Maradhi ya macho, dalili zake na matibabu yake
Makala hii itakufundisha maradho makuu ya macho, matibabu yake na tiba zake
MARADHI YA MACHO
Matatizo ya macho yapo mengi katika jamii, lakini mara nyingi matatizo ya macho yanatibika iwapo mgonjwa ataonana na daktari mara atakapoona dalili. Miongoni mwa matatizo ya macho ni kupoteza uwezo wa kuona.
1.Kutoona karibu (long sightedness)
Tatizo hili mara nyingi huwatokea watu wenye umri wa miaka 40 na kuendelea.
Dalili
A.Katika mazingira ya kawaida anaona sawa sawa
B.Kushindwa kusoma herufi ndogo ndogo
C.Kushindwa kufanya kazi za sehemu ndogo ndogo mfano kutunga sindano.
Matibabu: Kutumia miwani ya kusomea.
2.Kutoona Mbali (short sightedness)
A.Hayana umri maalum
B.Myopia – haoni mbali vizuri
C.Hyperopia – haoni mbali na kichwa kinauma akikosa kuvaa miwani yenye namba ndogo kusaidia lense.
NB: Mgonjwa anasoma karibu bila miwani
Matibabu: Kutumia miwani ya kuonea mbali
3.Mtoto wa Jicho (cataract)
Dalili
A.Kidoto cheupe katikati ya kioo cheusi cha jicho (kinafunika mboni ya jicho)
B.Kidoto cheupe kisichobadilika kwa mwangaza
C.Kupunguza nuru ya macho
NB - Mtu anaweza kuzaliwa nacho au kupata ukubwani, inaweza kuwa kwenye jicho moja au yote. Mgonjwa huona mchanganyiko wa rangi anapoangalia mwangaza kama taa za umeme au gari.
Matibabu
Mtoto wa Jicho huwa anatibika kwa upasuaji mdogo na kumuwezesha mgonjwa kuona tena.
4.Presha ya macho (glaucoma)
Tatizo hili husababishwa na kuongezeka presha ya jicho (intraocular pressure) kutokana na kukosekana uwiano wa mzunguko wa majimaji ndani ya jicho (aqueous fluid) kinachotoka kidogo kuliko kinachoingia.
Matokeo
Glaucoma hukandamiza na kuuharibu mshipa wa fahamu ya jicho na kusababisha kupungua kwa nuru na baadae kupoteza nuru ya macho.
Matibabu: Kuonana na daktari kwa ushauri na dawa
5.Macho tongo
Hutokea ama kwa mtu mmoja mmoja, makundi au kwa msimu.
Sababu:
Vimelea ambavyo huzaliwa kwenye sehemu za uchafu Wakati wa msimu huambukiza kwa kukosa elimu ya afya, kwa mfano kutokuosha mikono baada ya kuamkiana na mgonjwa mwenye maradhi haya au kutumia vifaa vya macho kwa zaidi ya mtu mmoja kama vile miwani.
Dalili
A.Kuhisi kama kuna mchanga ndani ya jicho
B.Kuvimba mifuniko ya macho bila kupoteza nuru.
C.Macho kuwa mekundu sana (conjuctivitis)
D.Kutoka tongo kila mara
Matibabu
Mgonjwa atumie dawa alizoandikiwa na daktari tu, kwani dawa za matone za macho ni nyingi na zina kazi tofauti.
6.Matatizo ya sehemu nyeusi ya jicho (cornea)
Kuna matatizo manne makubwa
1. Kovu - kidoto/kibaka cheupe
2. Kidonda - kidoto kijivujivu
3. Kuingiwa na kitu - kemikali,mdudu, vumbi n.k
4. Kutoboka na kutoa maji.
Indhari: hali ya pili mpaka ya nne zikitokea mgonjwa akimbizwe
hospital wakati jicho limefunikwa baada ya huduma ya kwanza
Dalili
KOVU
1.Haina maumivu
2.Jicho haliwi jekundu
3.Jicho halivimbi
4.kupungua nuru jicho
KIDONDA
A.Kinayo maumivu
B.Jicho lililoathirika huwa
C.jekundu
D.Jicho kupunguka nuru
E.Kuuma jicho kwenye
F.mwangaza
G.Kutoka machozi
H.Jicho kuvimba
Kidonda kinaweza kusababishwa na bakteria, fangas, ukosefu wa vitamin A au kwa kuumia mfano; kujichoma na kitu chenye ncha au kitu kigumu, kuingiwa na kitu jichoni, kuungua au kuingia kemikali jichon.
Indhari: Iwapo jicho litaumia lifunike jicho lisipate mwangaza kisha mpeleke mgonjwa hospitali.
7. Kemikali na kuungua
Kama mgonjwa ameingia kemikali kama vile acid, alkali, saruji, chokaa mtie maji ya mchuruziko kwa takriban dakika 15 mfululizo na baadae mpeleke hospitali
8.Macho kuwasha na kutokwa na machozi (conjuctivitis)
Huwakumba zaidi watoto wa umri kati ya miaka 5 -15 ambao hupendelea kucheza sehemu za vumbi au kwenye muangaza mkali (pwani yenye mchanga mweupe sana)
Watu wazima wenye kufanya kazi kwenye viwanda vinavozalisha vumbi, na wenye pumu ya muda mrefu.
Dalili
A.Macho kuwasha (Nuru ya macho haipungui)
B.Macho kubadilika rangi (kahawia)
C.Kutokwa na machozi mengi (sana)
D.Kushindwa kuangalia kwenye muangaza mkali
Matibabu
Kusafisha macho mara kwa mara kwa maji safi.
Kutumia dawa kwa maelekezo ya daktari
9.Kinundu katika mfuniko wa juu au chini wa jicho
DALILI
A.Kinundu kisichouma
B.Mara nyingi hupona wenyewe au unaweza kukikanda kwa maji ya uvuguvugu.
C.Kisipopona au kitakapokuwa kikubwa huhitaji upasuaji mdogo.
10.Uvimbe katika mfuniko wa jicho (cellulitis)
A.uvimbe kwenye mifuniko ya jicho
B.inaweza kuzuwia jicho kucheza (kutembea tembea)
C.mara nyingi hutokea baada ya kusambaa kwa maambukizo
D.ya socket ya jicho kutoka pembezoni kwa saines (sinusitis) za pua
E.husababisha kupoteza nuru za macho
Matibabu: Mpeleke mgonjwa kwa daktari wa masikio, pua na koo (ENT).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 ai web app 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Matatizo ya kisaikolojia kwa watoto (mfano, ADHD): Dalili zake.
Afya ya akili ya watoto ni msingi wa maendeleo yao ya baadaye. Katika ulimwengu wa sasa, matatizo ya kisaikolojia kama ADHD (Upungufu wa Umakini na Usikivu) yanazidi kuongezeka, lakini mara nyingi huchanganyikiwa na utovu wa nidhamu. Makala haya yanalenga kutoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu dalili za matatizo ya kisaikolojia kwa watoto, yakigusia kwa kina hali ya ADHD na jinsi wazazi wanavyoweza kutofautisha kati ya tabia za kawaida za utotoni na changamoto zinazohitaji msaada wa kisaikolojia.
Soma Zaidi...Kupambana na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na kisukari
Soma Zaidi...Dalili za UKIMWI na VVU kutoka mwanzoni mwa siku za mwanzo
Je na wewe ni katika wanaosumbuka sana kujuwa dalili za kwanza za ukimwi toka siku ya kwanza, ama dalili za ukimwi kwenye ulimi, ama unatakakujuwa ni muda gani ukimwi huonekana, na je ukishiriki ngono zembe ndio utapata ukimwi? Basi makala hii ni kwa ajil
Soma Zaidi...Ugonjwa wa ngozi (Eczema): Sababu na jinsi ya kutunza ngozi.
Muhtasari Eczema, inayofahamika kitaalamu kama atopic dermatitis, ni hali ya ngozi kuwa kavu, kuwasha, na kupata vipele vinavyoweza kujitokeza mara kwa mara. Makala haya yameandaliwa kwa kina kuchunguza visababishi vya eczema, vichochezi vyake, na kutoa mwongozo wa kitaalamu wa jinsi ya kutunza ngozi ili kudhibiti hali hii na kuboresha maisha ya kila siku.
Soma Zaidi...Dalili za Mimba ya Siku 7 kwa Mwanamke
Makala haya yanachunguza ukweli wa kifizikia kuhusu dalili za mimba katika hatua za awali kabisa (wiki ya kwanza baada ya utungisho). Tutafafanua nini kinatokea ndani ya mwili wa mwanamke ndani ya siku 7 na dalili zinazoweza kujitokeza, pamoja na kusisitiza umuhimu wa subira katika kufanya
Soma Zaidi...Je, UKIMWI Unaweza Kukaa Bila Dalili?
Jibu fupi ni ndiyo. VVU (Virusi vya Upungufu wa Kingamwili) vinaweza kuwepo mwilini kwa miaka mingi bila kuonyesha dalili zozote dhahiri za ugonjwa. Hali hii ya kutokuwa na dalili ndiyo inayochangia kwa kiasi kikubwa kusambaa kwa virusi hivi, kwani mtu anaweza kuwa anaambukiza wengine bila yeye mwenyewe au wengine kujua.
Soma Zaidi...