwa hiyo na sisi hamu yetu ni kuhakikisha kwamba mtoto anazaliwa kwa kuzuia mimba kuharibik

Njia za kuzuia mimba zisiharibike

 

1. Njia ya kwanza ni kuepuka matumizi ya pombe, dawa za kulevya na kuvuta sigara.

Hizi ndizo njia ambazo Usababisha mimba kutoka kwa sababu baadhi ya vilevi ni vikali na kuwepo kwa nicotine usababisha kuharibika kwa mimba.

 

2. Fanya mazoezi mepesi mepesi.

Kwa kufanya mazoezi hayo usababisha ukuaji mzuri wa kichanga ila mazoezi makubwa makubwa achana nayo hasa kufanyanya kazi nzito ambazo Usababisha mimba kutoka unapaswa kuepukana nayo ili kuweza kuepuka na matatizo ya kutoka mimba.

 

3. Jikinge  na Maambukizi mbalimbali hasa kwenye via vya uzazi.

Wakati wa ujauzito ni vizuri kabisa kujikinga na kuwepo kwa magonjwa kwenye via vya uzazi kwa sababu yanaweza kusababisha maambukizi.na kusababisha mimba kutoka kwa hiyo na siku zote epuka kujamiiana na wanaume wengi au mbalimbali wakati wa ujauzito ili kupunguza magonjwa.

 

4. Na pia wakati wa ujauzito ni vizuri kuepuka kutumia sabuni za kunukia  kusafisha uke daima tumia sabuni ya kawaida kwa sababu kuna hatari ya kuua bakteria wazuri wa kulinda uke na kusababisha Maambukizi kwenye via vya uzazi na kusababisha mimba kutoka.

 

5. Punguza matumizi ya vyakula visivyofaa.

Kwa kawaida kuna vyakula ambavyo havifai wakati wa ujauzito ni pamoja na vyakula vyenye kiwango kikubwa cha caffeine kwa mfano kahawa na matumizi ya mara kwa mara ya soda .

 

6. Tumia mlo kamili wakati wa ujauzito.

Kwa kawaida mlo kamili unatakiwa wakati wa ujauzito ni pamoja na vyakula na mboga mboga za majani na pia matumizi ya vyakula vyenye madini ya chuma kwa wingi kwa kufanya hivyo tunaweza kupunguza kiwango cha mimba kuharibika.fs

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 4287

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Dalili za kuvimba kwa ovari.

  Posti hii inazungumzia kuhusiana na kuvimba kwa ovari kunakosababishwa na maambukizo ya bakteria na kawaida huweza kusababishwa na magonjwa sugu katika Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi

Soma Zaidi...
CHANGAMOTO ZA UJAUZITO, NA DALILI ZAKE NA NAMNA YA KUKABILIANA NAZO

Utawezaje kukabiliana na changamoto za ujauzito, je ni zipi changamoto hizo. Hapa nitakujuza.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu fangasi za ukeni

Posti hii inahusu zaidi fangasi za ukeni, hili ni tatizo kubwa ambalo linawakumba watoto, akina dada na wanawake kwa hiyo na vizuri kujua Dalili zake na kuweza kuchukua hatua mapema.

Soma Zaidi...
Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto.

Soma Zaidi...