Maradhi ya macho, dalili zake na matibabu yake

Makala hii itakufundisha maradho makuu ya macho, matibabu yake na tiba zake

Maradhi ya macho, dalili zake na matibabu yake

MARADHI YA MACHO



Matatizo ya macho yapo mengi katika jamii, lakini mara nyingi matatizo ya macho yanatibika iwapo mgonjwa ataonana na daktari mara atakapoona dalili. Miongoni mwa matatizo ya macho ni kupoteza uwezo wa kuona.



1.Kutoona karibu (long sightedness)
Tatizo hili mara nyingi huwatokea watu wenye umri wa miaka 40 na kuendelea.



Dalili
A.Katika mazingira ya kawaida anaona sawa sawa
B.Kushindwa kusoma herufi ndogo ndogo
C.Kushindwa kufanya kazi za sehemu ndogo ndogo mfano kutunga sindano.



Matibabu: Kutumia miwani ya kusomea.



2.Kutoona Mbali (short sightedness)
A.Hayana umri maalum
B.Myopia – haoni mbali vizuri
C.Hyperopia – haoni mbali na kichwa kinauma akikosa kuvaa miwani yenye namba ndogo kusaidia lense.



NB: Mgonjwa anasoma karibu bila miwani
Matibabu: Kutumia miwani ya kuonea mbali



3.Mtoto wa Jicho (cataract)
Dalili
A.Kidoto cheupe katikati ya kioo cheusi cha jicho (kinafunika mboni ya jicho)
B.Kidoto cheupe kisichobadilika kwa mwangaza
C.Kupunguza nuru ya macho



NB - Mtu anaweza kuzaliwa nacho au kupata ukubwani, inaweza kuwa kwenye jicho moja au yote. Mgonjwa huona mchanganyiko wa rangi anapoangalia mwangaza kama taa za umeme au gari.



Matibabu
Mtoto wa Jicho huwa anatibika kwa upasuaji mdogo na kumuwezesha mgonjwa kuona tena.



4.Presha ya macho (glaucoma)
Tatizo hili husababishwa na kuongezeka presha ya jicho (intraocular pressure) kutokana na kukosekana uwiano wa mzunguko wa majimaji ndani ya jicho (aqueous fluid) kinachotoka kidogo kuliko kinachoingia.



Matokeo
Glaucoma hukandamiza na kuuharibu mshipa wa fahamu ya jicho na kusababisha kupungua kwa nuru na baadae kupoteza nuru ya macho.



Matibabu: Kuonana na daktari kwa ushauri na dawa




5.Macho tongo
Hutokea ama kwa mtu mmoja mmoja, makundi au kwa msimu.



Sababu:
Vimelea ambavyo huzaliwa kwenye sehemu za uchafu Wakati wa msimu huambukiza kwa kukosa elimu ya afya, kwa mfano kutokuosha mikono baada ya kuamkiana na mgonjwa mwenye maradhi haya au kutumia vifaa vya macho kwa zaidi ya mtu mmoja kama vile miwani.



Dalili
A.Kuhisi kama kuna mchanga ndani ya jicho
B.Kuvimba mifuniko ya macho bila kupoteza nuru.
C.Macho kuwa mekundu sana (conjuctivitis)
D.Kutoka tongo kila mara



Matibabu
Mgonjwa atumie dawa alizoandikiwa na daktari tu, kwani dawa za matone za macho ni nyingi na zina kazi tofauti.



6.Matatizo ya sehemu nyeusi ya jicho (cornea)
Kuna matatizo manne makubwa
1. Kovu - kidoto/kibaka cheupe
2. Kidonda - kidoto kijivujivu
3. Kuingiwa na kitu - kemikali,mdudu, vumbi n.k
4. Kutoboka na kutoa maji.
Indhari: hali ya pili mpaka ya nne zikitokea mgonjwa akimbizwe
hospital wakati jicho limefunikwa baada ya huduma ya kwanza



Dalili
KOVU
1.Haina maumivu
2.Jicho haliwi jekundu
3.Jicho halivimbi
4.kupungua nuru jicho



KIDONDA
A.Kinayo maumivu
B.Jicho lililoathirika huwa
C.jekundu
D.Jicho kupunguka nuru
E.Kuuma jicho kwenye
F.mwangaza
G.Kutoka machozi
H.Jicho kuvimba



Kidonda kinaweza kusababishwa na bakteria, fangas, ukosefu wa vitamin A au kwa kuumia mfano; kujichoma na kitu chenye ncha au kitu kigumu, kuingiwa na kitu jichoni, kuungua au kuingia kemikali jichon.



Indhari: Iwapo jicho litaumia lifunike jicho lisipate mwangaza kisha mpeleke mgonjwa hospitali.



7. Kemikali na kuungua
Kama mgonjwa ameingia kemikali kama vile acid, alkali, saruji, chokaa mtie maji ya mchuruziko kwa takriban dakika 15 mfululizo na baadae mpeleke hospitali




8.Macho kuwasha na kutokwa na machozi (conjuctivitis)
Huwakumba zaidi watoto wa umri kati ya miaka 5 -15 ambao hupendelea kucheza sehemu za vumbi au kwenye muangaza mkali (pwani yenye mchanga mweupe sana)



Watu wazima wenye kufanya kazi kwenye viwanda vinavozalisha vumbi, na wenye pumu ya muda mrefu.



Dalili
A.Macho kuwasha (Nuru ya macho haipungui)
B.Macho kubadilika rangi (kahawia)
C.Kutokwa na machozi mengi (sana)
D.Kushindwa kuangalia kwenye muangaza mkali



Matibabu
Kusafisha macho mara kwa mara kwa maji safi.
Kutumia dawa kwa maelekezo ya daktari



9.Kinundu katika mfuniko wa juu au chini wa jicho



DALILI
A.Kinundu kisichouma
B.Mara nyingi hupona wenyewe au unaweza kukikanda kwa maji ya uvuguvugu.
C.Kisipopona au kitakapokuwa kikubwa huhitaji upasuaji mdogo.



10.Uvimbe katika mfuniko wa jicho (cellulitis)



A.uvimbe kwenye mifuniko ya jicho
B.inaweza kuzuwia jicho kucheza (kutembea tembea)
C.mara nyingi hutokea baada ya kusambaa kwa maambukizo
D.ya socket ya jicho kutoka pembezoni kwa saines (sinusitis) za pua
E.husababisha kupoteza nuru za macho



Matibabu: Mpeleke mgonjwa kwa daktari wa masikio, pua na koo (ENT).





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 6553

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Je mtu anaweza kushiriki mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya ukimwi pasipo kuambukizwa?

Naomba kuuliza swaliJe mtu anaweza kushiriki mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya ukimwi pasipo kuambukizwa?

Soma Zaidi...
Dalili za UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UKIMWI

Soma Zaidi...
Ujue ugonjwa wa kuishiwa na damu

post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuishiwa damu kwa kitaalamu huitwa(Anemia) ni ugonjwa wa kuishiwa na damu mwilini na kusababisha maisha ya mtu kuwa hatarini

Soma Zaidi...
Mie ni mwanamke ninamaumivu chini ya kitovu upande wa kushoto, na nikishika tumbo nahisi kitu kigumu upande huo huo wa kushoto... hii itakua ni nini?

Je unasumbuliwa na maumivuvya tumbo chini ya kitovu upande wa kushito. Post hii itakuletea sababu za maukivubhayo na nini ufanye.

Soma Zaidi...
Tatizo la Kikohozi Cha muda mrefu

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za Kikohozi cha muda mrefu ni zaidi ya kero. Kikohozi cha muda mrefu kinaweza kuharibu usingizi wako na kukuacha unahisi uchovu. Matukio makali ya kikohozi cha muda mrefu yanaweza kusababisha kutapika, kizunguz

Soma Zaidi...
Hatua tatu anazozipitia mgonjwa wa tauni

Posti hii inahusu zaidi njia au hatua tatu muhimu anazopitia Mgonjwa wa gauni, kuanzia kwa Maambukizi mpaka kwenye hatua ya mwisho hasa kama Ugonjwa huu haujatibiwa mapema.

Soma Zaidi...
NJIA ZA KUKABILIANA NA MINYOO: kuosha mikono, kuwa msafi, kuvaa viatu, maji safi, kuivisha nyama vyema

NJIA ZA KUKABILIANA NA MINYOO Kwa kuwa tumekwisha kuona namna ambavyo minyoo huenezwa, hivyo basi ni rahisi sasa kutaja namna ya kubambana na minyoo.

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUGUNDUA VIDONDA VYA TUMBO

NAMNA YA KUGUNDUA VIDONDA VYA TUMBO Ili kugundua vidonda, daktari wako anaweza kwanza kuchukua historia ya matibabu na kufanya uchunguzi wa mwili.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Saratani ya ini.

Saratani ya ini ni Saratani inayoanzia kwenye seli za ini lako.

Soma Zaidi...
Dalili na sababu za mawe kwenye in yaani liver stone au intrahepatic stones

Katika post hii utakwend akujifunza kuhusu tatizo la kuwa na vijiwe kwenye ini vijiwe hivi hufahamika kama intrahepatic stones.

Soma Zaidi...