picha

Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.

Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo.

Sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.

1. Sababu ya kwanza ni pale mtoto anaposhindwa kuzunguka na kuruhusu bega lipite.

Kwa kawaida ili mtoto aweze kuzaliwa kabla ya kumvuta kutoka kwa mama ni lazima kubadilisha upande au kuzungusha upande ili kuruhusu bega kupita ila kuna watoto wengine hawafanyi hivyo kutokana na sababu mbalimbali hali inayosababisha watoa huduma kuvuta mtoto kwa nguvu wakiwa na lengo la kuokoa maisha ya Mtoto na hatimaye baadhi ya nevu kuachia na kusababisha mtoto  kuvunjika hasa hasa kwenye bega na shingo kwa hiyo utaona shingo la mtoto linacheza cheza na mkono hauna nguvu.

 

2. Pengine kinachosababisha mtoto kuvunjika ni mtoto juwa na uzito mkubwa.

Kwa kawaida uzito wa mtoto ni kuanzia kilo mbili na nusu mpaka tatu na nusu ila kuna watoto wengine unakuta wana uzito kuanzia nne mpaka tano kwa hiyo kuja kutoka nje wakati wa kuzaliwa ni shida nguvu za ziada zinapaswa kutumika ili kuweza kumvuta mtoto ili atoke nje katika kupambana na hali hii usababisha mtoto kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kama vile mkono, shingo na kupata maumivu kwenye sehemu mbalimbali za mwili.

 

3. Mtoto kutanguliza matako 

Hali hiyo pia usababisha mtoto kuvunjika kwa sababu kuja kumzalisha mtoto wa hivi kwa sababu pengine anakiwa ametanguliza matako na mguu mwingine unakuwa umejikunja kwa hiyo kuja kuutoa unakuta umevunjika.

 

4. Mtoto kukaa vibaya.

Unaweza kukuta mtoto katanguliza mkono mmoja mwingine umejikunja hali ambayo usababisha kuvunjika kwa mkono uliojikunja kwa sababu hujui umejikunjia wapi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2760

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 web hosting     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Dalili za kuziba kwa mirija ya uzazi

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea kwa sababu ya kuziba kwa mishipa ya uzazi, ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo la kuziba kwa mishipa ya uzazi.

Soma Zaidi...
Hatua Saba za kutibu au kuepuka uvimbe kwenye kizazi

Posti hii inahusu zaidi hatua ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kutibu uvimbe au kwa kitaalamu huitwa fibroids. Hizi hatua zikitumika uweza kusaidia kupunguza kiwango cha kupata au kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.

Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h

Soma Zaidi...
Malezi ya mtoto mchanga na mama mjamzito

Post hii itakwenda kukuletea mambo kadhaa yanayohusiana na malezi bora ya mama mjamzito na mtoto mchanga

Soma Zaidi...
Kiungulia kwa wajawazito, dawa yake na njia za kukabilianannacho

Wajawazito wamekuwa wakisumbuliwa sana na kiungulia, makala hii itakujulisha njia za kukabiliana na kiungulia, dalili zake na dawa zake

Soma Zaidi...