Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni
Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i
SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI
1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika kama gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.
2. Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika kama appendicitis. Kama utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili.
3.Vidonda vya tumbo
Yes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika kama duodenum.
3. Matatizo kwenye kongosho
Huu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali.
5.Kuwa na ngriri ya henia
Ugonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.
6.Kama kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-
1.Mashambulizi ya bakteria
2.Henia
3.Uvimbe
4.Kama kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.
7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu kama mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.
8.Kama kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili kama:-
1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
2.Kuona damu kwenye choo
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π2 Kitabu cha Afya π3 Simulizi za Hadithi Audio π4 Kitau cha Fiqh π5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Athari za unywaji wa pombe kupita kiasi kwenye Ini.
Ini ni kiungo cha ajabu chenye kazi nyingi, ikiwemo kusafisha sumu mwilini, kutengeneza protini, na kusaidia mmeng'enyo wa chakula. Hata hivyo, ini lina uwezo mdogo wa kuhimili kiasi kikubwa cha pombe. Unywaji wa pombe kupita kiasi hauumizi tu "roho" ya mtu, bali husababisha uharibifu wa kimwili kwa ini ambao unaweza kuwa wa kudumu. Makala haya yanaelezea mzunguko wa uharibifu huo na kwa nini ni muhimu kuelewa hatari hizi.
Soma Zaidi...Samahan naomb kujua staili za tendo la ndoa
Post hii inakwenda kujibu swali la muulizaji. Kuhusu syyle za tendo la ndoa
Soma Zaidi...Namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni
Post hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni, ni njia zinazotumika kuzuia maambukizi kwenye nephroni
Soma Zaidi...Sababu za Mtoto Kuharisha Mara kwa Mara
βUharishaji kwa watoto ni changamoto ya kawaida inayoweza kusababishwa na maambukizi, lishe, au mabadiliko ya kifizikia. Makala haya yatafafanua sababu kuu za tatizo hili, jinsi ya kukabiliana nalo nyumbani, na wakati mwafaka wa kumpeleka mtoto hospitalini.
Soma Zaidi...Dalili na ishara za Ugonjwa wa akili.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa akili .
Soma Zaidi...Tiba ya vidonda vya tumbo na dawa zake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Tina ya vidonda vya tumbo na dawa zake
Soma Zaidi...