Saratul-humaza
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
- Suratul-Humaza (104): Imeteremshwa Makkah, Ina Aya Tisa.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
- Adhabu kali itamthubutikia kila mwenye kuramba kisogo, asengenyaye, msengenyaji.
- Ambaye amekusanya mali na kuihesabu (tu bila ya kuitumia katika njia za kheri).
- Anadhania kuwa mali yake itambakisha milele.
- Hasha! Bila shaka atavurumishwa katika (moto unaoitwa) Huttama.
- Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata ukajua) ni nini (huo moto unaoitwa) Huttama?
- (Huo ni) moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa (kwa ukali bara bara).
- Ambao unapanda (mpaka) nyoyoni.
- Hakika watafungiwa ndani ya moto huo.
- Kwa manguzo marefu (ili wasiweze kutoka).
Mafunzo kwa Ufupi.
- Kusengenya ni katika makosa makubwa kabisa.
- Ni makosa makubwa kukusanya mali bila kuitumia katika njia za kheri.
- Matumizi mabaya ya ulimi na neema zingine hupelekea kwenye maangamizi na adhabu.
- Matumizi mabaya ya ulimi kama fitna, uongo, usengenyi, n.k. huleta chuki, husda na mtafaruku katika jamii.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
👉1 web hosting 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Aina za Madd far-iy
Mada zipo katika makundi mawili ambayo ni madda far-iy na mdada twab-iy.
Soma Zaidi...Ni zipi hukumu za nuni yenye sakina au tanwin?
Hapa utajifunza usomaji wa Quran pindi utakapokuta nuni yenyebsakina au tanwin
Soma Zaidi...mgawanyiko katika quran
MGAWANYIKO KATIKA QURAN Juzuu, Sura, Aya, Manzil, Qara Wataalamu wa elimu za Qurani katika fani za uandishi na usomaji wameigawanya Qurani katika mafungu ili kuwezesha urahisi kwa wasomaji wa qurani.
Soma Zaidi...