Sababu za Ugonjwa wa kifafa cha mimba.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kifafa cha mimba, kwa kawaida mpaka sasa hakuna taarifa zozote kuhusu sababu za kuwepo kwa kifafa cha mimba ila kuna visababishi vinavyofikiliwa kama ni Dalili za kifafa cha mimba kama ifuatavyo
Sababu za kuwepo kwa kifafa cha mimba.
1. Kuwepo kwa shinikizo la damu lisilo la kawaida ambapo sio kwa sababu ya mimba ila ni kawaida ya mtu mwenye Ugonjwa huo, kwa hiyo wale wenye Tatizo la shinikizo la damu wanaweza kupata Ugonjwa huu ingawa si wote wenye shinikizo la damu kupatwa na Tatizo hili.
2.pia tatizo hili linawatokea Sana wale wanaobeba mimba za kwanza kuliko wale ambao wamebeba mimba mara nyingi, kwa hiyo wale wa mimba za kwanza wako hatarini kupata Ugonjwa huu.
3.Kwa wale wajawazito wanaopata shinikizo la damu na kiwango cha protini kuwepo kwenye mkojo wakati wa mimba ila wakijifungua tatizo hili linaisha kwa hiyo wako kwenye hatari ya kupata kifafa cha mimba mara wabebapo mimba.
4. Pengine kifafa cha mimba kinakuwepo kwenye familia fulani yaani kuna familia ambazo kila mtu akibeba mimba ni lazima apate kifafa cha mimba, kwa hiyo tunapaswa kufahamu familia zetu na kuchukua hatua mapema ipasavyo hasa kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya na kupata uangalizi wakati wa ujauzito.
5. Pia ugonjwa huu utegemea na sehemu husika kwa mfano waafrika wanapatwa sana na matatizo haya ukilinganisha na wazungu pamoja na wa hindi mpaka sasa sababu haijawahi kujulikana.
6. Huduma za afya kuwa duni sana, tunasema hivyo kwa sababu kuna wakati mwingine huduma mbaya kwa wanawake huwa chini kwa sababu unakuta wajawazito ni wengi na wahudumu ni wachache hali ambayo Usababisha wajawazito kutopata vipimo vya kutosha, kwa hiyo kama Mama ana tatizo hili ni vigumu kuligundua mapema hali ambayo Usababisha kukuta hali ishakuwa mbaya zaidi ukilinganisha na pale ingegundulika mapema.
7. Watu wenye vitambi.
Kuna utafiti uliobainika kuwa watu wenye vitambi wanapata sana Ugonjwa huu kuliko wale ambao hawana vitambi.kwa hiyo akina Mama wanaotegemea kupata watoto jitahidi kupunguza vitambi ili kuepuka tatizo hili.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 ai web app 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Umuhimu wa uzazi wa mpango kwa Mama
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi.
Soma Zaidi...Dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dalili za mimba kuanzia week mbili Hadi mwezi
Soma Zaidi...Faida na hasara za kutumia kondomu kama njia ya uzazi wa mpango
Kondomu ni mpira ambao uwekwa kwenye uke au uume kwa ajili ya kuzuia mimba wakati wa kujamiiana
Soma Zaidi...Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni
Soma Zaidi...dalili za mimba baada ya tendo la ndoa na changa ndani ya wiki moja
Utajifunza dalili za mwanzoni za mimba changa kuanzia wiki moja baada ya tendo la ndoa
Soma Zaidi...Dalili za uvimbe kwenye kizazi
Posti hii inahusu zaidi Dalili za uvimbe kwenye kizazi,hizi ni Dalili ambazo ujitokeza kwa akina mama ambao wana uvimbe kwenye kizazi kwa hiyo endapo mama ameona Dalili kama hizi anapaswa kuwahi hospitali mara moja kwa uangalizi zaidi.
Soma Zaidi...