Sababu za wajawazito kupata Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinafanya wajawazito kupata ugonjwa wa Bawasili, kwa sababu tatizo hili linawapa wakina mama wajawazito, kwa hiyo tutaona kwa nini wajawazito wanapatwa na tatizo hili sana.
Sababu za kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwa wajawazito,
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba akina mama wajawazito upatwa na tatizo hili hii nikwa sababu ya kukua kwa mtoto kutoka hatua Moja kwenda nyingine na hivyo na uzito wa mtoto kuongezeka.
2. Kuwepo kwa mkandamizo au uzito kuzidi.
Kwamba tulivyotangulia kusema kwamba mwanamke Mjamzito uongezeka uzito na mgandamizo sehemu ya haja kubwa kwa sababu ya kuwepo kwa uzito wa mtoto na ukuaji wa mwili wa kizazi ( uterus) Hali hii upelekea mgandamizo sehemu ya haja kubwa na kusababisha mishipa ya damu midogo midogo kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa kupasuka hali inayosababisha kuota kwa vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa inayoambatana na miwasho.
3. Tatizo lingine ni ulaji wa udongo.
Tunafahamu kabisa wakati wa ujauzito akina Mama ula vitu vingi mbalimbali pamoja na udongo kwa sababu ya kukosa madini ya chuma kwa hiyo ulaji wa udongo usababisha wajawazito kupata choo kigumu hali ambayo usababisha wajawazito kutumia nguvu kubwa wakati wa kujisaidia hali inayosababisha Mishipa midogo midogo kwenye sehemu za haja kubwa kupasuka na hatimaye kuota uvimbe na vinyama kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
4. Unywaji mdogo wa maji wakati wa ujauzito.
Kwa kawaida wakati wa ujauzito akina Mama wanapaswa kunywa maji ya kutosha kwa sababu ya faida mbalimbali kwenye mwili.ila Kuna baadhi ya akina Mama wakati wa ujauzito wanabagua sana vyakula hata na maji wengine hawataki kabisa kutumia hali inayosababisha choo kuwa kigumu na katika harakati za kutoa choo unaweza kukuta mishipa ya haja kubwa kupasuka na kusababisha kuota uvimbe na vinyama kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
5. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kunywa maji ya kutosha pamoja na kutoa taarifa yoyote endapo wataona mabadiliko yoyote mwilini Ili kuepuka na balaa hili la bawasili na pia choo kikiwa kigumu no vizuri kabisa kutumia mboga mboga za majani na dawa Ili kurainisha choo hicho
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Dalili ninazoziona kwangu chuchu zinauma na sjapata period mwezi huu na nlishiriki tarehe 19 mwezi wa tisa
Nini humaanisha kama chuchu zinauma na hupati period mwanaidi mrefu.
Soma Zaidi...Madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu,ni madhara ambayo utokea kwa mtu anayetumia madawa ya kupunguza maumivu.
Soma Zaidi...dalili za mimba changa na siku ya kupata mimba
Jifunze namna ya kuthibitisha dalili za ujauzito kuwa ni za kweli. Tambuwa namna ya kupima mimba na muda mujarabu wa kupima
Soma Zaidi...Kazi na mdalasini katika kutibu matatizo ya homoni.
Posti hii inahusu zaidi kazi ya mdalasini katika matibabu ya homoni kwa wanawake.
Soma Zaidi...Imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba
Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...Maelekezo muhimu kwa Mama au mlezi wa mtoto mgonjwa
Posti hii inahusu zaidi maelekezo muhimu kwa mama au mlezi wa mtoto mgonjwa. Ni maelekezo muhimu hasa wakati wa kutoa dawa kwa mtoto.
Soma Zaidi...