picha

Saratul-humaza

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Adhabu kali itamthubutikia kila mwenye kuramba kisogo, asengenyaye, msengenyaji.
  2. Ambaye amekusanya mali na kuihesabu (tu bila ya kuitumia katika njia za kheri).
  3. Anadhania kuwa mali yake itambakisha milele.
  4. Hasha! Bila shaka atavurumishwa katika (moto unaoitwa) Huttama.
  5. Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata ukajua) ni nini (huo moto unaoitwa) Huttama?
  6. (Huo ni) moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa (kwa ukali bara bara).
  7. Ambao unapanda (mpaka) nyoyoni.
  8. Hakika watafungiwa ndani ya moto huo.
  9. Kwa manguzo marefu (ili wasiweze kutoka).

 

Mafunzo kwa Ufupi.

  1. Kusengenya ni katika makosa makubwa kabisa.
  2. Ni makosa makubwa kukusanya mali bila kuitumia katika njia za kheri.
  3. Matumizi mabaya ya ulimi na neema zingine hupelekea kwenye maangamizi na adhabu.
  4.  Matumizi mabaya ya ulimi kama fitna, uongo, usengenyi, n.k. huleta chuki, husda na mtafaruku katika jamii.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF Views 2604

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

HIKUMU YA BASMALLAH YAANI KUSOMA BISMILLAH

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Hoja juu ya kukubalika hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa

Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya.

Soma Zaidi...
ASBAB-NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN

ASBAB NUZUL SABABU ZA KUSHUKA AYA NA SURA KWENYE QURAN Quran imeteremka kwa muda wa miaka 23 kidogokido.

Soma Zaidi...