Sababu za Ugonjwa wa kifafa cha mimba.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kifafa cha mimba, kwa kawaida mpaka sasa hakuna taarifa zozote kuhusu sababu za kuwepo kwa kifafa cha mimba ila kuna visababishi vinavyofikiliwa kama ni Dalili za kifafa cha mimba kama ifuatavyo
Sababu za kuwepo kwa kifafa cha mimba.
1. Kuwepo kwa shinikizo la damu lisilo la kawaida ambapo sio kwa sababu ya mimba ila ni kawaida ya mtu mwenye Ugonjwa huo, kwa hiyo wale wenye Tatizo la shinikizo la damu wanaweza kupata Ugonjwa huu ingawa si wote wenye shinikizo la damu kupatwa na Tatizo hili.
2.pia tatizo hili linawatokea Sana wale wanaobeba mimba za kwanza kuliko wale ambao wamebeba mimba mara nyingi, kwa hiyo wale wa mimba za kwanza wako hatarini kupata Ugonjwa huu.
3.Kwa wale wajawazito wanaopata shinikizo la damu na kiwango cha protini kuwepo kwenye mkojo wakati wa mimba ila wakijifungua tatizo hili linaisha kwa hiyo wako kwenye hatari ya kupata kifafa cha mimba mara wabebapo mimba.
4. Pengine kifafa cha mimba kinakuwepo kwenye familia fulani yaani kuna familia ambazo kila mtu akibeba mimba ni lazima apate kifafa cha mimba, kwa hiyo tunapaswa kufahamu familia zetu na kuchukua hatua mapema ipasavyo hasa kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya na kupata uangalizi wakati wa ujauzito.
5. Pia ugonjwa huu utegemea na sehemu husika kwa mfano waafrika wanapatwa sana na matatizo haya ukilinganisha na wazungu pamoja na wa hindi mpaka sasa sababu haijawahi kujulikana.
6. Huduma za afya kuwa duni sana, tunasema hivyo kwa sababu kuna wakati mwingine huduma mbaya kwa wanawake huwa chini kwa sababu unakuta wajawazito ni wengi na wahudumu ni wachache hali ambayo Usababisha wajawazito kutopata vipimo vya kutosha, kwa hiyo kama Mama ana tatizo hili ni vigumu kuligundua mapema hali ambayo Usababisha kukuta hali ishakuwa mbaya zaidi ukilinganisha na pale ingegundulika mapema.
7. Watu wenye vitambi.
Kuna utafiti uliobainika kuwa watu wenye vitambi wanapata sana Ugonjwa huu kuliko wale ambao hawana vitambi.kwa hiyo akina Mama wanaotegemea kupata watoto jitahidi kupunguza vitambi ili kuepuka tatizo hili.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Namna za kujilinda na fangasi ukeni
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuepuka fangasi za ukeni, ni njia ambazo usaidia kuepuka madhara ya fangasi za ukeni.
Soma Zaidi...Fahamu siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba.
Posti hii inahusu zaidi siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba , tunapaswa kujua hivi Ili kuweza kupanga uzazi na kuepuka njia ambazo ni hatarishi kwa afya zetu.
Soma Zaidi...Faida za uzazi wa mpango kwa watu wenye ugonjwa wa Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.
Soma Zaidi...DALILI ZA TEZI DUME
Tezi dume hii ni tezi inayopatikana katika katika mfumo wa uzazi wa mwanaume Ila hujulikana kama PROSTATE GLAND. pia hukua karibu na kibofu Cha mkojo na mirija ya mkojo hutumika kuzalisha majimaji (simen) yanayobeba mbegu hivyo bas mk
Soma Zaidi...Dalili Za hatari ambayo zinaweza kusababisha ugumba
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zilijitokeza zinaweza kusababisha ugumba hasa kwa wanawake, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwa makini kwa Dalili hizi hasa kwa wadada, kama kuna uwezekano wa matibabu tibu mapema ili kuepuka tatizo la kuwa mgumba.
Soma Zaidi...Dalili za uchungu
Uchungu wa uzazi hutokana na kubana nakuachia kwa misuli hii husababishwa kufunhuka kwa mlango wa tumbo la uzazi pamoja na shingo ya kizazi na kumuongezea mama uchungu wakati wa kujifungua(during labour) Pia kubana na kuachia huanza polepole wakati wa
Soma Zaidi...