PHP level 1 somo la tano (5)

Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.

SOMO LA TANO:
PHP FUNCTIONS:
Katika programming language, php imepata ubora wake kwa kuwa na hiki kipengele cha functions. Katika php kuna functions zaidi ya 1000. pia php inakupa uwezo wa wewe kuandika function yako mwenyewe kulingana na matarajio yako. Hivyo basi zipo funtion ambazo tayari zipo. Hizi zinaitwa built-in PHP functions. Na kuna hizo ambazo unaweka mwenyewe, hizi huitwa user defined functions.


 

Sasa function ni nini hasa?
Function ya kikundi cha maelekezo (block of statement) katika code za php ambazyo huweza kutumika zaidi na zaidi katika program. Tofauti na statement nyingine kama echo na print, ambazo huleta matokea punde tu ukiran code ama ukurasa ukufunguliwa au kurefresh. Function zenyewe mpaka zitu ziitajwe kwenye code yaani (by calling the functions).

Katika somo hili tutaona baadhi ya mifano ya built-in-function na jinsi zinavyofanya kazi kwa mifano. Hapa tutaangalia hasa kwenye string. Kama tulivyojifunzakatika somo lililopita.


 

KANUNI ZA FUNCTION (built-in-php functions)
1.Kwanza ni jina la function ila lisianze na namba mfano salamu
2.Kisha linafatiwa na mabano () mfano salamu()
3.Ndani ya mabano kunawekwa ujumbe ama maudhui ya hiyo function mfano salami(hujamb)
4.Kisha coloni ; mfano salamu salami(hujamb);

Tutajifunza kanuni nyingine za function kwenye somo linalofata kuhusu user defined functions.


 

FUNCTIONS KWENYE STRING:
1.Kujuwa idadi ya character kwenye string
. Kama unataka kujuwa je katika string kuna herufi ngapi ama namba ngapi ama character ngapi, basi tunatumia strlen() function. Neno hili ni ufupisho wa maneno string length.
Mfano:
<?php
echo strlen (“bongoclass”);
?>
Hii itakupa matokeo 10 kumaanisha kuwa kuna character 10.


 

2.Kwa kutumia php functions unaweza kubadili ama ku replace baadhi ya maandishi ndani ya string. Function inayotumika ni str_replace (). Kwa mfano katika mfano ufuatao nita replace neno bongoclass na kwa google.
<?php
echo str_replace ('karibu', 'bongoclass', 'welcome google');
?>
Hii itakupa matokeo welcome google maneno ya kwanza utaona yamebadilishwa kwa maneno ya pili.


 

3.Kuhesabu idadi ya maneno kwenye string
Katika hali ya kawaida unaweza kusema kuwa hii haina haja.lakini chukulia mfano data zipo kwenye database, na huwezi kuhesabu idadi ya maneno, na kwa mfano unatakiwa umlipe mtu kulingana na maneno aliyoandik, hapa utahitaji function ya kuweza kukuhiabia idadi ya maneno kwenye database.

Hivyo kwa namna hii function inayotumika hi hii str_word_count() mfano:-
<?php
echo str_word_count("welcome at bongoclass");
?>
Hii itakupa jibu la 3 yaani katika string iliyotumika kuna maneno matatu.


 

4.Pia unaweza kugeuza maneno, yamomeke mbelenyuma nyuma mbele. Kwa mfabo “welcome at bongoclass “ ukiligeuza litasomeka “ssalcognob ta emoclew”. ili kufanya hivi function inayotumika ni strrev yaani string revise. Mfano

<?php
echo strrev("welcome at bongoclass");
?>


 

5.Pia kwa kutumia strpos() unaweza kutafuta neno fulani kama lipo, kisha kama lipo matokeo utaambiwa position lilipo kwenye string. Yaani kama lipo la tatu kutoka mwanzo ama la nne. Kwa mfano katika string ifuatayo tutaangalia position ya neno bongoclass.

<?php
echo strpos('welcome google,welcome bongoclass,welcome facebook', 'bongoclass');
?>
Hapa utapata jibu 23 yaani neno bongoclass linapatikana kuanzia kwenye string ya 23 kutoka mwanzo. Na katika kuhesabu huku huanzia 0 na sio kwenye 1.


 

6.Kujiwa aina ya data iliyotumika
Ili uweze kujuwa aina ya data iliyotumika huwa tunatumia var_dump(). hii ni function ambayo hutumika katika kuonyesha aina ya data iliyotumika kwenye php. Angalia mifano hapo chini:-


Mfano 1:
<?php
$a = "hello piga *112#";
Var_dump ($a);
?>

Hapa iakuletea: string(16) "hello piga *112#" hii inamaana kuwa data nilizotumia kwenye mfano huu ni string, ambazo ni mkusanyiko wa herufi, namba na alama kama * na #. hiyo 16 hapo ina maanisha kuwa string iliyotumika ina character 16.


Katika somo lijalo tutaona function kwenye tarehe na kalenda na baadhi ya built-in-functions kwenye php. Hakikisha somo hili umelimudu vyema kwa kulifanyia mazoezi kabla ya kuingia somo linalofata.


Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email:mafunzo@bongoclass.com
Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 994

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 7 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hii ni project ya HTML ambayo imetengenezwa kulingana na mafunzo ya HTML level1. Tunatarajia project hii kuboreshwa kadiri mafunzo yanavyozidi kusonga mbele.

Soma Zaidi...
Php level 1 somo la saba (7)

Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)

Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi.

Soma Zaidi...
Utangulizi wa Android App Development

Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la sita (6)

Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 4 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL somo la 3

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la nne (4)

somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya html level 2 (html full course for beginners)

haya ni mafunzo ya HTML level 2 kwa wenye kuanza. Mafunzo haya ni muendelezo wa level 1 html. Katika course hii utajifunza mengi zaidi lu;iko level1 pia tutazidi kuboresha project yetu.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 4 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 4)

Karibu tena katika somo la nne la mafunzo ya HTML level2 html full course for beginners. Katika somo hili utajifunza kuhusu attributes na namna zinavyofanya kazi

Soma Zaidi...