Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.
Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo.
Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.
1. Sababu ya kwanza ni pale mtoto anaposhindwa kuzunguka na kuruhusu bega lipite.
Kwa kawaida ili mtoto aweze kuzaliwa kabla ya kumvuta kutoka kwa mama ni lazima kubadilisha upande au kuzungusha upande ili kuruhusu bega kupita ila kuna watoto wengine hawafanyi hivyo kutokana na sababu mbalimbali hali inayosababisha watoa huduma kuvuta mtoto kwa nguvu wakiwa na lengo la kuokoa maisha ya Mtoto na hatimaye baadhi ya nevu kuachia na kusababisha mtoto kuvunjika hasa hasa kwenye bega na shingo kwa hiyo utaona shingo la mtoto linacheza cheza na mkono hauna nguvu.
2. Pengine kinachosababisha mtoto kuvunjika ni mtoto juwa na uzito mkubwa.
Kwa kawaida uzito wa mtoto ni kuanzia kilo mbili na nusu mpaka tatu na nusu ila kuna watoto wengine unakuta wana uzito kuanzia nne mpaka tano kwa hiyo kuja kutoka nje wakati wa kuzaliwa ni shida nguvu za ziada zinapaswa kutumika ili kuweza kumvuta mtoto ili atoke nje katika kupambana na hali hii usababisha mtoto kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kama vile mkono, shingo na kupata maumivu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
3. Mtoto kutanguliza matako
Hali hiyo pia usababisha mtoto kuvunjika kwa sababu kuja kumzalisha mtoto wa hivi kwa sababu pengine anakiwa ametanguliza matako na mguu mwingine unakuwa umejikunja kwa hiyo kuja kuutoa unakuta umevunjika.
4. Mtoto kukaa vibaya.
Unaweza kukuta mtoto katanguliza mkono mmoja mwingine umejikunja hali ambayo usababisha kuvunjika kwa mkono uliojikunja kwa sababu hujui umejikunjia wapi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 web hosting 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu,ni madhara ambayo utokea kwa mtu anayetumia madawa ya kupunguza maumivu.
Soma Zaidi...Jinsi ya kuongeza nguvu za kiume
Post hii itakwenda kukuletea orodha ya vyakla vinavyoaminika kuongeza nguvu za kiume.
Soma Zaidi...Chanzo cha tezidume, dalili zake na tiba zake.
Post hii inakwenda kukufunza mambo mengi kuhusu tezi dume kama chanzo, dalili, matibabu, njia za kujikinga na mambo hatari yanayoweza kukusababishia kupata tezi dume.
Soma Zaidi...Dalili za kupata uvimbe kwenye kizazi (fibroid)
Post hii inaenda kufundisha kuhusiana na uvimbe wa kizazi kwa wanawake. Uvimbe wa kizazi no uvimbe ambao hutokea kwenye tumbo la kizazi ambao unaweza kuwa ndan ya kizazi uvimbe huu ndan ya mwanamke hujulikana kama (uterine myoma au fibroid). Uvi
Soma Zaidi...Dalili za mimba inayotishi kutoka
Posti hii inahusu zaidi dalili za mimba inayotaka kutoka yenyewe, Kuna wakati mwingine mama anabeba mimba na mimba hiyo I atishia kutoka na huwa inaonyesha dalili mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni dalili za mimba kutaka kutoka yenyewe.
Soma Zaidi...Je ukitokea mchubuko wakati wa ngono unaweza pata ukimwi?
Kupata Ukimwi ama HIV hufungamana na mambo mengi. Si kila anayefanya ngono zembe nabmuathiria naye lazima aathirike. Hiivsibkweli, ila tangu kuwa hali hii ni hatari kwani kupata maambukizi ni rahisi sana.
Soma Zaidi...