picha

Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni

Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i

SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI

1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika kama gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.

 

2. Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika kama appendicitis. Kama utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili.

 

3.Vidonda vya tumbo

Yes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika kama duodenum.

 

3. Matatizo kwenye kongosho

Huu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali.

 

5.Kuwa na ngriri ya henia

Ugonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.

 

6.Kama kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-

1.Mashambulizi ya bakteria

2.Henia

3.Uvimbe

4.Kama kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.

 

7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu kama mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.

 

8.Kama kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili kama:-

1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo

2.Kuona damu kwenye choo

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 12912

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Athari za unywaji wa pombe kupita kiasi kwenye Ini.

Ini ni kiungo cha ajabu chenye kazi nyingi, ikiwemo kusafisha sumu mwilini, kutengeneza protini, na kusaidia mmeng'enyo wa chakula. Hata hivyo, ini lina uwezo mdogo wa kuhimili kiasi kikubwa cha pombe. Unywaji wa pombe kupita kiasi hauumizi tu "roho" ya mtu, bali husababisha uharibifu wa kimwili kwa ini ambao unaweza kuwa wa kudumu. Makala haya yanaelezea mzunguko wa uharibifu huo na kwa nini ni muhimu kuelewa hatari hizi.

Soma Zaidi...
Dalili za ngozi kuwasha.

Posti hii inaonyesha kiufupi kabisa kuhusiana na dalili za ngozi kuwashwa.

Soma Zaidi...
Vyakula vinavyosaidia afya ya mwanaume

Afya ya mwanaume inahitaji muundo wa kipekee wa virutubisho ili kulinda moyo, kuongeza nguvu za mwili, kusawazisha homoni ya testosterone, na kuzuia matatizo ya tezi dume (prostate). Makala haya yanachambua vyakula vikuu vyenye uwezo wa kuimarisha afya ya wanaume, jinsi vinavyofanya kazi, na kuondoa dhana potofu zilizopo mitaani kuhusu vyakula vya kuongeza nguvu za kiume. ​Utangulizi

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya ini.

posti inaonyesha dalili mbalimbali za Saratani ya ini. Saratani ya ini ni Saratani inayoanzia kwenye seli za ini lako. Ini lako ni kiungo cha ukubwa wa mpira wa miguu ambacho kinakaa sehemu ya juu ya kulia ya tumbo lako, chini ya diaphr

Soma Zaidi...
Madhara ya fangasi.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya fangasi za ukeni kwa kawaida tunajua kubwa fangasi zikiingia kwenye uke usababisha madhara mbalimbali ambayo mengine yanaweza ya kudumu na mengine ya mda kama yametibiwa mapema.

Soma Zaidi...
Nini chanzo cha malaria

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu chanzo cha ugonjwa wa malaria

Soma Zaidi...