image

Sifa au vigezo vya dini sahihi

Dini sahihi anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

  1. DINI SAHIHI ANAYOSTAHIKI KUFUATA MWANAADAMU.

Kulingana na umbile lake, mwanaadamu daima hutamani kuishi kwa furaha na amani ili kufikia lengo la kuumbwa, na hapo ndipo inambidi kuchagua dini (njia sahihi ya maisha) kati ya Uislamu, Ukafiri, Ushirikina au Utawa itakayomtimizia malengo yake. 

 

  1.  Sifa au Vigezo Vya dini sahihi

Dini sahihi ni ile inayomuwezesha mwanaadamu kuishi kwa furaha na amani ya kweli hapa Duniani na Akhera, na ni lazima iwe na sifa zifuatazo;

 

  1. Dini sahihi lazima ieleze ukweli juu ya maumbile;

Ni lazima ieleze ukweli juu ya mwanaadamu, lengo la kuumbwa kwake, hadhi/nafasi yake, dhima/kazi yake na maumbile yanayomzunguka na viumbe vyote vilivyo hai na visivyo hai, na hatima ya kila kitu.

 

  1. Dini sahihi ni lazima iwe na kanuni na sheria zinazoendana na maumbile yote;

Kanuni na sheria za dini sahihi ni lazima ziwe sambamba na kanuni za kimaumbile ili kuepusha mgongano wowote wa kimahitajio wa kimwili na kimazingira pia.

 

  1. Ni lazima itosheleze mahitajio ya mwanaadamu ya kimwili na kiroho;

Pia ni wajibu kwa dini sahihi kuelekeza na kutosheleza hisia za mwanaadamu pindi anapokuwa na hali ya furaha au hali ya majonzi, namna ya kukabiliana nazo ili kubakia katika lengo lake la kuumbwa (maisha).

 

  1. Dini sahihi pia lazima iwe ni mfumo wa maisha uliokamilika;

Dini sahihi haina budi kuwa na utaratibu kamili wa kila kipengele na Nyanja ya maisha ya kila siku kiuchumi, kisiasa, kiafya, kiutamaduni, kisheria, kielimu, n.k.

 

  1. Pia dini sahihi ni lazima iwe na ibada maalum zinazombakisha mwanaadamu katika maadili na hadhi yake;

Ni wajibu kwa dini sahihi kuwa na muongozo wa kumuinua na kumbakisha mwanaadamu katika mwenendo mzuri wa kiroho (kiutu) unaoweza kuustawisha mwili na kuleta mahusiano mazuri ya kiutu yasiyo na chuki, husuda, tamaa, kiburi, vurugu, n.k.

 

  1. Dini sahihi haina budi kuwa ya walimwengu wote na ya nyakati zote;

Ili kufikia lengo la kuumbwa mwanaadamu, dini sahihi ni lazima iwe inawahusu watu wa aina zote (wote), isiwe na jina la mtu au mahali na isiwe na mipaka ya kijiografia, rangi za watu, mahali, nyakati, n.k.

 

  1. Dini sahihi ni lazima iainishe na kusimamia haki zote za mwanaadamu;

Ni wajibu kwa dini sahihi kutoa na kusimamia haki, hukumu na adhabu kwa usawa na uadilifu kwa watu wote kibinafsi na kijamii bila upendeleo na ubaguzi wowote wa kirangi, taifa, nasaba, cheo au hadhi.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 2093


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

tarekh 06
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...

Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...

Historia ya maimam Wanne wa fiqh
Soma Zaidi...

Kuandaliwa Mtume (s.a.w) Kulingania Uislamu katika mji wa Makkah
7. Soma Zaidi...

Chanzo cha vita vya Siffin na matokeo yake: Vita vya Ally na Muawia
Soma Zaidi...

TAREKH, HISTORIA NA SIRA YA UISLAMU NA MTUME MUHAMMAD KUTOKA KUZALIWA MPAKA KUFARIKI NA HARAKATI ZAKE
1. Soma Zaidi...

NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU
Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hatua mbili kuu za kushuka kwa Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kifo cha Khalia Uthman kilivyotokea
Soma Zaidi...

Mtume kumuoa bi khadija
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 15. Hapa utajifunza kuhusu chimbuko la ndoa ya Mtume s.a.w na bi Khadija. Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KULELEWA NA BABA YAKE MDOGO MTUME (ABU TALIB)
KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake. Soma Zaidi...