picha

Saratul-humaza

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Adhabu kali itamthubutikia kila mwenye kuramba kisogo, asengenyaye, msengenyaji.
  2. Ambaye amekusanya mali na kuihesabu (tu bila ya kuitumia katika njia za kheri).
  3. Anadhania kuwa mali yake itambakisha milele.
  4. Hasha! Bila shaka atavurumishwa katika (moto unaoitwa) Huttama.
  5. Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata ukajua) ni nini (huo moto unaoitwa) Huttama?
  6. (Huo ni) moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa (kwa ukali bara bara).
  7. Ambao unapanda (mpaka) nyoyoni.
  8. Hakika watafungiwa ndani ya moto huo.
  9. Kwa manguzo marefu (ili wasiweze kutoka).

 

Mafunzo kwa Ufupi.

  1. Kusengenya ni katika makosa makubwa kabisa.
  2. Ni makosa makubwa kukusanya mali bila kuitumia katika njia za kheri.
  3. Matumizi mabaya ya ulimi na neema zingine hupelekea kwenye maangamizi na adhabu.
  4.  Matumizi mabaya ya ulimi kama fitna, uongo, usengenyi, n.k. huleta chuki, husda na mtafaruku katika jamii.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF Views 2212

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 ai web app     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

quran na tajwid

TAJWID Utangulizi wa elimu ya Tajwid YALIYOMO SURA YA 01 .

Soma Zaidi...
WAQFU WAL-IBTIDAAI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kshuka surat al Asr

Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo…

Soma Zaidi...