picha

Sababu za kutangulia kwa kitovu wakati Mtoto anazaliwa

Posti hii inahusu zaidi sababu za kutangulia kwa kitovu wakati wa mtoto anapozaliwa.

Sababu za kutangulia kwa kitovu wakati Mtoto anazaliwa.

1. Kwa kawaida tunajua kuwa mtoto utanguliza kichwa ila kwa wakati mwingine Kuna uwezekano mkubwa wa mtoto kutanguliza kitovu, na kwa wakati mwingine kitovu hicho kinaweza kuja kimejivilingisha kwenye shingo na mtoto akipata shida wakati wa kutoka kitovu kinaweza kumniga akafariki au kama Kuna ujuzi zaidi kwa wataalamu wa afya mtoto anaweza kuokolewa kwa hiyo zifuatazo ni sababu za kitovu kutangulia wakati mtoto anapozaliwa.

 

 2. Jinsi mtoto alivyolala.

Kwa kawaida mtoto tunamtegemea aanze kutoa kichwa wakati wa kuzaliwa ila Kuna watoto wanatanguliza matako, kichwa, uso, mgongo na vitu kama hivyo ambavyo ni kawaida na kichwa kwa hiyo katika kujigeuza geuza Ili aweze kupata sehemu ya kutanguliza saa nyingine kitovu kinatanguli mbele kabla ya mtoto.

 

3. Mtoto kuwa zaidi ya mmoja.

Kwa wakati mwingine hasa kwa akina Mama ambao ujifungua mapacha kwa sababu ya kuwepo mtoto Zaid ya mmoja kila mtoto utafuta jinsi ya kutoka Ili aweze kuzaliwa kwa hiyo katika kiangaika Ili kupata nafasi usababisha kutangulia kwa kitovu badala ya kichwa.

 

4. Kupasuka kwa membrane kabla ya mtoto kuingiza kichwa kwenye mlango wa kizazi.

Kuna wakati mwingine chupa upasuka mapema sana kabla ya mtoto kuingiza kichwa kwenye mlango wa kizazi hali hii nayo usababisha mtoto kutanguliza kitovu.

 

5. Muundo wa mlango wa kizazi.

Pengine Kuna akina Mama wameumbwa tofauti kabisa na kuwa na uwezo wa kupitisha mtoto na akifika wakati wa kusukuma mtoto hawezi kupita ingawa anahisi uchungu na sifa zote za kujifungua anakuwa Nazo katika kuangaika anajikuta mtoto ashatanguliza kitovu.

 

6. Kwa hiyo hali hii ni ya hatari endapo wahudumu wa afya hawana utaalamu wa kugundua mapema tatizo hili, ni vizuri kuligundua Ili kuweza kuokoa maisha ya Mama na mtoto wakati Mama akiwa anajifungua.

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3607

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Njia za kuondoa fangasi sehemu za siri

Makala hii itakujuza baadhi ya njia utakaoweza kuzifuata ili kukabiliana na fangasi sehemu za siri kwa wanaume

Soma Zaidi...
Mabadiliko kwenye uke wa Mama pale anapobeba mimba.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye uke wa Mama pale anapobeba tu mimba, Mama anapobeba mimba Kuna mabadiliko Katika uke wa Mama kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito, ni mabadiliko ambayo utokea kwa wajawazito hasa kwenye mfumo wa chakula.

Soma Zaidi...
Dr nahis kuchanganyikiwa nimetoka niliingia hedhi tar 18 mwezi wa9 lakini saivi Jana tena nmeingia dr hii imekaaje mimi?

Kamaumeshawahi kujiuliza kuhusu kutokwaba damu tofautivna siku za hedhi, base mwaka hii ni kwaajiki yako.

Soma Zaidi...
SABABU ZA KUTOKA KWA MIMBA (sababu za kuharibika kwa ujauzito)

Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka.

Soma Zaidi...
Ni ipi hasa siku ambayo nitafute ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kutafuta ujauzito

Soma Zaidi...