Sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa

Post hii inahusu zaidi sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa,ni sababu ambazo uweza kuchangia kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa.

Sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa.

1. Sababu ya kwanza vifaa vinavyotumika kuzalisha watoto.

Kuna wakati mwingine vifaa vinavyotumika kuzalisha watoto usababisha kuchubuka kwa mtoto inawezekana kabisa ni kwa kuchubuka kwa ndani au kuchubuka kwa ngozi ya nje, Kuna Kipindi mtoto anakuwa ameshatoa kichwa ila kutoka nje huwa ni shida na hata kama mama akisukuma kwa namna gani mtoto hawezi kutoka hali inayosababisha  vifaa mbalimbali kutumika Ili kuweza kumtoa mtoto nje na kuokoa maisha ya mtoto na Mama kwa hiyo katika kimvuta mtoto atoke usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa kwa hiyo ni vizuri kabisa wataalamu wa afya na wahudumu wa mtoto aliyevutwa kwa kutumia vyuma kuangalia mara kwa mara Ili kuweza kugundua kama michubuko ni ya ndani au ya nje na kuweza kutumia matibabu.

 

2. Pia michubuko utokea mara nyingi kwa watoto wanaozaliwa kwa kutanguliza matako, kwa kawaida mtoto anapaswa kutanguliza kichwa ikitokea mtoto akatanguliza matako, au miguu usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa,kwa sababu matako na miguu uweza kuzaliwa ila Kuna Kipindi mabega na mikono ushindwa kutoka, katika kupambana ili kuweza kutoa mikono na mabega au pengine kichwa usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa, na pia sio michubuko tu kwa wakati mwingine ulemavu wa mikono na mabega uweza kutokea kwa watoto, kwa hiyo kwa akina mama wanaojifungua ikitokea mtoto alikuwa ametanguliza matako au miguu na akazaliwa kwa shida kwa kupambana ni vizuri kabisa kuangalia mabadiliko yoyote na kumwambia wataalamu wa afya Ili kuweza kuepuka madhara mengine zaidi.

 

3. Mtoto kutanguliza mabega.

Kuna wakati mwingine mtoto anaweza kutanguliza kichwa na kichwa kikazaliwa ila mabega yakakwama kwenye mfupa wa mama ambao kwa kitaamu huiitwa pubic bone, kwa hiyo katika kupambana kuzalisha mabega Ili mtoto atoke usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa, kwa hiyo ni vizuri kabisa kujua dalili za mtoto aliyetanguliza mabega Ili kuweza kutafuta mbinu za kuzalisha mama huyo au kutafuta wataalamu zaidi, na dalili ambazo ujitokeza ni kama zifuatazo.

  1. Mtoto anaweza kutoa kichwa vizuri kabisa ila badala ya kuendelea kawaida kichwa uanza kurudi tena nyuma kilipotoka ,kwa wakunga dalili hii uinesha kwamba mabega bado hayajatoka.
  2. Pia kuzunguka kwa mtoto upungua ambapo kitendo hiki kwa kitaamu huiitwa decreasing of restitution, kwa kawaida mtoto akitoa kichwa uzunguka Ili kuweza kuruhusu na bega litoke ila kwa sababu mabega hayajatoka mtoto hawezi kuendelea na kuzunguka tena.

Mama huwa na wasiwasi mkubwa kuliko kawaida na pia uhisi kitu ambacho sio cha Kawaida kwa hiyo kwa wahudumu wa afya ni vizuri kabisa kuwa karibu na mama Ili kuweza kumweka mama kwenye hali nzuri na ya kwamba kila kitu kitakuwa sawa.

 

4.Kichwa cha mtoto kutolingana na kiuno cha mama kwa pale mtoto anapopaswa kupitia.

Kwa kawaida kichwa cha mtoto ni lazima kabisa kulingana na kiuno cha mama kwa pale mtoto anapopaswa kupitia, hali ambayo usababisha mtoto kutumia nguvu nyingi Ili kutoka nje ,hali hii kwa kitaamu huiitwa disproportionate pelvic, kwa hiyo kabla ya mama kujifungua ni lazima kujua hali halisi ya mtoto anapotaka kujifungua kama anaweza kupita au hawezi kupita kwa kufanya hivyo tunaweza kuepuka matatizo mbalimbali kwa watoto kama vile kuchubuka na ulemavu mwingine kama huo.

 

5. Na tatizo jingine mama kukaa kwenye Kipindi cha kujifungua kwa mda mrefu , yaani kwa kitaamu huiitwa prolonged labor.

Ni hali ambayo mama huwa na uchungu wa mda mrefu na pia anakaa kwenye uchungu kwa mda huo inawezekana ukawa mchache ule ambao haiwezekani mtoto kuzaliwa, kwa hiyo mtoto uchoka na kwa pengine usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa,

 

6. Vile vile Kuna hali ya uchungu kuwa mkali na kichwa cha mtoto hakishuki chini, kwa kitaamu huiitwa obstruction labour.

Hii ni Sina ya labor ambapo uchungu unakuwepo wa kutosha lakini kichwa cha mtoto hakishuki, kwa sababu uchungu upo na mtoto anapambana kutoka ila kichwa hakishuki kwa hiyo hali hiyo usababisha kuchoka kwa mtoto na pia mtoto uweza kupata michubuko,hali hii pia usababisha mama kupasuka kizazi na kusababisha kupoteza mtoto na pia kuleta matatizo kwa mama na pengine kizazi kikisha pasuka usababisha kutolewa hali hii inaweza kumfanya mama kushindwa kupata naomba ya watoto aliokusudia kupata.

 

7. Pengine hali inayosababisha kupata michubuko kwa watoto ni pamoja na uchungu kuwa mkubwa zaidi na WA mda mfupi, kwa kitaamu huiitwa precipitate labor.

Ni aina ya uchungu ambao utokea kwa akina mama kwa kawaida utokea kwa mda mfupi na pia mama uweza kujifungua kwa mda mfupi huo, kwa kawaida uchungu huo utumia masaa matatu tu, na pia mtoto uweza kuzaliwa, kwa hiyo mtoto ni kama vile anatoka kwa spidi kubwa na kujibamiza kwenye mifupa mbalimbali ya kiuno cha mama na kusababisha hali ya  michubuko.

 

6. Kwa hiyo akina mama wanapaswa kuwa makini katika Kipindi cha ujauzito kwa sababu Kuna vitu vingine ambavyo usababisha madhara kwa watoto na vile vile akina mama wanapaswa kuhudhuria Kipindi cha mahudhulio yote wakati wa ujauzito Ili kuweza kugundua dalili za hatari na mambo ambayo usababisha michubuko na matatizo mengi mbalimbali .

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 1852

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰4 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Yajue malengo ya kusafisha vidonda.

Posti hii inahusu zaidi malengo ya kusafisha vidonda, kwa sababu Kuna watu wengine huwa wanajiuliza kwa nini nisafishe kidonda hospitalini au kwenye kituo chochote Cha afya, yafuatayo ni majibu ya kwa Nini nisafishe kidonda.

Soma Zaidi...
Ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia

Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia Nimonia, hii ni chanjo inayozuia hasa hasa Magonjwa ya mfumo wa hewa kwa hiyo nayo upewa watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhsu vitamini E na kazi zake mwilini

Je unazijuwa faida za kuwa na vitamini E mwilini mwako.Unahani utapata matatizo yapi ya kiafya endapo utakuwa na upungufu wa vitamini E mwilini? Makala hii ni kwa ajili yako.

Soma Zaidi...
Aina za vidonda.

Posti hii inahusu zaidi aina kuu za vidonda,kuna aina kuu tatu za vidonda ambapo kila aina utumiwa kwa njia yake kama tutakavyoona hapo chini.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu vitamini C na kazi zake

Makala hii itakujulisha kazi kuu za vitamini C mwilini. Hapa pia utatambuwa ni kwa nini tunahitaji vitamini C na wapi tutavipata

Soma Zaidi...
Upungufu wa maji

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa maji mwilini

Soma Zaidi...
Utajuwaje kama kidonda kupona

Posti hii inahusu zaidi juu ya kuhakiki kama kidonda kimepona kwa mgonjwa mwenye vidonda, kwanza kabisa tunajua kuwa vidonda uwanyima Watu raha na pengine kuwafanya wakate tamaa kama wapo hospitalini kwa hiyo tunapaswa kutumia njia zifuatazo ili kuweza ku

Soma Zaidi...
Namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ambavyo mwili unapambana na maradhi

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENGโ€™ATWA NA NYUKI

Kungโ€™atwa na nyuki kunaweza kukahitaji huduma ya kwanza kwa haraka kama mgonjwa ana aleji na nyuki.

Soma Zaidi...
Njia juu zinazosababisha kuenea kwa ugonjwa wa Ukimwi

Post hii inahusu zaidi njia za kuenea kwa ugonjwa wa Ukimwi. Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini.

Soma Zaidi...