picha

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah


Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini. Wanatafuta kumdanganya Mwenyezi Mungu na wale walioamini, lakini hawadanganyi ila nafsi zao; nao hawatambui. Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi. Basi watakuwa na adhabu iumizayo kwa sababu ya kule kusema kwao uwongo. (2:8-10)


Na wanapoambiwa: "Msifanye uharibifu ulimwenguni." Husema "Sisi ni watengenezaji. "Hakika wao ndio waharibuji, laini hawatambui.Na wanapoambiwa: "Aminini kama walivyoamini watu" Husema"Oh! Tuamini kama walivyoamini wale wapumbavu?" Hakika wao ndio wapumbavu lakini hawajui. (2:11-1 3)



Na wanapokutana na walioamini husema: "Tumeamini"; na wanapokuwa peke yao kwa mashetani wao husema: "Hakika sisi tu pamoja nanyi, tunawacheza shere tu." Mwenyezi Mungu atawalipa shere yao na kuwawacha katika upotofu wao wakitangatanga ovyo. Hao ndio waliokhiari upotofu kuliko uongofu; lakini biashara yao haikupata faida wala hawakuwa wenye kuongoka. (2:14-1 6)


Mfano wao (hawa wanafiki) ni kama mfano wa wale (wasafiri waliokumbwa na kiza) wakakoka moto, (na) ulipowaonyesha yaliyo pembezoni mwao, Mwenyezi Mungu aliiondoa nuru yao hiyo na kuwawacha katika viza; hawaoni. (2:17)


Viziwi, mabubu, vipofu; kwa hivyo hawatarejea. (2:18)


Au (mfano wao pia) ni kama mvua kubwa itokayo mawinguni; ndani yake mkawa mna viza na radi na umeme; wakawa


wakitia vidole vyao masikioni mwao kwa ajili ya mingurumo, kwa kuogopa kufa; (na kufanya hivyo hawakusaidii kitu). Na Mwenyezi Mungu anawajua vyema hao makafiri. (2:19)


Unakaribia umeme huo kunyakua macho yao; kila unapowaangazia huenda ndani yake na unapowafanyia giza husimama. Na Mwenyezi Mungu angependa angaliondoa kusikia kwao na kuona kwao. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kuweza juu ya kila kitu. (2:20)



Kutokana na aya hizi tunajifunza sifa za wanafiki zifuatazo:
(i)Kuonesha imani ya uongo. Katika vinywa vyao wanadai kuwa ni waumini lakini katika nafsi zao na matendo yao wanaikanusha imani yao.
(ii)Wanauchukia Uislamu nyoyoni mwao, na wanazidi kuuchukia kila Uislamu unavyosonga mbele.
(iii)Hufanya uharibifu katika nchi huku wakidai kuwa wanatengeneza.
(iv)Huwabeza waumini wa kweli wanaofuata Uislamu vilivyo.
(v)Hawana msimamo. Wanataka wapate maslahi ya Uislamu na wakati huo huo wawe pamoja na makafiri.
(vi)Wanawacheza shere Waislamu.
(vii)Kwa mujibu wa mfano uliopigwa katika aya ya 17 (2:17) wamekhiyari kupotea baada ya kujiwa na mwongozo (nuru).
(viii)Kwa sababu wamedhamiria upotevu badala ya uongofu kwa ajili ya maslahi ya dunia, hata ukiwaita kwenye uongofu hawawezi kuja. Wamefananishwa na watu wenye vilema vitatu kwa pamoja vya uziwi, ububu na upofu. Hivyo hawawezi kusikia neno la mwenye kuadhini wala la mwenye kukimu.


Kwa mujibu wa mfano uliopigwa katika aya ya 19 na 20 (2:19-20), wanafiki wanatamani matunda yatokanayo na kusimama kwa Uislamu katika jamii lakini hawako tayari kukabiliana na changamoto zinazotokana na mchakato mzima wa kusimamisha Uislamu katika jamii. Wanafurahia matunda yanayotokana na mvua nzuri za masika lakini hawako tayari kukabiliana na radi, ngurumo na umeme vinavyoandamana na mvua hizo.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1679

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰2 ai web app    πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil

Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.

Soma Zaidi...
Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu...

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Soma Zaidi...
Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake

Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.

Soma Zaidi...
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...
Athari za vita vya Uhud

Vita vya uhudi viliweza kuleta athari nyingi. Post hii itakuletea athari baadhi za vita hivyo.

Soma Zaidi...
Ni ipi maana ya Imani katika Uislamu, na ni zipi sifa za muumini.

Katika Uislamu imani inanguzo kuu 6.Pia muumini anatakiwa ajipambe na sifa za waumini. Posti hii itakufundisha kuhusu imani katika Uislamu.

Soma Zaidi...