Sifa nyingine za kuchaguwa mchumba ambazo watu wengi hawazijui

Hizi ni sifa za ziada za mchumba katika uislamu. Sifa hizi wengi hawazijui ama hawazingatii.

Kizazi, Rika na Elimu

Sifa nyingine za kuzingatia wakati wa kuchagua mchumba ni kizazi na rika. Kuhusu kizazi Mtume (s.a.w) anatunasihi:
"Oeni wale wanawake wenye upendo na huruma, wenye kizazi na hakika watakuwa ni wenye manufaa katika kuongeza idadi yenu miongoni mwa matafa." (Abu Daud, Nasai)

 


Kwa vijana ambao ndio mara yao ya kwanza kuingia katika maisha ya ndoa, pamoja na kuzingatia sifa za msingi zilizoelezwa, ni vema wakachaguana vijana kwa vijana kama alivyoshauri Mtume (s.a.w) katika hadithi ifuatayo:

 


Jabir (r.a) ameeleza: "Tulikuwa na Mtume (s.a.w) katika vita. Tulipokaribia Madina wakati wa kurejea nilisema: "Ee Mtume wa Mwenyezi Mungu, hakika nimeoa hivi karibuni." Akauliza, "Umeoa"? Nikajibu, "Ndio" Akauliza: "Bikra au mjane?" Nikajibu "Mjane" Akasema, "Kwa nini asiwe bikra ili uweze kucheza naye, naye aweze kucheza nawe..." (Bukhari na Muslimu)

 


Jambo lingine Ia kuzingatia wakati wa kuchagua uchumba ni Elimu. Kama mume na mke watakuwa na Elimu sahihi juu ya Uislamu na taaluma nyingine za mazingira yao watakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuwalea watoto wao kimaadili na kitaaluma. Katika kusisitiza hili tuzingatie mchango wa bibi Khadija (r.a) alioutoa katika kuupeleka mbele Uislamu kutokana na utajiri wake na mchango wa bibi 'Aisha (r.a) alioutoa katika kuufundisha Uislamu kutokana na Elimu yake ya Uislamu.

 

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/08/16/Tuesday - 11:30:42 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 714

Post zifazofanana:-

Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu
Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha Soma Zaidi...

Taratibu za mahari katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu. Soma Zaidi...

Nini maana ya ndoa katia uislamu na ni upi umuhimu wake
Hapa utajifunza maana ya ndoa kulingana na uislamu na umuhimu wake katika jamiii Soma Zaidi...

Taratibu za kumuona mchumba katika uislamu
Hspa utajifunza taratibu za kuonana na mchumba katika uislamu. Soma Zaidi...

Faida na umuhimu wa nfoa katika jamii
Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi Soma Zaidi...

Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja
Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii
Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake? Soma Zaidi...

Sifa nyingine za kuchaguwa mchumba ambazo watu wengi hawazijui
Hizi ni sifa za ziada za mchumba katika uislamu. Sifa hizi wengi hawazijui ama hawazingatii. Soma Zaidi...

Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako. Soma Zaidi...

Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja. Soma Zaidi...

Kugungisha ndoa ya kiislamu hatuwa kwa hatuwa
Hapa utajifunza jinsi ya kuozesha hatuwa kwa hatuwa. Pia utajifunza masharti ya kuoa na masharti ya kuolewa. Soma Zaidi...

Taratibu za kuchaguwa mchumba katika uislamu
Hapa utajifunza hatuwa kwa hatuwa za kuchaguwa mchumba kulingana na sheria za kiislamu. Soma Zaidi...