Safari ya tano ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad
SAFARI YA TANO YA SINBAD
Baada ya watu kukusanyika siku ilofata sinbad akaanza kusimulia stori ya safari yake ya tano. Akaanza kusema kuwa “niliamua kutokuenda tena safari yoyote ya majini. Hali ilikuwa hivyo lakini baada ya miezi mingi nikapata wazo la kutengeneza jahazi langu ambalo litakuwa ni madhubutizaidi. Kwa mali nilizo nazo wakati huu nikaanza kuandaa jahazi kubwa na la kisasa lililo madhubuti sana. Muda ulitimia na jahazi kubwa na la kisasa zaidi lilikamilika.
Nikaanza kualika wafanyabiashara wakubwawakubwa na walio wazoefu zaidi. Tuliandaa bidhaa zetu na tukamtafuta nahodha aliye mahiri na safari hizi. Maandalizi yalipokamilika tukaanza safari usiku kwa kulingana na uwepo wa upepo. Kwa hakika safari ilikuwa njema, tuliweza kupita kwenye mikondo mikubwa na tukaingia visiwa kadhaa. Kwa hakika nahodha huyu alikuwa ni hodari na ni mzoefu, kwani hatukupita kisiwa ila alikuwa akitueleza habari zake. Hata visiwa visivyoishiwa na watu alikuwa akitueleza habari zake. Tulipita kenye kisiwa cha mawe yanayolia. Tukamueleza nahodha atuambie habari za mawe yale kaanza kutusimulia hadithi hii
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 ai web app 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 web hosting 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
SAFARI YA SABA YA SINBAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA SABA YA SINBAD Walipokusanyika siku ilofata Sinbad akawaambia kuwa kilichofanya nikavunja ahadi yangu ya kutosafiri tena ni kauli ya Sultani Nilipopunzika kwa muda wa miezi miwili nilipata habari kuwa Sultani
Soma Zaidi...Kitabu Cha hadithi ya wanawake watatu
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.
Soma Zaidi...Hadithi za Sinbad
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.
Soma Zaidi...HADITHI YA MZEE WA PILI NA MBWA
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MZEE WA PILI NA MBWA WAWILI WEUSI.
Soma Zaidi...TONGE LA MWISHO
Download kitabu Hiki Bofya hapa KWISHA KWA CHAKULA Watu waliaanza kumaliza vyakula vyao na wakaanza kufa baada ya siku kadhaa.
Soma Zaidi...