Sababu za miguu kufa ganzi.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili.
Sababu za miguu kufa ganzi.
1. Kupungua kwa virutubisho mbalimbali kwenye mwili,
Kwa kawaida mwili huwa na virutubisho mbalimbali ambavyo ufanya kazi tofautitofauti na vikiongezeka na pia uweza kuleta matatizo na vikipungua na penyewe uleta matatizo na kusababisha miguu kufa ganzi kwa hiyo kama kuna upungufu wa vitamini,B complex usababisha kuwepo kwa ganzi kwenye miguu kwa hiyo ndio maana watu wenye tatizo hili upewa dawa za vitamini B complex ili kuweza kupunguza kiwango cha ganzi mwilini.
2. Pengine kuna tatizo la matumizi ya dawa.
Matumizi ya dawa mbalimbali nazo usababisha kuwepo kwa matatizo ya kwa ganzi kwenye miguu, kwa sababu ya matumizi ya mda mrefu uweza kuleta matatizo kwa mfano kwa matumizi ya dawa za kurefusha maisha kwa wanaozitumia kwa mda mrefu usababisha kuwepo kwa ganzi kwenye miguu na pia kwa wale wanaotumia dawa za kifua kikuu nao pia wana tatizo la kuwepo kwa ganzi kwenye miguu, kwa hiyo wakishagundua tatizo hilo wanapaswa kuwahi kwa daktari ili kuweza kupata matibabu na kuendelea na hali yao ya kawaida.
3. Kuwepo kwa uzito mkubwa wa mwili.
Kuna wakati mwingine kunakuwepo na tatizo la kuwepo kwa uzito mkubwa wa mwili ambapo mwili uelemewa na jinsi ya kusafirisha damu huwa kwa shida hali ambayo Usababisha miguu kufa ganzi.
4. Kuwepo kwa Ugonjwa wa kisukari.
Kwa namna moja au nyingine kuna kipindigonjwa wa kisukari hasa wa siku nyingi upatwa na tatizo la kuwepo kwa ganzi mwilini hii ni hali ya kawaida kwa wagonjwa wa kisukari kwa hiyo wakipatwa na tatizo kama hili ni vizuri kabisa kupata matibabu ili kuweza kuendelea na maisha ya kawaida.
5. Pia na wagonjwa wenye shinikizo la damu huwa matatizo mbalimbali ambayo Usababisha pia miguu kufa ganzi kwa hiyo ni vizuri kabisa wagonjwa wa hivi wakishapata tatizo kama hili ni kujitahidi kabisa kumwona daktari ili waweze kupata msada zaidi.
6. Hili tatizo lipo na linatibika kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwaona wataalamu wa afya ili kuweza kupata msaada zaidi na kuepukana na tatizo hili.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Fahamu Ugonjwa wa hepatitis A
Hepatitis A ni ugonjwa wa kuambukiza wa ini unaosababishwa na virusi vya Hepatitis A. Virusi ni mojawapo ya aina kadhaa za virusi vya Hepatitis vinavyosababisha kuvimba na kuathiri uwezo wa ini wako kufanya kazi.
Soma Zaidi...Dalili za Dengue.
Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kichaa cha mbwa: Dalili na hatua za haraka.
Kichaa cha mbwa (Rabies) ni ugonjwa hatari wa virusi (Zoonotic disease) unaoambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu kupitia mate. Ugonjwa huu huathiri mfumo mkuu wa neva na, mara tu dalili zinapoanza kuonekana, huwa hauna tiba na husababisha kifo kwa asilimia karibu 100. Makala hii inaelezea utaratibu wa maambukizi, dalili za awali na za hatari, na hatua za dharura za kuokoa maisha pale mtu anapong'atwa na mnyama mwenye maambukizi.
Soma Zaidi...Matatizo yanayosababisha mshtuko wa moyo.
Mshtuko wa moyo hutokea wakati mtiririko wa damu kwa moyo umezuiwa, mara nyingi kwa mkusanyiko wa mafuta, cholesterol na vitu vingine, ambayo huunda plaque katika mishipa inayolisha moyo (mishipa ya moyo). Mtiririko wa damu ulioingiliwa unaweza kuharibu
Soma Zaidi...