Saratul-humaza
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
- Suratul-Humaza (104): Imeteremshwa Makkah, Ina Aya Tisa.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
- Adhabu kali itamthubutikia kila mwenye kuramba kisogo, asengenyaye, msengenyaji.
- Ambaye amekusanya mali na kuihesabu (tu bila ya kuitumia katika njia za kheri).
- Anadhania kuwa mali yake itambakisha milele.
- Hasha! Bila shaka atavurumishwa katika (moto unaoitwa) Huttama.
- Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata ukajua) ni nini (huo moto unaoitwa) Huttama?
- (Huo ni) moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa (kwa ukali bara bara).
- Ambao unapanda (mpaka) nyoyoni.
- Hakika watafungiwa ndani ya moto huo.
- Kwa manguzo marefu (ili wasiweze kutoka).
Mafunzo kwa Ufupi.
- Kusengenya ni katika makosa makubwa kabisa.
- Ni makosa makubwa kukusanya mali bila kuitumia katika njia za kheri.
- Matumizi mabaya ya ulimi na neema zingine hupelekea kwenye maangamizi na adhabu.
- Matumizi mabaya ya ulimi kama fitna, uongo, usengenyi, n.k. huleta chuki, husda na mtafaruku katika jamii.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
π1 Kitau cha Fiqh π2 Kitabu cha Afya π3 Madrasa kiganjani π4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π5 kitabu cha Simulizi π6 Bongolite - Game zone - Play free game
π1 Kitau cha Fiqh π2 Kitabu cha Afya π3 Madrasa kiganjani π4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π5 kitabu cha Simulizi π6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA (MIIM SAKINA)
HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA : Mym sakina ni miym ambayo haina iβrab ( Ω Ω).
Soma Zaidi...HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa
Soma Zaidi...Ni nini maana ya Idh-har katika usomaji wa Quran
Hapa utajifunza kuhusu hukumu ya Idh-har katika usomaji wa Quran.
Soma Zaidi...Makundi ya Id-ghamu katika usomaji wa Quran Tajwid
Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu.
Soma Zaidi...Sababu za kushuka Surat al fatiha (Alhamdu)
Kwa kuwa hakuna sababu mwalumu ikiyonukuliwa kuwa ndio chanzo cha kushushwa suravhii. Basi post hii itakujuza mambo ambayo huwenda hukuyajuwa kuhusu fadhika za surabhii na mengineyo.
Soma Zaidi...