picha

Sababu za Ugonjwa wa kifafa cha mimba.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kifafa cha mimba, kwa kawaida mpaka sasa hakuna taarifa zozote kuhusu sababu za kuwepo kwa kifafa cha mimba ila kuna visababishi vinavyofikiliwa kama ni Dalili za kifafa cha mimba kama ifuatavyo

Sababu za kuwepo kwa kifafa cha mimba.

 

1. Kuwepo kwa shinikizo la damu lisilo la kawaida ambapo sio kwa sababu ya mimba ila ni kawaida ya mtu mwenye Ugonjwa huo, kwa hiyo wale wenye Tatizo la shinikizo la damu wanaweza kupata Ugonjwa huu ingawa si wote wenye shinikizo la damu kupatwa na Tatizo hili.

 

2.pia tatizo hili linawatokea Sana wale wanaobeba mimba za kwanza kuliko wale ambao wamebeba mimba mara nyingi, kwa hiyo wale wa mimba za kwanza wako hatarini kupata Ugonjwa huu.

 

3.Kwa wale  wajawazito wanaopata shinikizo la damu na kiwango cha protini kuwepo kwenye mkojo wakati wa mimba ila wakijifungua tatizo hili linaisha kwa hiyo wako kwenye hatari ya kupata kifafa cha mimba mara wabebapo mimba.

 

4. Pengine kifafa cha mimba kinakuwepo kwenye familia fulani yaani kuna familia ambazo kila mtu akibeba mimba ni lazima apate kifafa cha mimba, kwa hiyo tunapaswa kufahamu familia zetu na kuchukua hatua mapema ipasavyo hasa kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya na kupata uangalizi wakati wa ujauzito.

 

5. Pia ugonjwa huu utegemea na sehemu husika kwa mfano waafrika wanapatwa sana na matatizo haya ukilinganisha na wazungu pamoja na wa hindi mpaka sasa sababu haijawahi kujulikana.

 

6. Huduma za afya kuwa duni sana, tunasema hivyo kwa sababu kuna wakati mwingine huduma mbaya kwa wanawake huwa chini kwa sababu unakuta wajawazito ni wengi na wahudumu ni wachache hali ambayo Usababisha wajawazito kutopata vipimo vya kutosha, kwa hiyo kama Mama ana tatizo hili ni vigumu kuligundua mapema hali ambayo Usababisha kukuta hali ishakuwa mbaya zaidi ukilinganisha na pale ingegundulika mapema.

 

7. Watu wenye vitambi.

Kuna utafiti uliobainika kuwa watu wenye vitambi wanapata sana Ugonjwa huu kuliko wale ambao hawana vitambi.kwa hiyo akina Mama wanaotegemea kupata watoto jitahidi kupunguza vitambi ili kuepuka tatizo hili.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2682

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 ai web app     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 web hosting     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID

Posti hii inahusu zaidi tiba ya awali kwa mwanamke mwenye changamoto ya PID, tunaita tiba ya awali kwa sababu baada ya kupima na kugunduliwa kwamba una tatizo au changamoto ya PID ni vizuri kutumia tiba hiii baadae ndipo utumie dawa.

Soma Zaidi...
Madhara ya tumbaku na sigara

Post hii itakwenda kuangalia madhara ya tumbaku na sigara anayoweza kuyapata mvutaji

Soma Zaidi...
Je tumbo huanza kukua baada ya mda gan?

Ni Swali kila mjamzito anataka kujiuliza hasa akiwa katika mimba ya kwanza. Wengine wanataka kujuwa ni muda gani anujuwe mavazi makubwa. Kama na wewe unataka kujuwa muda ambao tumbo huwa kubwa, endelea kusoma.

Soma Zaidi...
je mwana mke ana weza kubeba mimba kama hayupo kwenye siku zake za hatali ama

Mimba haipatikani kila siku, na pia mimba huingia kwa siku moja na katika muda mmoja. Baada ya mimba kutungwa hakuna tena nafasi ya kutungwa mimba nyingine.

Soma Zaidi...
Faida za kula yai lililopikwa kwa mama mjamzito

Yai lililopikwa ni chanzo kizuri cha protini, vitamini, na madini muhimu kwa mama mjamzito. Husaidia katika ukuaji wa mtoto tumboni, afya ya mama, na kuimarisha kinga ya mwili.

Soma Zaidi...
Namna ya kuongeza na mjamzito ili kupata taarifa zake na kutoa msaada

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kugundua tatizo lake na kutoa msaada pale penye uhitaji.

Soma Zaidi...