Saratul-humaza
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
- Suratul-Humaza (104): Imeteremshwa Makkah, Ina Aya Tisa.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
- Adhabu kali itamthubutikia kila mwenye kuramba kisogo, asengenyaye, msengenyaji.
- Ambaye amekusanya mali na kuihesabu (tu bila ya kuitumia katika njia za kheri).
- Anadhania kuwa mali yake itambakisha milele.
- Hasha! Bila shaka atavurumishwa katika (moto unaoitwa) Huttama.
- Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata ukajua) ni nini (huo moto unaoitwa) Huttama?
- (Huo ni) moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa (kwa ukali bara bara).
- Ambao unapanda (mpaka) nyoyoni.
- Hakika watafungiwa ndani ya moto huo.
- Kwa manguzo marefu (ili wasiweze kutoka).
Mafunzo kwa Ufupi.
- Kusengenya ni katika makosa makubwa kabisa.
- Ni makosa makubwa kukusanya mali bila kuitumia katika njia za kheri.
- Matumizi mabaya ya ulimi na neema zingine hupelekea kwenye maangamizi na adhabu.
- Matumizi mabaya ya ulimi kama fitna, uongo, usengenyi, n.k. huleta chuki, husda na mtafaruku katika jamii.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 web hosting 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Madrasa kiganjani
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 web hosting 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?
Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet
Soma Zaidi...Utofauti wa Quran na hadithi Al Quds
Has utakwenda kujifunza utofauti was Hadithi Al Quds na Quran
Soma Zaidi...quran na sayansi
QURANI KATIKA ZAMA ZA SAYANSI NA TEKNOLOJIAAsalaalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh.
Soma Zaidi...ASBAB-NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN
ASBAB NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN Quran imeteremka kwa muda wa miaka 23 kidogokido.
Soma Zaidi...