image

Njia za kuzuia uwepo wa ugonjwa wa Bawasili.

Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.

Njia za kuzuia kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili.

1. Njia ya kwanza ni kuhakikisha kuwa ukipata haja kubwa fanya haraka kuitoa na usisubiri mda na pia kama kuna tatizo la choo kuwa ngumu ni vizuri kutafuta matibabu ili kuweza kuepuka madhara ya uwepo wa Bawasili.

 

2. Kuachana na tabia ya kufanya mapenzi kinyume cha maumbile.

Hii ni tabia ambayo imeingia na inatumiwa na watu wengi sana hasa kwa vijana hali inayopelekea kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili na pia kuwepo kwa Maambukizi mbalimbali kwa sababu ya kulegea kwa mishipa ya haja kubwa hali inayosababisha kuwepo kwa Bawasili.

 

3. Kutibu magonjwa ya kuharisha endapo yametokea.

Kwa kawaida kuharisha kwa mda mrefu usababisha kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili kwa kufanya hivyo tutaweza kuepuka kuwepo kwa Ugonjwa huu.

 

4. Kupunguza matumizi ya vyoo vya kukalia.

Kwa wale wanaotumia sana vyoo vya kukalia wanapaswa kupunguza au kutumia njia nyingine ili kuepuka kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.

 

5. Kupunguza tabia ya kunyanyua vitu vizito.

Kwa wale ambao kazi zao mara nyingi ni kunyanyua vitu vizito wanapaswa kupunguza ili kuepuka matatizo ya gonjwa la Bawasili.

 

6. Kupunguza uzito na unene wa kupitiliza.

Kwa kawaida watu wanene na wenye uzito wa kupitiliza wako kwenye hatari kubwa ya kupata ugonjwa huu.

 

7. Kuachana na msongo wa mawazo.

Kuna watu ambao wanaweza kila siku kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo kwenye maisha yao kwa hiyo tunapaswa kuwakwaza na kutafuta kitu chochote cha kuwafanya waachane na kukaa kwenye mawazo mda wote.

 

8. Kutoa elimu kwa watu kuhusu Ugonjwa huu. Maana yake, jinsi unavotokea, madhara yake na njia za kufanya ili kuweza kutokomeza kabisa ugonjwa huu kwenye jamii.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 924


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Ugonjwa wa kuchelewa kuganda kwa Damu unaojulikana Kama hemophilia.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na tatizo la Kurithi ambapo Damu inatoka kwa muda mrefu wakati au baada ya jeraha bila kuganda. Soma Zaidi...

Ni nini husababisha mate kujaa mdomoni, na ni yapi matibabu yake
Hapa tutaangalia baadhi ya sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate na namna ya kutibu tatizo la kujaa kwa mate mdomoni Soma Zaidi...

Uvimbe wa mishipa midogo ya Damu kwenye ngozi
Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wenye uchungu wa mishipa midogo ya damu kwenye ngozi yako ambayo hutokea kutokana na ongezeko la joto la ghafla kutokana na halijoto ya baridi. Pia inajulikana kama pernio, chilblain inaweza kusababisha kuwasha, Soma Zaidi...

Ujue ugonjwa wa tauni
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa tauni ambao kwa kitaalamu huitwa plague ni Ugonjwa unaosababishwa na wadudu ambao huitwa kitaalamu huitwa yersinia pestis ambao ukaa ndani ya panya. Soma Zaidi...

Saratani ya matiti (breasts cancer)
Post yetu inaenda kuzungumzia kuhusiana na Saratani ya Matiti ni Saratani ambayo hutokea katika seli za matiti. Baada ya Saratani ya Ngozi, Saratani ya matiti ndiyo Saratani inayojulikana zaidi hugunduliwa kwa wanawake Mara nyingi. Saratani ya Soma Zaidi...

Dalili za madhara ya figo
Posti hii inahusu dalili za figo.figo husawazisha maji mwilini pamoja na kuchuja mkojo. Soma Zaidi...

Dalili za tetekuwanga
Tetekuwanga (varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, upele kama vile malengelenge. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya kawaida ya tetekuwanga, karibu watu Soma Zaidi...

ninaisi kma kunakitu kwenye koo alafu kuna ali ya weupe kwenye ulimi na Mashavu kwa ndan
Weupe kwenye ulimi unaweza kuwa ni hali ya kawaida. Weupe huu ukichanganyika na utandu huwenda ikaashiria uwepo wa hali fulani za kiafya. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa ukoma ni Ugonjwa unaosababishwa na bacteria anayejulika kama mycobacterium leprae. Soma Zaidi...

Aina za kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za kisukari Soma Zaidi...

Nini chanzo cha malaria
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu chanzo cha ugonjwa wa malaria Soma Zaidi...

Dalili za UTI upande wa wanawake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanawake Soma Zaidi...