Kujiepusha na kula mali ya Yatima
Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).
(f)Kujiepusha na kula mali ya Yatima
Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).
Katika aya ya (17:34) tunakatazwa hata kukurubia mali ya yatima kwa maana ya kwamba tusithubutu kuchanganya mali zao na zetu kwa kisingizio chochote kile na tusizitumie hata kwa matumizi yao wenyewe iwapo tunao uwezo wa kuwalea pasina kuhitajia mali zao:
"Na wapeni mayatima mali zao wala msibadilishe kibaya kwa kizuri. Wala msile mali zao pamoja na mali zenu. Hakika (yote) hayo ni jukumu kubwa." (4:2)
βNa waogope (Mawasii kuwadhulumu mayatima; na wakumbuke) kama na wao wangewacha nyuma yao watoto madhaifu wangekuwa na khofu juu yao; basi wamwogope Mwenyezi Mungu na waseme maneno yaliyo sawa (kwa hao mayatima waliousiwa kuwatazama). Hakika wale ambao wanakula mali ya may atima kwa dhuluma, bila shaka wanakula moto matumboni mwao; na wataungua katika huo Moto (wa jahannam) uwakao.β (4:9-10)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Bongolite - Game zone - Play free game π2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π3 Kitabu cha Afya π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Himizo la kuwasamehe waliotukosea
βNa wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita).
Soma Zaidi...Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.
Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini.
Soma Zaidi...Sifa za waumini zilizotajwa katika surat As-Sajida
Nao husema (kwa maskhara): "Je, tutakapopotea katika ardhi, (tukageuka mchanga) ndio tutarudishwa katika umbo jipya?
Soma Zaidi...