image

Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni

Somo hili linakwenda kukuletea sababu za maumivu ya tumbo kitovu i

SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI

1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika kama gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.

 

2. Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika kama appendicitis. Kama utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili.

 

3.Vidonda vya tumbo

Yes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika kama duodenum.

 

3. Matatizo kwenye kongosho

Huu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali.

 

5.Kuwa na ngriri ya henia

Ugonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.

 

6.Kama kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-

1.Mashambulizi ya bakteria

2.Henia

3.Uvimbe

4.Kama kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.

 

7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu kama mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.

 

8.Kama kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili kama:-

1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo

2.Kuona damu kwenye choo





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 4936


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Dalili na Sababu za homa ya manjano kwa watoto
Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili na Sababu za Homa ya manjano ya watoto wachanga ni kubadilika rangi kwa manjano katika ngozi na macho ya mtoto mchanga. Homa ya manjano ya mtoto hutokea kwa sababu damu ya mtoto ina ziada ya rangi ya Soma Zaidi...

Je vvu inaweza sababisha mate kujaa mdomoni
Je kujaa kwa mate mdomoni ni dalili ya kuwa na VVU, na je ni zipi dalili za Virusi Vya Ukimwi (VVU) mdomoni? Soma Zaidi...

Ugonjwa wa kisonono
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisonono, ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu huitwa Neisseria gonococcal. Soma Zaidi...

Namna ya kutoa huduma kwa mgonjwa wa Dengue.
Posti hii inahusu zaidi huduma anayopaswa kupata mgonjwa wa ndengue, kwa sababu tunafahamu wazi Ugonjwa huu hauna dawa ila kuna huduma muhimu ambayo anaweza kupata na akaendelea vizuri. Soma Zaidi...

Sababu zinazopelekea tumbo kujaa gesi
Kiufipi posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na sababu zinazopelekea tumbo kujaa gesi Soma Zaidi...

Je mtu akapima ukimwi na kile kipimo kidogo .je kina usahihi au la ..na pia kama inaonyesha mistari miwili.
Hivi umeshawahi kuwazakuwa jekipimo cha HIV ni sahihi kwa kiasi gani. Unadhani huwa kinakoseaga kutoa majibu? Soma Zaidi...

Sasa UKIMWI unatokeaje?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo UKIMWI hutokea Soma Zaidi...

Namna ya kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo,ni njia ambazo mtu anaweza kutumia Ili kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.zifuatazo ni njia zinazoweza kutumika kama mtu amepata uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo. Soma Zaidi...

Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis. Soma Zaidi...

Dalili za mawe kwenye kibofu Cha mkono
Mawe ya kibofu ni mkusanyiko mgumu wa madini kwenye kibofu chako. Mawe kwenye kibofu hukua wakati mkojo kwenye kibofu chako unapokolea, na kusababisha madini katika mkojo wako kung'aa. Soma Zaidi...

Dalili za ugonjwa wa Donda koo
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Donda Koo ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea viitwavyo kwa kitaalamu corynebacterium diphtheria, ugonjwa huu ushambulia Koo na unaweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa, mate na Soma Zaidi...

Saratani ya tishu zinazounda Damu mwilini (leukemia)
Post hii inaelezea kuhusiana na Saratani ya tishu zinazounda damu mwilini, ikijumuisha uboho na mfumo wa limfu.ugonjwa huu kitaalamu huitwa leukemia. Soma Zaidi...