Muhutasari wa sifa za wanafiki

Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.

Muhutasari wa sifa za wanafiki

Muhutasari wa sifa za wanafiki


Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:-
(1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.


(2)Hujaribu kumdanganya Mwenyezi Mungu pamoja na waumini wakidhani kuwa yaliyo nyoyoni mwao hayajulikani.


(3)Hufanya maovu katika ardhi huku wakidai kuwa wanatenda mema.


(4)Huwaona waumini wa kweli kuwa ni wajinga kwa kufuata kwao Uislamu inavyotakikana.


(5)Huwacheza shere Waislamu.


(6)Hujiiona kuwa wao ni bora kuliko waumini


(7)Hujikomba kwa viongozi wa kitwaaghuti.


(8)Huwafanya makafiri na Washirikina kuwa marafiki zao wa ndani badala ya Allah(s.w) Mtume wake na waumini.


(9)Huyapenda zadi maslahi ya dunia kuliko ya akhera.


(10)Hukataa kuhukumiwa na sheria za Allah (s.w).


(11)Hutumia viapo kama kifuniko cha maovu yao.


(12)Huchanganya haki na batili, kufuru na Uislamu.


(13)Huendea swala kwa uvivu.


(14)Hawamtaji Allah ila kidogo sana.


(15)Huwafitinisha Waislamu.


(16)Huchukia Waislamu wanapofikwa na kheri na kufurahia wanapofikwa na msiba.


(17)Hawako tayari kutoa mali zao katika njia ya Allah (s.w) na wakitoa chochote hutoa kwa ria


(18)Huwazuia watu kutoka katika njia ya Allah.


(19)Huzifanyia stihizai (shere) aya za Qur-an.


(20)Huamrisha maovu na kukataza mema.


(21)Husema uongo na kuvunja ahadi.


(22)Huwa vunja moyo na kuwakatisha tamaa Waislamu wa kweli ili wabakie katika ukafiri sawa na wao.


(23)Hufanya hiyana katika mambo ya kheri na kuchagua mambo mepesi mepesi.


(24)Wanawaogopa na kuwachelea watu zaidi kuliko Allah (s.w).


(25)Hush irikiana na maadui kuupiga vita Uislamu na Waislamu.



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 145


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

maana na asili ya dini, kazi zake na nadharia potofu za makafiri kuhusu dini
2. Soma Zaidi...

DUA 32 - 40
32. Soma Zaidi...

Sifa za wanafiki katika quran
Soma Zaidi...

MASHARTI YA KUKUBALIWA KWA DUA
MASHART YA KUKUBALIWA KWA DUA. Soma Zaidi...

Kuamini Mwenyezi Mungu sio suala la Kibubusa au Kufuata Mkumbo
Kuamini Mwenyezi Mungu sio suala la Kibubusa au Kufuata Mkumbo. Soma Zaidi...

NAMNA YA KUSWALI: NIA YA SWWALA, NA KUPIGA TAKBIRA (yaani kusema Allah akbar)
Mtume (s. Soma Zaidi...

haki na wajibu kwa watumishi wa nyumbani (house boy and house girl)
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII YUNUS
Soma Zaidi...

Bara la Arabu Zama za Jahiliyyah
Wakati Mtume(s. Soma Zaidi...

Uendeshaji na Kupanuka kwa Dola ya Kiislamu Kipindi cha Makhalifa Waongofu
Soma Zaidi...

tarekh 5
KUZALIWA KWA MTUME (S. Soma Zaidi...

Kwa Nini Mwanaadamu Hawezi Kuunda Dini Sahihi ?
1. Soma Zaidi...