Sababu za kupata hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi mmoja, mara nyingi kuna Watu ambao huwa wanalalamika kwa sababu ya kupata hedhi za mara kwa mara kwa mwezi mmoja.
Sababu za kuwepo kwa hedhi za mara kwa mara katika mwezi mmoja.
1.Mabadiliko ya homoni.
Mara nyingine hedhi za mara kwa mara utokea kwa sababu ya kuwepo kwa mabadiliko ya homoni, homoni nyingine baada ya kuruhusu yai moja Litoke kwa mwezi mmoja uweza kuruhusu mayai mawili ndani ya mwezi mmoja na hali hiyo usababisha msichana au mama kupata hedhi mara mbili kwa mwezi mmoja.
2.Kukua kwa mfuko wa kizazi.
Hali hii uwapata sana wale wanaoanza kuingia kwenye hedhi wanaweza kupata hedhi mara mbili ni kwa sababu mfuko wa uzazi unakuwa unakomaa au pengine wanaweza kukosa kwa miezi miwili au mitatu ya mwanzo na baadaye hali inakuwa kawaida wasiogope hali hiyo ni ya kawaida utokea na mara maisha yanaendelea.
3.Kwa wanawake wanaotumia vitanzi.
Hawa ni wale wanaotumia njia hii ya uzazi wa mpango na uweza kuingia kwenye siku zao za mwezi mara moja zaidi na baadae hali uwa kawaida ni kwa sababu ya mabadiliko kwenye mwili kwa sababu ya kitu kilichoingilia mfumo wa via vya uzazi na mabadiliko utokea kwa mda kama miezi miwili hivi na baadae hali inaendelea kama kawaida.
4.Kuwepo kwa maambukizi kwenye mfuko wa uzazi , kama kunaagonjwa au kuwepo kwa uvimbe usababisha pi mtu kuingia kwenye siku zake za mwezi mara mbili au zaidi kwa mwezi mmoja, kwa hiyo ni vizuri kabisa kupima maambukizi mara kwa mara ili kuangalia kama kuna mambukizi au kama kuna uvimbe wowote unaosababisha mwanamke kuingia kwenye siku zake za mwezi zaidi ya mara moja
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Mambo ya kuzingatia kwa Mama mwenye mimba
Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa Mama mwenye mimba, ni kipindi ambacho Mama uhitahi uangalizi wa karibu zaidi.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kulia
Soma Zaidi...Njia za kuongeza nguvu za kiume
Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuongeza nguvu za kiume
Soma Zaidi...SIKU HATARI ZA KUPATA UJAUZITO KWA MWENYE MZUNGURUKO WA SIKU KIDONGO AU NYUNGI
SIKU YA KUPATA UJAUZITO Kawaida wanawake walio wengi mzunguruko wa siku zao ni siku 28 lakini wapo ambao ni zaidi ya hapo na wapo ambao ni chini ya hapo.
Soma Zaidi...Vipimo muhimu kabla ya kubeba mimba
Posti hii inahusu zaidi vipimo muhimu kabla ya kubeba mimba,ni vipimo vya moja kwa moja kutoka maabara na vingine sio vya maabara.
Soma Zaidi...