Safari ya damu kwa Kila siku

Posti hii inakwenda kukuletea mfumo wa damu mwilini na safari zake za Kila siku

SAFARI YA DAMU KWA KILA SIKU.

 

picDamu ni tishu iliyopo katika hali ya kimiminika. Bila ya damu mwanadamu hawezi kuishi. Moyo ndio kiungo kikuu wenye mwili chenye kazi ya kuisambaza damu mwili mzima. Ukubwa wa kiungo hichi hufanana na ngumi. Moyo husafirisha damu kwenye mishipa inayokadiriwa kuwa na urefu wa kilomita elfu tisini na saba (97) na hii hufanyika ndani ya sekunde 20 tu.pic

 

Damu imeundwa kwa seli hai nyekundu za damu, seli hai nyeupe za damu, plasma, maji na seli sahani. Kila moja kati ya hizi ina kazi yake maalumu. Katika makala hii fupi tutaona vitu hivi kwa ufupi tu. Pia itambulike kuwa kuna viumbe hawana damu kama minyoo na baadhi ya samaki. Na hii ni kutokana na jinsi maumbile yao yalivyo. Asilimia 7% ya mwili wa binadamu ni damu na mtu mzima ana damu kuanzia lita 3.7 mapaka lita 5.6.

 

Seli nyekunsu za damu (red blood cell), hizi kitaalamu huitwa erythrocytes na hutengenezwa kwenye uroto wa mifupa yaani bone marrow. Kwa wastani seli hizi zinaweza kuishi kwa muda wa siku 120 tu baada ya kutengenezwa. Asilimia 40@ ya damu ni seli hizi na ndio ambazo zinaipa damu rangi nyekundu. Seli zina protini na haemoglobin (chembechembe nyekundu) na hizi ndio huipa rangi nyekundu. Kazi ya seli hizi ni kubeba heya ya oxygeni kutoka kwenye mapafu na kuipeleka kwenye moyo ili isambazwe zaidi mwilini. Ka kutoa hewa ya kabondaioksaidi kutoka kwenye moyo na kuipelekwa kwenye mapafu ili itolewe nje. Pia hubeba viinilishe (nutrients) kupeleka sehemu zingine za mwili.

 

Seli n yeupe za damu (white blood cell) kwa jina la kitaalamu huit wa leukocytes. Kazi kubwa ya seli hizi ni kupambana na maambukizi na wadudu wa baya wanaoshambulia mwili. Seli hizi zinaweza kuishi kuanzia siku moja mpaka mwezi mmoja tu baada ya kutengenezwa. Pia hutengenezwa kwenye uroto wa mifupa. Seli hizi zipo aina nyingi, kuna ambazo hupambana na kula bakteria na wadudu wengine wavamizi mwilini, kuna nyingine zinatoa antibodies kwa ajili ya kusaidia kupambana.

 

Seli sahani (platelets) kitaalamu huitwa thrombocytes pia hutengenezwa kwenye uroto wa mifupa. Sinaishi siku sita tu baada ya kutengenezwa. Kazi yao kubwa ni kugandisha damu pindi kunapokuwa na jeraha. Plasma sio seli ni maji ya njano ambayo husaidia damu huogelea vizuri kupita kwenye mirija ya damu. Asilimia 90 ya plasma ni maji, ila pia ina madimi, vitamin na viinilishe (nutrients)

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-09     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 914

Post zifazofanana:-

Dalili za upungufu wa maji mwilini.
Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji. Soma Zaidi...

Dalili za Dengue.
Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg Soma Zaidi...

Dalili za maumivu ya jino
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za maumivu ya jino Soma Zaidi...

Vyakula vya vitamini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za vyakula vya vitamini Soma Zaidi...

Dalili za maambukizi kwenye nephroni
Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye nephroni, uweza kutokea kwenye figo Moja au zote mbili. Soma Zaidi...

Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu
Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Faida za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe Soma Zaidi...

Dalili za kuziba kwa mirija ya uzazi
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea kwa sababu ya kuziba kwa mishipa ya uzazi, ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo la kuziba kwa mishipa ya uzazi. Soma Zaidi...

Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mapema, kwa sababu ya kuwepo kwa saratani ya matiti, kuna dalili ambazo zikijitokeza zinapaswa kutolewa taarifa mara moja bila kuchelewa kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Upungufu wa maji
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa maji mwilini Soma Zaidi...

Dawa za kutibu kiungulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za kutibu kiungulia Soma Zaidi...

Madhara ya minyoo
Posti hii inaonyesha kiufupi kabisa madhara ya minyoo kwenye mwili wa binadamu. Yafuatayo Ni madhara ya minyoo; Soma Zaidi...