picha

Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni

Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i

SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI

1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika kama gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.

 

2. Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika kama appendicitis. Kama utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili.

 

3.Vidonda vya tumbo

Yes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika kama duodenum.

 

3. Matatizo kwenye kongosho

Huu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali.

 

5.Kuwa na ngriri ya henia

Ugonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.

 

6.Kama kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-

1.Mashambulizi ya bakteria

2.Henia

3.Uvimbe

4.Kama kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.

 

7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu kama mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.

 

8.Kama kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili kama:-

1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo

2.Kuona damu kwenye choo

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 13276

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰5 ai web app     πŸ‘‰6 web hosting    

Post zinazofanana:

Tabia za kujikosoa kupita kiasi na jinsi ya kujenga upendo

​Katika ulimwengu wa kisasa, shinikizo la kuwa "mkamilifu" mara nyingi husababisha watu wengi kuangukia katika mtego wa kujikosoa kupita kiasi. Makala haya yanachunguza asili ya sauti hii ya ndani (inner critic), madhara yake katika afya ya akili, na kutoa mwongozo wa hatua kwa hatua wa jinsi ya kugeuza mtazamo huo kuwa upendo na huruma kwa nafsi yako (self-compassion).

Soma Zaidi...
Kazi ya kongosho na athari za ugonjwa wa kisukari.

Kongosho ni kiungo muhimu katika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula na udhibiti wa homoni mwilini. Ugonjwa wa kisukari hutokea pale kongosho inaposhindwa kufanya kazi zake ipasavyo, hasa katika uzalishaji wa insulini. Makala hii inachunguza kwa kina kazi za kongosho, uhusiano wake na ugonjwa wa kisukari, athari za muda mrefu za ugonjwa huu, na mbinu za kitaalamu za kuzuia na kudhibiti hali hii ili kulinda afya ya kongosho na mwili kwa ujumla.

Soma Zaidi...
Namna ya kuishi na vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuishi na vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Matibabu ya vidonda vya tumbo

Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu matibabu ya vidonda vyatumbo. Pia utajifunza kwa nini kunakuwa na vidonda vya tumbo sugu.

Soma Zaidi...
nina maambukizi ya zinaha maumivu wakati wa kukojoa na usaha

Mimi nilifanya ngono isiyo salama Tar 14/07 mwaka huu, nilikutana tu na mwanamke ambae sikuwa hata na background yake yoyote hivyo baada ya siku tatu nilijikuta nina maambukizi ya zinaha (maumivu wakati wa kukojoa na usaha), hivyo nilienda hospital na kup

Soma Zaidi...