picha

Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni

Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i

SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI

1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika kama gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.

 

2. Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika kama appendicitis. Kama utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili.

 

3.Vidonda vya tumbo

Yes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika kama duodenum.

 

3. Matatizo kwenye kongosho

Huu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali.

 

5.Kuwa na ngriri ya henia

Ugonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.

 

6.Kama kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-

1.Mashambulizi ya bakteria

2.Henia

3.Uvimbe

4.Kama kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.

 

7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu kama mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.

 

8.Kama kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili kama:-

1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo

2.Kuona damu kwenye choo

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 13062

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia

Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia

Soma Zaidi...
ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3

Habari, samahani ninasumbuliwa Sana na mapunye ya kichwani nimetumia dawa takribani miaka 3 ila yanapona Tena baada ya Muda flani yanatokea.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa schizophrenia

Schizophrenia ni ugonjwa wa akili ambao huathiri jinsi mtu anavyofikiri, kuhisi, na kuamua. Dalili za schizophrenia zinaweza kuwa kama ifuatavyo hapo chini

Soma Zaidi...
DALILI ZA UTUMBO KUZIBA

Kuziba kwa utumbo ni kuziba kwa chakula au kimiminika kisipite kwenye utumbo mwembamba au utumbo mpana (colon). Kuziba kwa matumbo kunaweza kusababishwa na mikanda ya nyuzi kwenye fumbatio ambayo huunda baada ya upasuaji, mifuko iliyovimba au iliyoambuk

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa dondakoo

Dondakoo ni ugonjwa mbaya unaosababishwa na sumu inayotengenezwa na bakteria. Husababisha mipako nene nyuma ya pua au koo ambayo inafanya kuwa ngumu kupumua au kumeza. Inaweza kuwa mauti.

Soma Zaidi...
Athari za kula vyakula vyenye sukari nyingi kila siku.

Katika ulimwengu wa sasa, sukari imekuwa kiungo kikuu katika vyakula vingi vilivyosindikwa, hali inayochangia kwa kiasi kikubwa magonjwa yasiyoambukiza. Makala haya yanachambua athari za muda mrefu za ulaji wa sukari nyingi, ikizingatia afya ya moyo, uzito wa mwili, na utendaji wa kimetaboliki, huku ikitoa mikakati ya kitaalamu ya kupunguza matumizi ya sukari kwa maisha marefu na yenye tija.

Soma Zaidi...