image

Qur-an Kushuka Kidogo Kidogo kwa Kipindi cha Miaka 23:

Qur-an Kushuka Kidogo Kidogo kwa Kipindi cha Miaka 23:

(iv)Qur-an Kushuka Kidogo Kidogo kwa Kipindi cha Miaka 23:



Historia inatuthibitishia kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) hakuanza kuufundisha Uislamu na kuutangaza ulimwengu mzima kwa kurejea Qur-an kama Kitabu tulicho nacho hivi sasa bali aya za Qur-an zilikuwa zikimshukia kidogo kidogo kulingana na haja na wakati kwa kipindi chote cha Utume wake cha miaka 23. Kwa maana nyingine Qur-an imeshuka kidogo kidogo katika kipindi chote cha utume kuanzia mwanzo wa Utume 610 A.D. mpaka siku chache kabla ya kutawafu Mtume(saw), 632 A.D. Kuhusu Qur-an kushuka kidogo kidogo tunafahamishwa katika aya zifuatazo:


Na Qur-an tumeigawanya sehemu mbali mbali ili uwasomee watu kwa kituo, na tumeiteremsha kidogo kidogo. (17:106)



Na wakasema wale waliokufuru; Mbona hakuteremshiwa Qur-an yote kwa mara moja? Kama hivi (mnavyoona, tumeiteremsha kidogo kidogo) ili tuuthibitishe, (tuutie nguvu), moyo wako (kwa hizo aya mpya mpya zinazoteremshwa wakati baada ya wakati) na tumeipanga kwa uzuri. (25:32)


Hakika sisi tumekuteremshia Qur-an sehemu sehemu (kidogo kidogo). (76:23).
Kama inavyoonekana katika aya hizi. Qur-an imeshushwa kidogo kidogo ili iwe wepesi kwa Mtume Muhammad (s.a.w) kuufikisha ujumbe uliotangulia kwa ukamilifu kinadharia na kimatendo kabla ya ujumbe mwingine uliofuata.



Kwa upande mwingine Qur-an imeshuka kidogo kidogo ili kuwawezesha waumini wa mwanzo kuihifadhi Qur-an kwa wepesi, kuyaelewa fika mafundisho yake kinadharia na kuwawezesha kuitekeleza Qur-an katika kila kipengele cha maisha yao ili wawe jamii bora ya kuigwa na jamii zitakazofuatia.



Kushuka Qur-an kidogo kidogo kwa muda wa miaka 23 ni hoja nyingine kuwa Qur-an ni Kitabu cha Allah (s.w). Kwa yeyote yule anayeisoma Qur-an kwa makini na akajua mpangilio wake wa aya na sura kama vile sura moja kuwa na mchanganyiko wa aya za mwanzo na zilizoshushwa mwishoni lakini bado kunapatikana mtiririko mzuri wa maudhui na mpangilio wa sura usiofuata mtiririko wa kushuka, utaona kuwa haiyumkiniki kuwa Qur-an ni Kitabu kilichoandikwa na Mtume Muhammad (s.a.w) kama wanavyodai makafiri.


Pia Qur-an ingelikuwa imeandikwa na Mtume Muhammad (s.a.w) isingelichukua muda wote huo, bali ingelibidi aiandike yote kwa muda mfupi ili aweze kuitumia katika kazi yake ya kuwaongoza watu. Ni kawaida kuwa ili kufanikiwa katika utekelezaji wa jambo lolote ni lazima kwanza pawe na nadharia nzuri inayoelekeza namna ya utekelezaji. Halikadhalika, Mtume Muhammad (s.a.w) aliyekuwa kiongozi wa Dola ambaye mfano wake haujapatikana, asingeliweza kufanya kazi nzito na kubwa kiasi hicho bila ya kuwa na nadharia ya kumwongoza. Hivyo, kwa kutokuwa na Qur-an yote mkononi mwake ili kuitumia katika kila hatua ya kazi yake, inadhihirisha kuwa alikuwa akiletewa mwongozo kutoka kwa Allah(sw) katika kila hatua ya kazi yake mpaka alipoikamilisha.




                   




           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 495


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Fadhila za kusoma Quran na umuhimu wa kusoma Quran
Unazijua faida za kusoma Quran, na je ni faida gani utapata ukisoma Quran? Soma Zaidi...

WAQFU WAL-IBTIDAAI
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr
Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii Soma Zaidi...

yaliyomo: HUKUMU YA MIM SAKINA, NUN SAKINA, MADA, WAQFU, QALAQALA, TAFKHIM NA TARQIQ, USOMAJI WA QURAN
DARSA ZA TAJWID YALIYOMOSURA YA 01 . Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al Mauun
Sura hii ni katika sura ambazo zinahitaji kusomwa kwa mazingatio sana. Wanaoswali bila ya kuzingatia swala zao, wameonywa vikali sana. Wanaowatesa na kuwanyanyasa mayatima wameonywa vikali. Wanaowanyima wenye haja na masikini huku wakiwakaripia nakuwasem Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al humazah
Sura hii inaonya vikali tabia ya kusengenya na kusambaza habari za uongo. Wameonywa vikali wenye tabia ya kujisifu kwa mali, kukusanya mali bila ya kuitolea zaka. Soma Zaidi...

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake
Soma Zaidi...

Naman ya kuiendea quran na kuifanyia kazi baada ya kuisoma
Soma Zaidi...

Sababu za kushukasurat an Nasr
Sura hii ni katika sura za mwisho kushuka, huwendakuwa ndio ya mwisho kabisa. Masahaba waliamini kuwa sura hii imetabiri kifo cha Mtume S.A.W Soma Zaidi...

Nini maana ya Iqlab katika hukumu za tajwid
Hapa utajifunza maana ya iqlab katika usomaji wa Quran kwa tajwid Soma Zaidi...

DARSA ZA QURAN
Soma Zaidi...