image

Sababu za kshuka surat al Asr

Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo…

SURAT AL-ARS
Wafasiri wengi wanasema sura hii ilishuka Makka.
Imam Shafii anasema, Sura hii ina maana nyingi na pana. Na kama mtu aifikiri, haja zake zote za dini zinaweza kutimizwa. Imesimuliwa katika Hadithi ya kuwa masahaba wawili kila mara walipokuwa wanakutana wakati wa kuagana walikuwa wakisomeana sura hii.


 


Neno hili maana yake ni wakati, wakati wa alasiri, na pia maana yake ni kukamua. Katika Aya hii Mwenyezi Mungu analeta ushahidi wa wakati kuonyesha ya kwamba kadiri wakati unavyopita umri wa kila mtu unapungua na kuingia katika hasara maana kila kitu kinasogelea mwisho wake na kitakufa. Lakini watu wanaweza kujiepusha na hasara hiyo kwa kuamini na kutenda mema na kuusiana kushika haki na subira, maana mambo haya yatafanya roho zao ziendelee katika maisha ya raha huko Akhera.


 

Katika sura hii habari za watu wa namna mbili zimeelezwa. Ya kwanza ni wale ambao wamo hasarani, na pili ni wale ambao wameamini na kufanya vitendo vizuri. Ni dhahiri ya kuwa wasioamini wala hawafanyi vitendo vizuri wao ndio watakaokuwa katika hasara. Lakini wanaoamini kwa moyo wote, tena wanaionyesha imani yao kwa viungo vyao, kwa kutenda sawa na walivyoamini, bila shaka wao watalindwa na hasara. Tena ikumbukwe ya kuwa Mwenyezi Mungu aliposema "walioamini" kwa hakika ameashiria kwenye ukamilifu wa elimu; maana imani haiwezi kupatikana bila elimu, Basi mtu anapopata ukamilifu katika elimu, anakuwa mwenye imani hasa. Na Mwenyezi Mungu aliposema "kufanya vitendo vizuri" ameelekeza kwenye ukamilifu wa amali, yaani matendo. Hivyo Mwenyezi Mungu amesema ya kuwa watu wanaokamilika katika elimu, na wanaokamilika katika vitendo, wao wanasalimika katika hasara na wanaokoka.


 

Hakuna sababu maalumu yenye kuaminika juu ya kushuka kwa sura hii.


 

UMUHIMU WA SURA HII
Sura hii inachukuliwa kama muhtasari wa Qur'ani nzima na karibu wasomi wote mashuhuri wa kitamaduni na wa kisasa wa Kiislam wakiwemo Imam Shafi, Ibn Kathir, Israr Ahmed na Farhat Hashmi.


 

Ibn Kathir, mfasiri wa Quran anashikilia kwamba sura hii, kama onyo kwa waumini kutopoteza wakati au wangeweza kudhalilishwa au hata kuharibiwa.


 

Imam Shafi, alishikilia-kwamba ikiwa Mungu angefunua tu surah hii ingetosha kwa mwongozo wa wanadamu wote. Ilielezea kwa muhtasari kiini cha ujumbe wa Kurani. Kwa hivyo, Imam Shafi'i anasisitiza kwamba ikiwa mtu angefuata ushauri wake, ilitosha kwa wanadamu kupata mafanikio maishani.


 

Sayyid Qutb, Mfasiri wa Quran, anathibitisha kwamba surah hii inaelezea mfumo kamili wa maisha ya mwanadamu kulingana na maoni ya Kiisilamu. Anasema kuwa inafafanua, kwa njia iliyo wazi na fupi zaidi, dhana ya kimsingi ya imani katika muktadha wa ukweli wake kamili.


 

Al-Tabarani: wakati wanadamu wanajikuta wamepotea; inaweza kujihuisha kwa kurudi kwenye fomula iliyotolewa na aya ya tatu na kanuni / masharti manne, ambayo yanazingatiwa kama msingi.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2563


Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r.a)
Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r. Soma Zaidi...

Maisha ya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 19. Hapa utajifunza maisha ya Mtume kabla ya utume. Soma Zaidi...

Saratul-asr 103
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

ASBAB-NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN
ASBAB NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN Quran imeteremka kwa muda wa miaka 23 kidogokido. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat al qariah
Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume. Soma Zaidi...

HUKUMU ZA IDGHAM
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Lugha ya kiarabu Lugha ya quran: kwa nini quran katika lugha ya kiarabu
Soma Zaidi...

HUKUMU ZA QALQALA
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

quran na sayansi
Soma Zaidi...

Sababu za Quran kuwa mwongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA (MIIM SAKINA)
HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA : Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’). Soma Zaidi...

Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa
Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya. Soma Zaidi...