v

Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake.

v

Maadili katika surat Al-Ahqaf


Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu na akamza kwa taabu. Na kubeba mimba yake hata kumwachisha ziwa; (uchache wake) ni miezi thelathini. Hata anapofikia baleghe yake na akawa mwenye umri wa miaka arubaini, (mtoto mwema) husema: "Ee Mola wangu! Niwezeshe nishukuru neema zako ulizonineemesha mimi na wazazi wangu, na niwezeshe nifanye vitendo vizuri unavyovipenda, na unitengenezee watoto wangu; kwa yakini ninatubu kwako; na hakika mimi ni miongoni mwa waliosilimu (walionyenyekea)." (46:15).


Hao ndio tunaowakubalia vitendo vyao vyema walivyovifanya, na tunayapita kando makosa yao, (tunayasamehe); (watakuwa) miongoni mwa watu wa Peponi: miadi ya kweli waliyoahidiwa. (4 6:16).



Na ambaye anawaambia wazazi wake: "Kefule nyi! Oh! Mnanitishia kuwa nitafufuliwa; na hali karne nyingi, (watu wengi) zimekwisha pita kabla yangu (wala hazikufufuliwa)?" Na hao (wazee wake) wawili huomba msaada wa Mwenyezi Mungu; (na humwambia mtoto wao:) "Ole wako! Amin (haya unayoambiwa). Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli." Lakini yeye husema: "Hayakuwa haya (mnayoyasema) ila ni visa vya watu wa kale (tu si maneno ya kweli)."



Hao ndio ambao imelazimika hukumu juu yao (ya kutiwa Motoni, pamoja na mataifa yaliyopita kabla yao ya majini na watu, hakika hao ndio waliojitia khasarani. (46:17-18)
Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa:



(a)Hatunabudi kuwafanyia wema wazazi wawili na hasa mama ambaye anapata dhiki kubwa katika kutuzaa na kutunyonyesha mpaka kufikia umri wa miaka miwili.



(b)Hatunabudi kumshukuru Allah (s.w) kwa kutuneemesha kwa neema mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuwapa wazazi wetu moyo wa huruma na mapenzi ya kutulea mpaka kufikia utu uzima.



(c)Pamoja na kumshukuru Allah (s.w), hatubabudi kuwashukuru wazazi wetu kwa kutulea kwa huruma na mapenzi. Shukrani zetu kwao tutazidhihirisha kwa kuwatii, kuwafanyia ihsani na kuwaombea dua na maghfira kwa Allah (s.w).


(d)Hatuna budi kujiepusha mbali na kuwafanyia wazazi wetu ufedhuli na jeuri. Tusisubutu hata kuwagunia.



(e)Hatunabudi kuomba kizazi chema na kumuomba Allah (s.w) atuwezeshe kukilea vyema kizazi chetu.



(f)Hatunabudi kufuatilia kwa makini usia mwema wanaotupa wazazi wetu.



(g)Hatunabudi kuleta toba na kuomba maghfira mara kwa mara (angalau kila siku mara mia moja).




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 223


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Vitimbi vya Makafiri Dhidi ya Nabii Salih(a.s) na Waumini na kuangamizwa kwao
Makafiri wa Kithamud hawakuishia tu kwenye kuukataa ujumbe wa Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Hijra ya Mtume(s.a.w) Kwenda Madinah
Njama za Kumuua Mtume(s. Soma Zaidi...

quran na sayansi
2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA Soma Zaidi...

Uendeshaji na Kupanuka kwa Dola ya Kiislamu Kipindi cha Makhalifa Waongofu
Soma Zaidi...

Namna ya kutambuwa kibla na umuhimu wa kuelekea kibla wakati wa kuswali
4. Soma Zaidi...

udhaifu wa hoja za kuunga mkono kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango
Udhaifu wa Hoja za Kudhibiti Uzazi:Hoja nyingi zinazotolewa kuunga mkono udhibiti wa uzazi zimejengwa juu ya hali na mazingira ya maisha yaliyoletwa na utamaduni na maendeleo ya nchi za Ulaya na Marekani. Soma Zaidi...

v
Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Soma Zaidi...

Vipi funga yaani swaumu itapelekea uchamungu na kutekeleza lengo
Funga inavyomuandaa mtu kuwa mcha-Mungu. Soma Zaidi...

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana
Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a. Soma Zaidi...

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)
Baada ya Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

maana ya swala kilugha na kisheria
Soma Zaidi...

Baada ya kumzika maiti nini kifanyike kumsaidia marehemu
Tumesha mzika maiti sasa imebakia mali yae nyumbani, watoto, wake na menginyeo. Soma Zaidi...