Saratul-humaza
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
- Suratul-Humaza (104): Imeteremshwa Makkah, Ina Aya Tisa.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
- Adhabu kali itamthubutikia kila mwenye kuramba kisogo, asengenyaye, msengenyaji.
- Ambaye amekusanya mali na kuihesabu (tu bila ya kuitumia katika njia za kheri).
- Anadhania kuwa mali yake itambakisha milele.
- Hasha! Bila shaka atavurumishwa katika (moto unaoitwa) Huttama.
- Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata ukajua) ni nini (huo moto unaoitwa) Huttama?
- (Huo ni) moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa (kwa ukali bara bara).
- Ambao unapanda (mpaka) nyoyoni.
- Hakika watafungiwa ndani ya moto huo.
- Kwa manguzo marefu (ili wasiweze kutoka).
Mafunzo kwa Ufupi.
- Kusengenya ni katika makosa makubwa kabisa.
- Ni makosa makubwa kukusanya mali bila kuitumia katika njia za kheri.
- Matumizi mabaya ya ulimi na neema zingine hupelekea kwenye maangamizi na adhabu.
- Matumizi mabaya ya ulimi kama fitna, uongo, usengenyi, n.k. huleta chuki, husda na mtafaruku katika jamii.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 web hosting 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 ai web app
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 web hosting 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Sababu za kushuka surat al Mauun
Sura hii ni katika sura ambazo zinahitaji kusomwa kwa mazingatio sana. Wanaoswali bila ya kuzingatia swala zao, wameonywa vikali sana. Wanaowatesa na kuwanyanyasa mayatima wameonywa vikali. Wanaowanyima wenye haja na masikini huku wakiwakaripia nakuwasem
Soma Zaidi...Sababu za kushuka suratul al-quraysh na fadhila zake
SURAT AL-QURAYSH Sura hii ina majina mawili.
Soma Zaidi...Sababu za kushuka surat at Takaathur
Kuwa na tamaa huhitaji vitu vya watu si jambo jema. Ila kama tamaa hii itakuhamasisha na wewe kutafuta kitu hicho, kwa uwezo ambao Allah amekupa bila ha kuvuka mipaka yake, hili sio tatizo. Sura hii itakufundisha mengi
Soma Zaidi...