image

Sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa

Post hii inahusu zaidi sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa,ni sababu ambazo uweza kuchangia kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa.

Sababu za michubuko kwa watoto wanaozaliwa.

1. Sababu ya kwanza vifaa vinavyotumika kuzalisha watoto.

Kuna wakati mwingine vifaa vinavyotumika kuzalisha watoto usababisha kuchubuka kwa mtoto inawezekana kabisa ni kwa kuchubuka kwa ndani au kuchubuka kwa ngozi ya nje, Kuna Kipindi mtoto anakuwa ameshatoa kichwa ila kutoka nje huwa ni shida na hata kama mama akisukuma kwa namna gani mtoto hawezi kutoka hali inayosababisha  vifaa mbalimbali kutumika Ili kuweza kumtoa mtoto nje na kuokoa maisha ya mtoto na Mama kwa hiyo katika kimvuta mtoto atoke usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa kwa hiyo ni vizuri kabisa wataalamu wa afya na wahudumu wa mtoto aliyevutwa kwa kutumia vyuma kuangalia mara kwa mara Ili kuweza kugundua kama michubuko ni ya ndani au ya nje na kuweza kutumia matibabu.

 

2. Pia michubuko utokea mara nyingi kwa watoto wanaozaliwa kwa kutanguliza matako, kwa kawaida mtoto anapaswa kutanguliza kichwa ikitokea mtoto akatanguliza matako, au miguu usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa,kwa sababu matako na miguu uweza kuzaliwa ila Kuna Kipindi mabega na mikono ushindwa kutoka, katika kupambana ili kuweza kutoa mikono na mabega au pengine kichwa usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa, na pia sio michubuko tu kwa wakati mwingine ulemavu wa mikono na mabega uweza kutokea kwa watoto, kwa hiyo kwa akina mama wanaojifungua ikitokea mtoto alikuwa ametanguliza matako au miguu na akazaliwa kwa shida kwa kupambana ni vizuri kabisa kuangalia mabadiliko yoyote na kumwambia wataalamu wa afya Ili kuweza kuepuka madhara mengine zaidi.

 

3. Mtoto kutanguliza mabega.

Kuna wakati mwingine mtoto anaweza kutanguliza kichwa na kichwa kikazaliwa ila mabega yakakwama kwenye mfupa wa mama ambao kwa kitaamu huiitwa pubic bone, kwa hiyo katika kupambana kuzalisha mabega Ili mtoto atoke usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa, kwa hiyo ni vizuri kabisa kujua dalili za mtoto aliyetanguliza mabega Ili kuweza kutafuta mbinu za kuzalisha mama huyo au kutafuta wataalamu zaidi, na dalili ambazo ujitokeza ni kama zifuatazo.

  1. Mtoto anaweza kutoa kichwa vizuri kabisa ila badala ya kuendelea kawaida kichwa uanza kurudi tena nyuma kilipotoka ,kwa wakunga dalili hii uinesha kwamba mabega bado hayajatoka.
  2. Pia kuzunguka kwa mtoto upungua ambapo kitendo hiki kwa kitaamu huiitwa decreasing of restitution, kwa kawaida mtoto akitoa kichwa uzunguka Ili kuweza kuruhusu na bega litoke ila kwa sababu mabega hayajatoka mtoto hawezi kuendelea na kuzunguka tena.

Mama huwa na wasiwasi mkubwa kuliko kawaida na pia uhisi kitu ambacho sio cha Kawaida kwa hiyo kwa wahudumu wa afya ni vizuri kabisa kuwa karibu na mama Ili kuweza kumweka mama kwenye hali nzuri na ya kwamba kila kitu kitakuwa sawa.

 

4.Kichwa cha mtoto kutolingana na kiuno cha mama kwa pale mtoto anapopaswa kupitia.

Kwa kawaida kichwa cha mtoto ni lazima kabisa kulingana na kiuno cha mama kwa pale mtoto anapopaswa kupitia, hali ambayo usababisha mtoto kutumia nguvu nyingi Ili kutoka nje ,hali hii kwa kitaamu huiitwa disproportionate pelvic, kwa hiyo kabla ya mama kujifungua ni lazima kujua hali halisi ya mtoto anapotaka kujifungua kama anaweza kupita au hawezi kupita kwa kufanya hivyo tunaweza kuepuka matatizo mbalimbali kwa watoto kama vile kuchubuka na ulemavu mwingine kama huo.

 

5. Na tatizo jingine mama kukaa kwenye Kipindi cha kujifungua kwa mda mrefu , yaani kwa kitaamu huiitwa prolonged labor.

Ni hali ambayo mama huwa na uchungu wa mda mrefu na pia anakaa kwenye uchungu kwa mda huo inawezekana ukawa mchache ule ambao haiwezekani mtoto kuzaliwa, kwa hiyo mtoto uchoka na kwa pengine usababisha kuwepo kwa michubuko kwa watoto wanaozaliwa,

 

6. Vile vile Kuna hali ya uchungu kuwa mkali na kichwa cha mtoto hakishuki chini, kwa kitaamu huiitwa obstruction labour.

Hii ni Sina ya labor ambapo uchungu unakuwepo wa kutosha lakini kichwa cha mtoto hakishuki, kwa sababu uchungu upo na mtoto anapambana kutoka ila kichwa hakishuki kwa hiyo hali hiyo usababisha kuchoka kwa mtoto na pia mtoto uweza kupata michubuko,hali hii pia usababisha mama kupasuka kizazi na kusababisha kupoteza mtoto na pia kuleta matatizo kwa mama na pengine kizazi kikisha pasuka usababisha kutolewa hali hii inaweza kumfanya mama kushindwa kupata naomba ya watoto aliokusudia kupata.

 

7. Pengine hali inayosababisha kupata michubuko kwa watoto ni pamoja na uchungu kuwa mkubwa zaidi na WA mda mfupi, kwa kitaamu huiitwa precipitate labor.

Ni aina ya uchungu ambao utokea kwa akina mama kwa kawaida utokea kwa mda mfupi na pia mama uweza kujifungua kwa mda mfupi huo, kwa kawaida uchungu huo utumia masaa matatu tu, na pia mtoto uweza kuzaliwa, kwa hiyo mtoto ni kama vile anatoka kwa spidi kubwa na kujibamiza kwenye mifupa mbalimbali ya kiuno cha mama na kusababisha hali ya  michubuko.

 

6. Kwa hiyo akina mama wanapaswa kuwa makini katika Kipindi cha ujauzito kwa sababu Kuna vitu vingine ambavyo usababisha madhara kwa watoto na vile vile akina mama wanapaswa kuhudhuria Kipindi cha mahudhulio yote wakati wa ujauzito Ili kuweza kugundua dalili za hatari na mambo ambayo usababisha michubuko na matatizo mengi mbalimbali .

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1090


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Nna swali mimi nimefanya Romance na mtu ambaye sijampima kbsa sasa naogopa anaeza kuwa mgonjwa na mm nkaupata
Muulizaji anauliza he kula denda, ama kumbusu ama kufanya romance na muathirika was HIV na wewe uta ambukizwa? Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu protini na kazi zake mwilini
Tunahitaji kuwa na protini mwilini. Kuna baadhi ya makundi ya watu wanahitaji protini zaidi. Je unawajuwa hao ni kina nana?, na je unauwa kazi za protini mwilini na athari za upungufu wake? endelea na makala hii. Soma Zaidi...

Ukiwa unalima sana unaweza kukonda
Unadhanivkufanya kazi kunaweza kukusababishia maradhi ama mwili kudhoofu, ama kukonda. Umeshawahivkujiuliza wanao nenepa huwa hawafanyi kazi? Soma Zaidi...

Njia ambazo maradhi huambukizwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo maradhi huambukizwa Soma Zaidi...

Nini husababisha kizunguzungu?
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo mbalimbali ambayo husababisha kizunguzungu. Soma Zaidi...

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPATWA NA SHAMBULIO LA MOYO
Soma Zaidi...

Namna ya kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha mwenyewe ni
Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo. Soma Zaidi...

Utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyeaha
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu utaratibu wa lishe kwa wajawazito na wanaonyonyesha Soma Zaidi...

Namna ya kusaidia vijana wakati wa kubarehe
Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia vijana wakati wa kubarehe, ni njia za kuhakikisha kuwa vijana wanakuwa na mwelekeo , Soma Zaidi...

HUDUMA YA KWANZA KWA MWENYE KIZUNGUZUNGU
Unapokuwa na kizunguzungu unashindwa kuudhibiti mwili wako, unaweza kuanguka kabisa. Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu fati na mafuta na kazi zake mwilini
Hata kama mtu atakuambbia usile vyakula yenye mafuta bado itahitajika kula tu. Kuna mafuta na fati je unajuwa utofauti wao. Ni zipi kazi zao mwilini? Endelea na makala hii Soma Zaidi...

Aina za kuungua
Post hii inahusu Aina za kuungua, kuungua ni Hali ya kubabuka kwa ngozi ya mwili na kusababisha madhara mbalimbali Soma Zaidi...