Sababu za kuwepo fangasi ukeni
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa Ugonjwa wa fangasi,ni sababu mbalimbali ambazo zinaweza kusababisha fangasi.
Sababu za kuwepo kwa fangasi ukeni.
1. Mabadiliko ya homoni yaani vichocheo.
Kuna wakati mwingine vichocheo vya mwili usababisha kuwepo kwa fangasi ukeni hasa wakati wa uchevushaji wa mayai,uja uzito, uzazi wa mpango na kukoma kwa hedhi, kutokana na hali hizo usababisha kuwepo kwa fangasi.
2. Kuwepo kwa upungufu wa kinga mwilini.
Kwa kawaida kinga ya mwili ikipungua kila ugonjwa unakuwepo kwa hiyo watu wale wenye magonjwa ya kupunguza kinga ya mwili wako kwenye hatari Kupata fangasi za ukeni ,kama vile wenye kansa, Ukimwi na magonjwa makubwa makubwa wako kwenye hatari ya kupata tatizo la fangasi ukeni.
3. Wenye ugonjwa wa kisukari.
Kwa kawaida walio na Ugonjwa wa kisukari wana sukari nyingi mwilini kwa hiyo na fangasi wanapenda sana sukari na pia wenye kisukari hasa cha mda mrefu wanakuwa katika hatari ya kupungua kwa kinga ya mwili.
4. Kuwepo kwenye mazingira ya joto.
Kwa kawaida watu wanaopenda kuvaa nguo zinazoingiza joto hasa za siri wako kwenye hatari ya kupata tatizo la fangasi ukeni, kwa hiyo ni vizuri kuvaa nguo ambazo haziruhusu joto kuingia kwenye shehemu za siri.
5. Matumizi ya kondomu na mbegu za kiume.
Kwa wale wote wanaotumia sana kondomu wakati wa kujamiiana wako katika hatari ya kupata fangasi ukeni.
6. Walio na vidonda kwenye sehemu za siri.
Kwa sababu ya kuwepo kwa wa aina ya uwazi kwenye sehemu za siri kama vile vidonda ni rahisi sana kuingiwa na fangasi kwenye sehemu za siri.
7. Kutumia sabuni wakati wa kujitawadha
Kwa kawaida kama mtu anajitawadha na sababu anaua bakteria wazuri na kusababisha kuwepo kwa fangasi ukeni
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 web hosting 👉3 ai web app 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Nini husababisha korodani moja kuwa kubwa kuliko nyingine
kama pumbu moja ni kubwa uliko jingine post hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakwend akuangalia vinavyoweza kusababisha korodani moja kuw akubwa zaidi ya lingine
Soma Zaidi...Dali za udhaifu wa mbegu za kiume.
Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo zinaweza kujitokeza na zikaonesha kwamba mbegu za kiume ni dhaifu au ni chache.
Soma Zaidi...Watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango
Post hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango, Ni watu ambao Wana matatizo mbalimbali endapo wakitumia wanaoweza kuleta madhara mbalimbali.
Soma Zaidi...Wajibu wa mjamzito katika utaratibu wa uleaji wa mimba
Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote.
Soma Zaidi...Je nitahakikisha vipi Kama Nina ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuhakiki Kama u-mjamzito
Soma Zaidi...