picha

Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Post hii inahusu zaidi Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, hali hii uwatokea sana wanawake zaidi ya wanaume, kwa kitaalamu hali hii ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo huitwa cystitis.

Sababu za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

1. Uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo usababishwa na bakteria ambao uingia na kushambulia sehemu za ndani za kibofu Cha mkojo, bakteria hao wanaweza kutoka sehemu mbalimbali kama vile kwenye mkojo wenyewe ikiwa mkojo umekaa kwa mda mrefu bila kutolewa nje hao bakteria wanaweza kushambulia sehemu za ndani ya kibofu Cha mkojo na hatimaye kuleta maambukizi kwenye kibofu Cha yanayoambatana na uvimbe.kwa hiyo ni lazima kukojoa tu baada ya kuhisi mkojo Ili kuepuka madhara ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

 

2. Kutumia sana ngono zembe yaani kujamiiana bila kutumia kondomu.

Hii ni mojawapo ya sababu ya kuwa na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu ya kuwepo kwa magonjwa ya ngono ambapo bakteria kutoka kwa mtu Mwenye maambukizi kwenda kwa mwingine ambaye Hana maambukizi na kusababisha kuwepo kwa bakteria ambao uingia kwenye kibofu Cha mkojo na kushambulia na kusababisha uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, hasa hasa kama bakteria hawa wasipotibiwa  mapema uweza kuleta madhara makubwa zaidi na kusababisha ugumba. Kwa hiyo tunapaswa kutumia kondomu wakati wa kujamiiana.

 

3. Kuaribika kwa sehemu za kuchuja mkojo.

Wakati mwingine Kuna kuharibika kwa sehemu mbalimbali zinazohusika na kuchuja mkojo, kama vile figo, nephroni na sehemu zote kwa hiyo hali hii usababisha bakteria kusababisha maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu mkojo hauwezi kutoka kwa wakati au pengine kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo, hali ambayo usababisha bakteria kuendelea kusababisha maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo. Kwa hiyo tunapaswa kuangalia mfumo wote wa kibofu Cha mkojo.

 

4. Kutumia catheter kwa mda mrefu au mara kwa mara.

Hii ni sababu mojawapo ambayo ufanya kuleta uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, kwa sababu catheter inaweza kuharibu kwenye milija wa mkojo na kusababisha bakteria kuingia na kuleta madhara makubwa ambayo yanasababisha kuleta uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo kwa hiyo inabidi catheter kuwepo kwa mda unaohitajika, mda isizidi Ili kuzuia maambukizi.kwa hiyo wataalamu wa afya wanapaswa kuhakikisha kuwa catheter unatolewa kwa mda.

 

5. Wanawake wanaotumia uzazi wa mpango.

Wanawake wengi wanaoweka mipira kwaenye uke illi kuzuia  mimba isitungwe usababisha bakteria kupita na kuingia kwenye sehemu ya kibofu Cha mkojo na kuleta madhara makubwa zaidi ambayo yanaweza kusababisha uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu mipira hiyo uacha uwazi ambao usababisha bakteria kuweza kupita na kuzaliana huko na kuleta uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3501

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Dalili za ugonjwa wa kipindupindu

Post hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa kipindupindu.Ni dalili zinzojitokeza kwa magonjwa wa kipindupindu.

Soma Zaidi...
Sababu za Kuvimba kwa kope.

Post hii inazungumzia kuhusiana na Sababu zinazopelekea kuvimba kwa kope, kawaida huhusisha sehemu ya kope ambapo kope hukua na kuathiri kope zote mbili. Pia hutokea wakati tezi ndogo za mafuta ziko karibu na msingi wa kope huziba. Hii inasababisha kuw

Soma Zaidi...
Mate yanaweza kuambukiza ukimwi

Jibu ni hapana, matehayawezi kuambukiza HIV. Lakini swali unalotakiwa kulijibu je ni kwa nini mate hayaambukizi. Makala hii itakwend akukupa majibu haya

Soma Zaidi...
Dalili za maambukizi kwenye uume

Post hii inahusu zaidi dalili za maambukizi kwenye uume, ni dalili ambazo ujitokeza pale maambukizi yanapotokea kwenye uume.

Soma Zaidi...
Sababu za Maumivu ya shingo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na maumivu ya shingo na ndani yake kunasababu zinazopelekea shingo kupata maumivu.

Soma Zaidi...
Dalili za Pua iliyovunjika

posti hii inahusu dalili za Pua iliyovunjika, pia inaitwa fracture ya pua, ni kuvunjika au kupasuka kwa mfupa katika pua yako

Soma Zaidi...