SABABU ZINAZOPELEKEA KUJAA KWA MATE MDOMONI NA MATIBABU YAKE
Kutokwa na mate mengi mdomoni si ugojwa ni hali inayoweza kutokea kwa mtu yeyote. Mara nyingi hali hii haihitaji matibabu wa dawa, na huondoka yenyewe. Lakini hutokea baadhi ya nyakati ikawa mate yanatoka zaidi mdomoni. Je na wewe ni miongoni mwao? Makala
Hapa tutaangalia baadhi ya sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate. Sababu hizi zipo nyingine ni kwa wanawake tu, pia zipo ambazo ni kwa watu wa jinsia zote. Tunatarajia baada ya kusoma makala hii utaweza kuzijuwa sababu zinazopelekea mdomo kujaa mate, pia utaweza kupata kujuwa nini unatakiwa ufanye kulingana na tatizo lako.
HUJAA KWA MATE MDOMONI NI NINI HASA?
Kitaalamu kitendo hiki cha kujaa kwa mate mdomoni hufahamika kama hypersalivation. Hiki ni kitendo cha mdomo kujaa mate na wakati mwengine hutokea mate yakatoka yenyewe kwenye midomo baada ya kujaa. Kitaalamu kitendo hiki sio ugonjwa ila ni dalili ya kuwepo kwa tatizo lakiafya ama kuwepo kwa jambo lililopelekea mabadiliko ya mwili na kiafya.
JE MATE NI NINI?
Mate ni kimiminika cheupe kinachopatikana mdomoni ambacho hutengenezwa kwenye tezi za mate zinazojulikana kama salivary glands. Mate yana vichochezi (enzymes) ambavyo hutumika katika mmeng'enyo wa chakula hasa chakula cha wanga mdomoni. Mate pia husaidia katika kulainisha chakula na kuweka mgomo katika hali ya usafi, usalama na ubichibichi.
Tafiti zinaeleza kuwa mtu wa kawaida anaweza kuzalisha mate yanayofikia lita moja na nusu kwa siku. mate huzalishwa kwa wingi mtu anapokula na uzalishaji huu hupunguwa pale anapolala.
MADHARA YA KUWA NA MATE KIDOGO
Kwa kuwa mate yana faida kubwa mwilini hivyo endapo uzalishaji wa mate hautakuwa wa kutosheleza madhara huweza kumpata mtu ni kama:-
1.mdomo kuwa mkavu
2.Mmeng’enyo wa chakula kutofanyika vyema mdomoni kwa vyakula vya wanga
3.Mtu anaweza kupata taabu wakati wa kumeza
4.Anaweza kupata vidonda vya mdomo
5.Mdomo utaweza kuathiriwa kwa urahisi na fangasi, bakteria na sumu na kemikali za kwenye vyakula
6.Hata kuzungumza kunaweza kuathiriwa endapo mtu atakosa mate ya kutosha
MADHARA GANI ATAYAPATA MTU KAMA ATAKUWA NA MATE MENGI ZAIDI?
Kama ilivyokuwa kuna hasara kwa mate kukosekana mwilini, halikadhalika endapo mate yatakuwa mengi zaidi pia hali hii itakuwa na madhara yake. Madhara hayo ni kama:-
1.Matatizo wakati wa kusema, yaani hatoweza kuema vyema kama mate yatakuwa yamejaa mdomoni
2.Itakuwa vigumu kuufunga mdomo
3.Pia mdomo utaweza kupata mashambulizi ya bakteria kwa urahisi.
4.Mtu atashindwa kujiamini na kukaa na watu kwa sababu ya mate yake.
NINI HUSABABISHA MDOMO KUJAA MATE?
Hizi ni katika sababu ambazo hupelekea mate kujaa mdomoni:-
1.Kuongezeka kwa uzalishwaji wa mate mdomoni
2.Kama mtu atakuwa na shida na kushindwa kumeza mate ama mdomo kuondoa mate yote wakati wa kutema
3.Kama mtu atakuwa na matatizo ya kutoweza kuufunga mdomo
NINI HUSABABISHA ONGEZEKO LA UZALISHAJI WA MATE MDOMONI
Kama ulivyoona hapo juu sababu za kuwa na mate mengi mdomoni ni ongezeko la uzalishwaji wa mate mdomoni. Sasa swali la msingi kuwa “ni nini husababisha hili ongezeko la uzalishwaji wa mate mdomoni” . Sababu gizo ni kama:-
1.Kichefuchefu
2.Homa ya asubuhi na ujauzito
3.Kama kuna maabukizi na mashambulizi ya bakteria na virusi kwenye koo, tonsil na meneo mengine ya mdomoni
4.Kama umeng’atwa na buibui mwenye sumu, ama umekula uyoga ama umeng’atwa na wadudu
5.Kama unatumia meno ya bandia
6.Kama hufanyi usafi wa kinywa kwa umakini
7.Kama una maambukizi ya T.B ama ugonjwa wa rabies
8.Kama una kiungulia cha mara kwa mara
9.Mipasuko kwenye taya ma amifupa ya taya kutojipanga vyema
10.Vidonda vywnyw mfumo wa mmeng’enye wa chakula kama mdomoni, kooni na tumboni
NINI HUSABABISHA KUSHINDWA KUMEZA MATE AMA KUTEMA MATE YOTE?
Kama tulivyoona kuwa katika sababu zinazopelekea mate kujaa mdomoni ni kushindwa kuyameza yote, ama kuyatema yote. Sasa ni kitu gani husababisha hali hii?
1.Kuwa na shida ya kiafya kwenye mfumo wa fahamu
2.Kuwa na shida ya kiafyakwenye figo
SABABU NYINGINE ZINAZOPELEKEA MDOMO KUJAA MATE
1.Mpangilio mbaya wa meno
2.Majeraha kwenye mdomo
3.Hewa mbaya
4.Upungufu wa maji mwilini
5.Matatizo kwenye mfumo wa fahamu hasa katika kuhisi ladha ya chakula
6.Kama una maradhi ya pneumonia
NINI UFANYE KAMA UNA HILI TATIZO:
1.Kwa kupitia dalili zilizotajwa hapo juu, angalia ambayo huwenda ndio sababu kwako.
2.Kawaida tatizo hili halihitaji dawa, ila kama imezidi fika hospitali kwa uchunguzi zaidi.
3.Fika kituo cha afya kwa vipimo zaidi kama hali yako itaendelea kwa muda bila kurudi nyuma.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 web hosting 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
TIBA YA MINYOO AU DAWA YA MINYOO: praziquantel (biltricide) mebendazole (vermox, emverm) na albendazole (albenza).
TIBA YA MINYOO Moja katika sifa za minyoo ni kuwa wanatibika kwa urahisi pindi mgonjwa akipewa dawa husika.
Soma Zaidi...Sababu zinazoweza kumfanya figo kuharibika.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kufanya figo kuharibika.hili ni janga ambalo linawakumba Watu wengi siku hizi na kusababisha kupoteza maisha kwa wagonjwa wa figo hasa hasa kwa wale ambao hawana uwezo wa kulipia hela ya kusafishia figo.
Soma Zaidi...Maumivu wakati wa hedhi
Maumivu wakati wa hedhi, kitaalamu yakijulikana kama Dysmenorrhea, ni changamoto inayowaathiri mamilioni ya wanawake duniani kote. Wakati maumivu mepesi yakichukuliwa kama hali ya kawaida ya mabadiliko ya mwili, maumivu makali yanayomzuia mwanamke kufanya shughuli zake za kila siku yanaweza kuwa ishara ya matatizo makubwa ya kiafya. Makala haya yanajadili aina za maumivu haya, vyanzo vyake vikuu, njia za nyumbani na za kitabibu za kupata suluhisho, pamoja na ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu.
Soma Zaidi...Dalili za macho makavu.
Posti hii inahusu zaidi njia za kutambua Dalili za macho makavu, kama tulivyotangulia kuona kubwa macho kuwa makavu Usababishwa na sehemu ya kuzalisha maji kwenye jicho kushindwa kufanya kazi na jicho hilo huwa kavu na Dalili zake ni kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Upungufu wa damu (Anemia): Dalili na vyakula vya kuongeza damu.
Upungufu wa damu (Anemia) ni changamoto kubwa ya afya ya jamii duniani inayotokea pale mwili unapokosa seli nyekundu za damu au protini ya hemoglobin ya kutosha kusafirisha oksijeni. Makala haya ya kitaalamu yanachambua kwa kina dalili za kliniki za anemia, makundi yaliyo katika hatari kubwa, na namna ya kukabili tatizo hili kupitia lishe. Muundo maalum wa makala haya unalenga kutoa mwongozo wa vyakula vyenye madini ya chuma ya Heme na Non-Heme, nafasi ya Vitamini C katika ufyonzwaji wa virutubisho, na mbinu za kuzuia anemia kwa mujibu wa miongozo ya kisayansi ya Shirika la Afya Duniani (WHO).
Soma Zaidi...Saratani ya matiti (breasts cancer)
Post yetu inaenda kuzungumzia kuhusiana na Saratani ya Matiti ni Saratani ambayo hutokea katika seli za matiti. Baada ya Saratani ya Ngozi, Saratani ya matiti ndiyo Saratani inayojulikana zaidi hugunduliwa kwa wanawake Mara nyingi. Saratani yaÂ
Soma Zaidi...