image

Sababu za kushuka surat al Zilzalah

surat Zalzalah ni sura ya 99 katika mpangilio wa Quran, na ina aya 8. Sura hii imeteremshwa Madina ila pia kuna kauli zinathibitisha kuwa ni ya Makkah. Katika hadithi iliyopewa daraja la hassan na Imam Tirmidh Mtume S.A.W amesema kuwa kusoa surat Zilzalah

Asbab Nuzul Surat Zilzalah

Ama kuhusu sababu za kushuka sura hii, hakuna nukuu za kutosha kuonyesha hasa tukio ambalo lilitokea hata sura hii ikashushwa. Hata hivyo kutokana na maelezo ya Sa'id bin Jubair ni kuwa baada ya kushuka aya ya 8 ya surat Al insan watu walidhani kuwa wak=liotoa sadaka kidogo sana hawatalipwa na wengine wakadhani kuwa dhambi ndogo wanazozifanya hawataadhibiwa, hivyo Allah akashuka aya 7 na 8 katika surat al zilzalah.

 

Kutokana na maelezo Maelezo ya Sura hii kuwa ukifanya dhambi iwe ndogo kiasi gani utalipwa malipo yake, na ukifanya wema mdogo kiasi gani pia utalipwa. Ama kuhusu wema kuna maelezo mengine zaidi ni kuwa Quran inasibitisha kuwa wema hulipwa kwa marakumi zaidi ama zaidi ya hapo. Yaani mfano umetenda wema mmoja, basi Allah atazidisha kwa kumi malipo yake. Na huwenda akazidisha zaidi ya hapo hata mara mia saba kama Surat Al Baqarah inavyoeleza ama zaidi na zaidi.

 

Imesimuliwa Kutoka kwa Abdallah Inb Umar kuwa wakati sura hii iliposhuka Abubakar alikuwa amekaa, basi akaanza kulia. Mtume S.A.W akamuuliza "nikipi kinachokuliza ewe Abubakar? " Abubakar akajibu " ni hii sura " basi Mtume wa Allah akasema "lau kama nyinyi mngelikuwa si wenye hamkosei na hamfanyi madhambi basi Allah angeumbwa umma mwingine baada yenu ambao watu wake wanakosea na wanafanya madhambi na kisha wanataka msamaha na Allah atawasamehe"  

 

KIPENGELE CHA TAWHID:

Sura hii ukiisoma kwa mazingatio Ina mambo mengi ya kiimani tunapasa kuyaweka katika fahami zetu:

1. Ardhi itatetemeshwa na itoe kila kilichomo ndani yake marehemu na hazina zilizomo

2. Mwanadamu atapata hofu sana na kujiuliza ina nini hii ardhi

3. Siku ya kiyama Ardhi itatoa siri zote, itatoa ushahidi wa kila wema na uovu uliofanywa na mtu katika ardhi.

4. Allah ameipa idhini Ardhi ianze kutoa habari. katika surat Yasin Allah anatujulisha kuwa siku ya kiyama midomo yetu haitafanya kazi, yaani haitazungumza, ila Allah atazungumzishwa viungo na viseme yaliyo ya kweli, viungo hivyo ni kama mikono, ngozi na vinginevyo. Hivyo hivyo ardhi nayo itapewa idhini ya kuzungumza kweli tupu kila kilichofanywa na mwanadamu iwe kidogo aka kikubwa.

5. basi mwenye kufanya wema ama uovu ulio mdogo kama dhara basi atalipwa kama ni wema kwa wema na kama ni uovu kwa adhabu. Neno dhara hili leo linatafsiriwa kwa maana ya atom. Atom ni chembe ndoogo sana ambayo huwezi kuiona kwa macho ya kawaida kwa udogo wake. Hii inamaanisha kuwa hata kama wema ni mdogo kiasi gani utalipwa na hata kama uovu ni mdogo kiasi gani pia utalipwa.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2102


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Sababu za kushuka Surat al fatiha (Alhamdu)
Kwa kuwa hakuna sababu mwalumu ikiyonukuliwa kuwa ndio chanzo cha kushushwa suravhii. Basi post hii itakujuza mambo ambayo huwenda hukuyajuwa kuhusu fadhika za surabhii na mengineyo. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al adiyat
Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah. Soma Zaidi...

Ni nini maana ya Tajwid, na ni ipi nafasi yake kwenye uislamu
Hapa utajifunza maana ya Tajwid kilugha na kisheria. Pia nitakujuza jukumu ya kusoma tajwid. Soma Zaidi...

Fadhila za kusoma surat al Baqarah
Surat al Baqarah ni katika sura ambazo tunapaswa tuwe tunasoma mara kwa mara. Post hii itakufundisha kuhusu fadhila za sura hii. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat Dhuha
Sura hii imetermka Makkah na ina aya 11. Sura hii ni moja ya sura ambazo zimeshuka mwanzoni wakati ambapo Mtume ameanza kazi ya utume. Soma Zaidi...

Maana ya Quran na Majina ya quran n amaana zao
Soma Zaidi...

Aina za Madda twabiy kwenye usomaji wa Quran
Madda zimegawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo ni madda twabiy na madda fariy Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat an-Nas na surat al Falaq
Sura mbili hizi pia hujulikana kwa jina la al muawidhatain ambazo ni surat an Nas na surat al falaq. Soma Zaidi...

Wanaoongozwa na wasioongozwa na quran
Soma Zaidi...

surat al mauun
SURATUL-MAM’UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat.. Soma Zaidi...

Saratul-humaza
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kutokea Kweli Matukio yaliyotabiriwa katika Qur-an
Soma Zaidi...