picha

Saratul-humaza

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Adhabu kali itamthubutikia kila mwenye kuramba kisogo, asengenyaye, msengenyaji.
  2. Ambaye amekusanya mali na kuihesabu (tu bila ya kuitumia katika njia za kheri).
  3. Anadhania kuwa mali yake itambakisha milele.
  4. Hasha! Bila shaka atavurumishwa katika (moto unaoitwa) Huttama.
  5. Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata ukajua) ni nini (huo moto unaoitwa) Huttama?
  6. (Huo ni) moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa (kwa ukali bara bara).
  7. Ambao unapanda (mpaka) nyoyoni.
  8. Hakika watafungiwa ndani ya moto huo.
  9. Kwa manguzo marefu (ili wasiweze kutoka).

 

Mafunzo kwa Ufupi.

  1. Kusengenya ni katika makosa makubwa kabisa.
  2. Ni makosa makubwa kukusanya mali bila kuitumia katika njia za kheri.
  3. Matumizi mabaya ya ulimi na neema zingine hupelekea kwenye maangamizi na adhabu.
  4.  Matumizi mabaya ya ulimi kama fitna, uongo, usengenyi, n.k. huleta chuki, husda na mtafaruku katika jamii.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF Views 2483

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

surat al mauun

SURATUL-MAM’UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat..

Soma Zaidi...
quran na sayansi

2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio.

Soma Zaidi...
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...
Fadhila za kusoma surat al Baqarah

Surat al Baqarah ni katika sura ambazo tunapaswa tuwe tunasoma mara kwa mara. Post hii itakufundisha kuhusu fadhila za sura hii.

Soma Zaidi...