Sababu za wajawazito kupata Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinafanya wajawazito kupata ugonjwa wa Bawasili, kwa sababu tatizo hili linawapa wakina mama wajawazito, kwa hiyo tutaona kwa nini wajawazito wanapatwa na tatizo hili sana.
Sababu za kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwa wajawazito,
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba akina mama wajawazito upatwa na tatizo hili hii nikwa sababu ya kukua kwa mtoto kutoka hatua Moja kwenda nyingine na hivyo na uzito wa mtoto kuongezeka.
2. Kuwepo kwa mkandamizo au uzito kuzidi.
Kwamba tulivyotangulia kusema kwamba mwanamke Mjamzito uongezeka uzito na mgandamizo sehemu ya haja kubwa kwa sababu ya kuwepo kwa uzito wa mtoto na ukuaji wa mwili wa kizazi ( uterus) Hali hii upelekea mgandamizo sehemu ya haja kubwa na kusababisha mishipa ya damu midogo midogo kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa kupasuka hali inayosababisha kuota kwa vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa inayoambatana na miwasho.
3. Tatizo lingine ni ulaji wa udongo.
Tunafahamu kabisa wakati wa ujauzito akina Mama ula vitu vingi mbalimbali pamoja na udongo kwa sababu ya kukosa madini ya chuma kwa hiyo ulaji wa udongo usababisha wajawazito kupata choo kigumu hali ambayo usababisha wajawazito kutumia nguvu kubwa wakati wa kujisaidia hali inayosababisha Mishipa midogo midogo kwenye sehemu za haja kubwa kupasuka na hatimaye kuota uvimbe na vinyama kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
4. Unywaji mdogo wa maji wakati wa ujauzito.
Kwa kawaida wakati wa ujauzito akina Mama wanapaswa kunywa maji ya kutosha kwa sababu ya faida mbalimbali kwenye mwili.ila Kuna baadhi ya akina Mama wakati wa ujauzito wanabagua sana vyakula hata na maji wengine hawataki kabisa kutumia hali inayosababisha choo kuwa kigumu na katika harakati za kutoa choo unaweza kukuta mishipa ya haja kubwa kupasuka na kusababisha kuota uvimbe na vinyama kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
5. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kunywa maji ya kutosha pamoja na kutoa taarifa yoyote endapo wataona mabadiliko yoyote mwilini Ili kuepuka na balaa hili la bawasili na pia choo kikiwa kigumu no vizuri kabisa kutumia mboga mboga za majani na dawa Ili kurainisha choo hicho
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Wanaopasawa kutumia PEP
PEP Ni dawa ambazo utumiwa na watu wanaojamiiana na watu wenye virus vya ukimwi ila wenyewe hawawezi kupata kwa sababu ya kutumia dawa hizo.
Soma Zaidi...Changamoto za ujauzito
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu changamoto za ujauzito na dalili zake endelevu
Soma Zaidi...DALILI ZA UJAUZITO KICHEFU CHEFU, KUTAPIKA, HEDHI, DAMU UKENI, KUJOJOAKOJOA N.K (mimba changa, mimba ya wiki moja, mimba ya mwezi mmoja )
DALILI KUU ZA MIMBA (UJAUZITO) Watu wengi sana wamekuwa wakilalamika kuwa mimba zao zinatoka, ama kupotea bila ya kujulikana tatizo wala bila ya kuugua.
Soma Zaidi...Njia za uzazi wa mpango kwa akina Mama kuanzia miezi sita baada ya kujifungua mpaka mwaka mmoja
Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango kwa mama aliyejifungua kuanzia miezi sita mpaka mwaka mmoja.
Soma Zaidi...Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni
Soma Zaidi...Jinsi ya kushusha homoni za kiume.
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza homoni za kiume kwa akina dada.
Soma Zaidi...