Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo.
Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.
1. Sababu ya kwanza ni pale mtoto anaposhindwa kuzunguka na kuruhusu bega lipite.
Kwa kawaida ili mtoto aweze kuzaliwa kabla ya kumvuta kutoka kwa mama ni lazima kubadilisha upande au kuzungusha upande ili kuruhusu bega kupita ila kuna watoto wengine hawafanyi hivyo kutokana na sababu mbalimbali hali inayosababisha watoa huduma kuvuta mtoto kwa nguvu wakiwa na lengo la kuokoa maisha ya Mtoto na hatimaye baadhi ya nevu kuachia na kusababisha mtoto kuvunjika hasa hasa kwenye bega na shingo kwa hiyo utaona shingo la mtoto linacheza cheza na mkono hauna nguvu.
2. Pengine kinachosababisha mtoto kuvunjika ni mtoto juwa na uzito mkubwa.
Kwa kawaida uzito wa mtoto ni kuanzia kilo mbili na nusu mpaka tatu na nusu ila kuna watoto wengine unakuta wana uzito kuanzia nne mpaka tano kwa hiyo kuja kutoka nje wakati wa kuzaliwa ni shida nguvu za ziada zinapaswa kutumika ili kuweza kumvuta mtoto ili atoke nje katika kupambana na hali hii usababisha mtoto kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kama vile mkono, shingo na kupata maumivu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
3. Mtoto kutanguliza matako
Hali hiyo pia usababisha mtoto kuvunjika kwa sababu kuja kumzalisha mtoto wa hivi kwa sababu pengine anakiwa ametanguliza matako na mguu mwingine unakuwa umejikunja kwa hiyo kuja kuutoa unakuta umevunjika.
4. Mtoto kukaa vibaya.
Unaweza kukuta mtoto katanguliza mkono mmoja mwingine umejikunja hali ambayo usababisha kuvunjika kwa mkono uliojikunja kwa sababu hujui umejikunjia wapi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza uke, tunajua wazi kuna magonjwa mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo uke hautaweza kutunzwa vizuri na pia uke ukitunzwa vizuri kuna faida ya kuepuka maradhi ya wanawake kwa njia ya kutunza uke.
Soma Zaidi...Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi?
Soma Zaidi...Download Kitabu cha elimu ya Ujauzito na malezi ya mimba.
Soma Zaidi...Miongoni mwa changamoto za ujauzito ni maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanawezakuwaya kawaida ama makali zaidi. Vyema kufika Kituo cha Afya endapoyatakuwa makali.
Soma Zaidi...Dalili za kuharibika kwa ujauzito na dalili za kuharibika kwa ujauzo
Soma Zaidi...Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za mtoto kuzaliwa akiwa na miezi Saba na nane kwa kawaida mtoto wa hivi anakuwa hajafikisha mda wake kwa hiyo uzaliwa akiwa na miezi saba na nane, kwa hiyo kuna sababu mbalimbali kama tutakavyoona
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.
Soma Zaidi...