Sababu za wajawazito kupata Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinafanya wajawazito kupata ugonjwa wa Bawasili, kwa sababu tatizo hili linawapa wakina mama wajawazito, kwa hiyo tutaona kwa nini wajawazito wanapatwa na tatizo hili sana.
Sababu za kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwa wajawazito,
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu kwamba akina mama wajawazito upatwa na tatizo hili hii nikwa sababu ya kukua kwa mtoto kutoka hatua Moja kwenda nyingine na hivyo na uzito wa mtoto kuongezeka.
2. Kuwepo kwa mkandamizo au uzito kuzidi.
Kwamba tulivyotangulia kusema kwamba mwanamke Mjamzito uongezeka uzito na mgandamizo sehemu ya haja kubwa kwa sababu ya kuwepo kwa uzito wa mtoto na ukuaji wa mwili wa kizazi ( uterus) Hali hii upelekea mgandamizo sehemu ya haja kubwa na kusababisha mishipa ya damu midogo midogo kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa kupasuka hali inayosababisha kuota kwa vinyama au uvimbe kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa inayoambatana na miwasho.
3. Tatizo lingine ni ulaji wa udongo.
Tunafahamu kabisa wakati wa ujauzito akina Mama ula vitu vingi mbalimbali pamoja na udongo kwa sababu ya kukosa madini ya chuma kwa hiyo ulaji wa udongo usababisha wajawazito kupata choo kigumu hali ambayo usababisha wajawazito kutumia nguvu kubwa wakati wa kujisaidia hali inayosababisha Mishipa midogo midogo kwenye sehemu za haja kubwa kupasuka na hatimaye kuota uvimbe na vinyama kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
4. Unywaji mdogo wa maji wakati wa ujauzito.
Kwa kawaida wakati wa ujauzito akina Mama wanapaswa kunywa maji ya kutosha kwa sababu ya faida mbalimbali kwenye mwili.ila Kuna baadhi ya akina Mama wakati wa ujauzito wanabagua sana vyakula hata na maji wengine hawataki kabisa kutumia hali inayosababisha choo kuwa kigumu na katika harakati za kutoa choo unaweza kukuta mishipa ya haja kubwa kupasuka na kusababisha kuota uvimbe na vinyama kwenye sehemu mbalimbali za haja kubwa.
5. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kunywa maji ya kutosha pamoja na kutoa taarifa yoyote endapo wataona mabadiliko yoyote mwilini Ili kuepuka na balaa hili la bawasili na pia choo kikiwa kigumu no vizuri kabisa kutumia mboga mboga za majani na dawa Ili kurainisha choo hicho
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 ai web app 👉3 web hosting 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Dalili za mimba yenye uvimbe
Mimba ya tumbo - pia inajulikana kama hydatidiform mole - ni ugumu usiyo na kansa (benign) ambayo hutokea kwenye uterasi. Mimba ya molar huanza wakati yai linaporutubishwa, lakini badala ya mimba ya kawaida, yenye uwezo wa kutokea, plasenta hukua na kuwa
Soma Zaidi...Mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama ananyonyesha
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama anaenyonyesha
Soma Zaidi...Tatizo la kutokwa na utelezi wenye damu baada ya hedhi
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali za kutokwa na damu baada ya hedhi hili ni tatizo ambalo uwapata wanawake wengi pamoja na akina Mama kwa sababu ya kutokwa na damu yenye utelezi baada ya hedhi.
Soma Zaidi...siku za hatari
Hizi ni siku za hatari kupata ujauzito.Siku hizi ndio siku za kupata mimba kwa urahisi
Soma Zaidi...Zifahamu fibroids (uvimbe kwenye via vya uzazi)
Posti hii inahusu zaidi fibroids au uvimbe kwenye via vya uzazi hasa hasa utokea kwenye tumbo la uzazi ambapo kwa kitaalamu huitwa uterusi, uvimbe huu ulitokea watu wengine huwa hawawezi kutambua Dalili zake mapema kwa hiyo leo tunapaswa kujua Dalili zake
Soma Zaidi...Tatizo la muingiliano wa majimaji ya Amniotic au seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito.
posti hii inaelezea kuhusiana tatizo la muingiliano wa majimaji ya seli za Mtoto kwenye Damu ya mama mjamzito ambao hujulikana Kama Amniotic Fluid Embolism ni hali adimu lakini mbaya ambayo hutokea wakati Maji ya amniotiki Majimaji ambayo huzunguka mtot
Soma Zaidi...