Quran si maneno ya shetani

Quran si maneno ya shetani

(v) Dai kuwa Qur-an ni aya za Shetani



Katika mwaka 1988 Salman Rushdie, Muingereza mwenye asili ya kihindi, aliandika kitabu chake alichokiita "Satanic Verses" (yaani aya za Shetani) ambamo amemtukana Mtume (s.a.w), Uislamu na Qur-an kwa kuiita "aya za Shetani."



Katika kitabu chake hicho, Rushdie amedai kuwa hapakuwa na wahy wowote uliomshukia Muhammad (s.a.w) bali alikuwa akidai tu kuwa anashushiwa Wahy. Aidha Rushdie anadai kuwa Muhammad (s.a.w) alikuwa ni mtu aliyekuwa akifuata matashi yake mwenyewe akiongozwa na shetani na kwa hiyo yote yaliyomo ndani ya Qur-an ni maneno ya shetani.



Pia Rushdie katika kitabu chake hicho amedai kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa na uwezo wa kutofautisha wahy kutoka kwa Malaika au wahy kutoka kwa shetani.

Vile vile Salman Rushdie amedai kuwa Mtume (s.a.w) hakuwa na kumbukumbu ya kile alichowasomea waandishi wake na wala hakuweza kutambua hata kile ambacho waandishi hao wamekiongeza kichini-chini. Amepiga mfano wa mwandishi mmoja wa Kifursi kuwa alisomewa na Mtume aandike "Mwenye kusikia, mwenye kujua kila kitu" lakini yeye akaandika "Mwenye kujua na Mwenye hikma" na Mtume hakung'amua mabadiliko hayo!



Udhaifu wa madai ya Salman Rushdie
Kwanza,
ujumbe wa Qur-an umeteremshwa ili kumtoa binaadamu kutokana na hadaa zote za shetani. Shetani katika Qur-an ameelezwa wazi pamoja na vitimbi vyake na watu anaowatumia ili wanaadamu wasiweze kupotezwa naye. Hebu turejee aya chache zifuatazo:


"Na namna hii tumemfanyia kila Nabii maadui, (nao ni) mashetani katika watu na (mashetani) katika majini. Baadhi yao wanawafunulia wenzao maneno ya kupamba pamba ili kuwadanganya. Na Mola wako angelipenda wasingelifanya hayo. Basi waache na uongo wao." (6:112)


"Enyi wanaadamu! Shetani (Iblisi) asikutieni katika matata, kama alivyowatoa wazee wenu katika Pepo akawavua nguo zao ili kuwaonesha tupu zao. Hakika yeye pamoja na kabila yake wanakuoneni na hali ya kuwa hamuwaoni." Bila shaka sisi tumewajaalia mashetani kuwa marafiki wa wale wasioamini." (7:2 7)



"Kwa yakini Shetani ni adui yenu, basi mfanyeni adui (yenu; kwa hivyo msimtii) kwani anaita (analiita) kundi lake liwe katika watu wa Motoni." (35:6)
Kama Qur-an ni maneno ya Shetani, inakuwaje tena shetani mwenyewe ajidhihirishe kiasi hicho ili watu wamkimbie?



Pili, Allah (s.w) anasema kuwa laiti ingelikuwa hii Qur-an inatoka kwa mwingine asiye kuwa Yeye au kama ingekuwa ina waandishi wawili tofauti ambao wana malengo yanayopingana mmoja anavutia kwenye mema na mwingine kwenye uovu pangelikuwa na khitilafu nyingi (Qur-an 4:82). Je, uko mgongano wowote katika maneno ya Qur-an? Haupo, bali maneno yote ya Qur-an ni yenye kusadikishana. Hivyo haiwezekani Qur-an kuwa na mchanganyiko wa maneno ya shetani na ya Allah (s.w) kwa pamoja.



Tatu, Qur-an yenyewe imekataa kuwa Qur-an si maneno ya shetani."Wala hii si kauli ya shetani aliyefukuzwa (katika rehma za Mwenyezi Mungu.) (81:25)



Nne, Sote tunamfahamu shetani kuwa ni kiumbe dhaifu pamoja na kuwa hatumuoni. Sasa ikiwa shetani ameleta maneno na ujumbe mzito uliomo ndani ya Qur-an, kwanini na mashetani wengine nao hawakai pamoja kujibu zile changamoto zilizotolewa? "Mahound" kama alivyomwita Rushdie ni shetani mmoja tu, je pamekuwa na uzito gani kwa wanaadamu pamoja na majini wakichanganyika kuleta mfano wa angalau sura moja ya Qur-an? Qur-an imetoa changamoto hiyo tangu kuanza kushuka kwake:


"Sema "Hata wakijikusanya watu (wote) na majini kuleta mfano wa hii Qur-an basi hawangaliweza kuleta mfano wake, hata kama watasaidiana (vipi) wao kwa wao." (17:88)




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 295


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina
Baada ya matukio haya ndipo Musa(a. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa Surat al-Kawthar na fadhila zake
SURATUL-KAUTHAR Imeteremshwa maka, na sura hii imeshuka kwa sababu al-aAs ibn Waail. Soma Zaidi...

hukumu ya ombaomba katika uchumi wa kiislamu
Suala la omba-ombaTukiliangalia suala la omba-omba kwa upana kidogo, ambalo hivi sasa linaongelewa katika vikao mbalimbali vya kitaifa na kimataifa, tutaona kuwa ni Uislamu pekee unaotoa namna bora ya kulishughulikia suala hili. Soma Zaidi...

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki
Soma Zaidi...

DARSA ZA QURAN
Soma Zaidi...

Simu au Kompyuta inastak? (inasumbua)
Jifunze matumizi ya simu yako na namna ya kutatua matatizo mbalimbali kwenye simu na kompyuta.. Soma Zaidi...

JARIBU LA PILI LA ALADINI
Soma Zaidi...

Kupotoshwa Mafundisho ya Nabii Isa(a.s)
Pamoja na Isa(a. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al-Falaq na surat an-Nas na fadhila za kusoma sura hizi
SURAT AL-MUAWIDHATAYN (SURAT AL-FALAQ NA SURATUN-NAS) Inaelezwa kuwa sura mbili hizi zilishuka pamoja, na maulamaa wanaelezea kuwa Mtume (s. Soma Zaidi...

Hizi ndio suna za swala kwa swala za faradhi na suna
Soma Zaidi...

swala ya kuomba mvua na namna ya kuiswali
12. Soma Zaidi...

KWA NINI DIRISHA MOJA?
KWA NINI DIRISHA MOJA? Soma Zaidi...