Sababu za kutoka kwa mimba na dalili zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kutoka kwa mimba na dalili zake

KUTOKA KWA UJAUZITO, DALILI ZAKE NA SABABU ZAKE.Kutoka kwa ujauzito mara nyimgi hutokea katika hiki kipindi cha kwanza yaani ndani ya wiki 12 za mwanzo. Inakadiriwa kuwa robo ya mimba zinazotoka basi hutoka katika kipindi hiki. Mwanamke anaweza akatokwa na mimba kwa kujuwa ana bila ya kujuwa. Inaweza kutokea pia mwanamke akabeba ujauzito na ukatoka bila kuwa na habari yeyote kama alikuwa na miba na imetoka. Ni kuwa mimba inaweza kutoka bila ya kuwa na dalili za wazi kama kutoka na damu.

Dalili za kutoka kwa mimba:A.Maumivu ya mgongoB.KuharishaC.KichefuchefuD.Maumivu ya maeneo ya nyonga na kiuno kama unahisi unataka kuingia kwenye siku zakoE.Maumivu makali ya tumboF.Kutokwa na majimaji kwenye uke.G.Kutokwa na vitu kama vijioande vya nyama vijidogo kwenye ukeH.Uchovu mkali sana usio na sababuI.Kupotea kwa dalili nyingine za ujauzitoJ.Kutokwa na damu mabonge manonge ama damu nyingi

 

Kumbuka hizi ni dalili tu, unaweza kuwa nazo na ujauzito ukawa salama kabisa. Ukiona unahisi dalili hizo muone daktari atathibitisha vyema kwa vipimo ikiwemo utrasound ama kuangalia kiwango cha homoni ya ujjauzito kwneye damu yako.

 

Ni zipi sababu za kutoka kwa mimba?Mara nyingi kutoka kwa ujauzito kunaweza kusababishwa na chromosomal abnormalities. Hili ni tatizo la kigenetics. Hapa seli za mtoto zinashindwa kugawanyika vyema na kukuza mtoto. Sababu nyingine za kutoka ujauzito ni:-A.Matatizo katika homoni kuwa nyingi sana ama kidogo sanaB.Kama mama mjamzito ana kisukari na hafuati masharti vyemaC.Mazingira yanaweza kuchangia kama kuna mionzi hatari kama ya madini ya uraniumD.Maambukizi na mashambulizi ya vijidudu kama bakteria kwenye via vya uzazi.E.Shida katika mlango wa uzazi (cevix)F.Kutumia madawa kiholela ama kutumia madawa kusudi kwa lengo la kutoa ujauzitoG.Ugonjwa wa endometriosis (kuvimba kwa kuta za mji wa mimba “uterus”)H.Magonjwa ya ngono kama gonoria

 

Sababu nyingine za kutoka kwa mimbaA.Utapia mloB.Kuwa na kitambiC.Matumizi ya vilevi na sigaraD.Maradhi ya tezi ya thyroidE.Shinikizo la damu la juu sana

NITAZUIAJE MIMBA KUTOKA?Mimba nyingi zinazotoka husababishwa na genetics ama mambo ya kiafya ambayo si rahisi kuzuilika. Hivyo kwa mimba hizi ni ngumu sana kuzuia kutoka kwake. Hata hivypo kitu ambacho unaweza kukifanya ni kuhakikisha kuwa unabakia katika afya salama kabla na baada ya kubeba ujauzito. Fafya mabo yafuatayo yatasaidia katika kuboresha afya yako na kuzuia kiutoka kwa ujauzito:-

 

A.Kula mlo kamili wenye virutubisho (balanced diet)B.Fanya mazoezi mara kwa mara. Si lazima eti mazoezi ya kukutoa mijasho, unaweza kufanya mazoezi ya viungo pia hata ukiwa kitandani.C.Wacha ama punguza kutumia pombe, sigara ama dawa za kulevya.D.Punguza unywaji wa chai kama unakunywa kwa wingi kupitiliza. Hapa ninazungumzia chai ya majani ya chai ambayo ina caffein.E.Fanya uchunguzi wa afya yako mara kwa mara.F.Wacha kutumia dawa kiholelaG.Jiepushe na mambo ambayo yataweza kuwa ni hatari kwa ujauzito kama kupigana ama miereka.H.Fuata maelekezo vyema kutoka kwa wahudumu wa afya.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1774

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 web hosting    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

tuseme nilifanya ngono jana na leo nipata period,je kuna uwezekano wa kupata mimba

Mimba inatungwa katika siku maalumu na hazizidi 10. Sio kila ukishiriki tendo unaweza pata mimba. Je unaweza kupata mimba baada ya kushiriki tendo wiki moja kabla ya kuingia hedhi?

Soma Zaidi...
Kuwepo kwa maziwa wakati wa ujauzito.

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa maziwa kwa akina Mama wakati wa ujauzito ni kawaida kwa sababu ya kuzaliwa kwa homoni ambayo usaidia kutoa maziwa.

Soma Zaidi...
Mimi imepita miezi mitatu sioni hedhi na wala sioni dalili ya kuwa na mimba unaweza ukaniambia tatizo la kuwa na hali hii

Kama na wewe una tatizo la kupitiliza siku zako za hedhi hli ya kuwa huna ujauzito, soma post hii ina majibu yako.

Soma Zaidi...
Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Posti hii inaelezea kiufupi kabisa kuhusiana na Dalili za hatari kwa mama aliyejifungua.

Soma Zaidi...
Sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa.

Posti hii inahusu zaidi sababu za mfuko wa kizazi kushindwa kisinyaa, ni sababu ambazo utokea kwa akina Mama wengi kadri ya wataalamu wametafuta asilimia kuwa asilimia sabini ya wanawake mifuko yao ya kizazi kushindwa kisinyaa.

Soma Zaidi...
Uume ukiwa unaingia na ukiwa ndani nahic maumivu Kama uke unawaka Moto tafadhali nishauri

Je unasumbuliwa namaumivi wakati wa nlishiriki tendo la ndoa ama baada. Huwenda post hii ikakusaidia.

Soma Zaidi...
Dalili za uchungu

Uchungu wa uzazi hutokana na kubana nakuachia kwa misuli hii husababishwa kufunhuka kwa mlango wa tumbo la uzazi pamoja na shingo ya kizazi na kumuongezea mama uchungu wakati wa kujifungua(during labour) Pia kubana na kuachia huanza polepole wakati wa

Soma Zaidi...
Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa watoto, sio akina Mama peke yao wanaofaidika na uzazi wa mpango vile vile na watoto wanafaidika na uzazi wa mpango kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...