Siku za kupata mimba

Nitakujulisha siku ya kupata mimba na sifa zake, na namna ya kuweza kuitafuta

Siku za kupata mimba

SIKU ZA KUPATA MIMBA
Kwa wale wanaohangaika kutafuta ujauzito makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakwenda kukujuza siku yako mujarabu ambayo utatapa ujauzito. Pia nitakujuza sifa za siku za kupata mimba. Unajuwa wanawake wanatofautiana sana katika mifumo yao ya uzazi, simaanishi maumbile, namaanisha hali zao. Watu wengi wanaelewa kuwa mwanamke anaweza kupata mimba siku zote. Hapa hii sio sahihi kabisa. Ukweli ni kuwa kuna siku maalumu na ni chache. Kitaalamu siku hizi hufahamika kama faertile window.



Siku ya kupata ujauzito utaweza kuijuwa kwanza kuangalia mambo kadhaa nitakayoyatajahapo chini. Kabla ya kuyajuwa mabo hayo haklikisha kuwa unakula lishe bora na inayoshawishi kutafuta mtoto kweli kama unatafuta mtoto. Kwa wanaume wale vyakula vya kuongeza mbegu za kiume kama karangga, korosho, kunywa maji mengi na vyakula vingine, wasiliana nasi hapo chini nikueleze. Pia hakikisha wewe na mwenza mnakula vyakula vya kuongeza hamu ya tendo lando kwaingi. Hakikisha mwili ni msafi na kila mmoja amejiandaa vyema kumpokea mwenza. Sasa nakwenda kukufundisha siku za kupata mimba.



1.Kutambuwa siku za kupata mimba kwa mahesabu.
Kwanza hakikisha unaujuwa tarehe yako ukiwa ni mwanmke, na kama ni mwanaume itambuwe vyema tarehe ya mwenzio. Tambua byema mzunguruko wake wa hedhi unakwenda siku ngapi. Ukitambua vitu hivyo sasa twende pamoja. Wataalamu wanaeleza kuwa mwaname anaweza kubeba mimba siku 12 mpaka 14 kabla ya kuingia hedhi yake. Pia wataalamu wanatueleza kuwa yai la mbegu ya mwanaume inaweza kuwa hai ndani ya siku tatu mbaka 5 na yai la mwanamke linaweza kukaa masaa 12 mpaka 24 . ila sanasana ni siku 3, yaani mbegu iliyoingia leo inaweza kurutubisha yai siku tatu zijazo. Hivyo tyujaalie mwaname ana mrunguruko wa hedhi wa siku 28. tutafanya hivi:-



Mfano wa kwanza mwenye siku 28
A.28 - 12 = 16 (ongeza moja iwe 17, kufidia yai la mama)
B.16 - 02 = 14
C.14 - 3 = 11 (tunapunguza 3 nyuma kufidia mbegu ya maba)
Hivyo mwanamke huyu siku zake za kupata mimba ni kati ya siku ya 11 mpaka 17 toka siku ya kwanza aingie hedhi.



Mfano wa pili mwenye siku 35
A.35 - 12 = 23 (ongeza 1 iwe 24)
B.23 - 02 = 21
C.21 - 03 = 18
Hivyo mwenye mzunguruko wa siki 35 siku zake hatari kupata mimba ni kati ya siku ya 18 mpaka 24 toka siku ya kwanza kuona hedhi.



Mfano wa tatu mwenye siku 21
A.21 - 12 = 9 (ongeza 1 iwe 10)
B.9 - 2 = 7
C.7 - 3 = 4
Mwanamke huyu anaweza kubeba ujauzito punde tu baada ya kumaliza hedhi mpaka siku ya 10



Unaweza kutumia mifano hii kitafuta skuku yako ya kupata mimba. Wanawake wanatofautiana sana siku zao. Kuna ambao ni 21, kuna ambao ni 35. ila kwa hali ya kawaida siku za hedhi ni kati ya 21 mpaka 35. ikizidi hapo ama kuwa chini ya hapo kutakuwa na shida kwenye mfumo wa homoni. Kama upo katika kutafuta ujauzito hakikisha unashiriki ngono katika siku zote hizo ama unaweza kuruka ruka ila hakikisha unaanza na siku ya kwanza, kisha unaweza kuacha moja na kushiriki inayofata.



2.Sifa za siku za kupata mimba.
Baada ya kujuwa kuitafuta siku ya kupata mimba sasa napenda ujuwe ssifa za siku hiyo. Sasa hata kama unaijuwa kwa mahesabu ukweli ni kuwa unaweza pia kuikosa kwani sio maalumu. Sasa hapa nitakurahisishia kazi kwa kukutajia sifa za siku hizo za kupata mimba.



1.Siku ya kupata mimba ina sifa hii, kwanza joto la mwili linakuwa kubwa tofauti na siku zilizotangulia na siku zijazo. Tambuwa kuwa hapa mwili utakuwa na joto ila haliusiani na ugionjwa wowote ama mambo mengine. Kwa mfano kuchelewa kulala, misongo ya mawazo maradhi na homa kwa pamoja hupelekea joto la mwili kupata. Joto tunalolizungumzia hapa halisababishwi na sababu yeyeote katika hizi.



2.Uteute wa ukeni utakuwa mwingi kulinganisha na siku zilizopita. Uteute huu husaidia kati akuzisafirisha mbegu za kiume kwenda kutungisha mimba. Uteute kuu ni mlaini na unateleza sana. Mwanamke anaweza kuuiona baada ya kuingiza kidole ndani sana kwenye shingo ya uzazi.



3.Siku hii mwanamke atakuwa na hamu sana ya kushiriki tendo la ndoa kuliko siku zilizopita. Hii ni kutokana na miamsho iliyosababishwa na homoni ambazo zinaandaa mwili kwa ajili ya ujauzito.



Sifa hizi huweza kupotea baada ya kupata ujauzito ama muda wa kubeba mimba ukiisha. Mabadiliko hayo pia huweza kuathiriwa na mabo mengine kama matumizi ya uzazi wa mpango hasa wa kutumia sindano. Je utakuwa na maoni, maswali ama mapendekezo?. wasiliana nasi kwa hapo chini





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 3719

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 web hosting    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Mapendekezo muhimu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi mapendekezo muhimu kwa wajawazito, haya ni mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa afya ili wajawazito waweze kule mimba zao vizuri na kuweza kujifungua vizuri na kupata watoto wenye afya njema na makuzi mazuri pasipokuwepo na ule

Soma Zaidi...
Zijue mbegu za kiume zilizo bora.

Posti hii inahusu zaidi mbegu ambazo ni nzima na ambazo zina sifa ya kutungisha mimba kwa hiyo mbegu hizi utazigundua kwa kuwa na sifa zifuatazo.

Soma Zaidi...
Faida na hasara za kutumia kondomu kama njia ya uzazi wa mpango

Kondomu ni mpira ambao uwekwa kwenye uke au uume kwa ajili ya kuzuia mimba wakati wa kujamiiana

Soma Zaidi...
Huduma kwa wasioona hedhi

Posti hii inahusu zaidi msaada au namna ya kuwahudumia wale wasioona hedhi na wamefikiwa kwenye umri wa kuweza kuona hedhi.

Soma Zaidi...
je mtu kam anaona dalili za mimb ila akapima nakipim hakijamuonyesha kam ana mimb am hana je kuna uwezekan wakuw anayo

Dalili za mimba pekee haziwezi kuthibitisha uwepo wa mimba. Bila vipimo kwa. Muda sahihi huwezi kuwa. Na uhakika. Je na wewe unasumbuliwa na dalili za mimba na ukapona hakuna mimba? Makala hii ni kwa ajili yako. Swali

Soma Zaidi...
je mwana mke ana weza kubeba mimba kama hayupo kwenye siku zake za hatali ama

Mimba haipatikani kila siku, na pia mimba huingia kwa siku moja na katika muda mmoja. Baada ya mimba kutungwa hakuna tena nafasi ya kutungwa mimba nyingine.

Soma Zaidi...
Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni

Soma Zaidi...
Watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango

Post hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kutumia njia za uzazi wa mpango, Ni watu ambao Wana matatizo mbalimbali endapo wakitumia wanaoweza kuleta madhara mbalimbali.

Soma Zaidi...
tuseme nilifanya ngono jana na leo nipata period,je kuna uwezekano wa kupata mimba

Mimba inatungwa katika siku maalumu na hazizidi 10. Sio kila ukishiriki tendo unaweza pata mimba. Je unaweza kupata mimba baada ya kushiriki tendo wiki moja kabla ya kuingia hedhi?

Soma Zaidi...
Vitu vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid (majimaji yanayomzungruka mtoto aliyekuwepo tumboni wakati wa ujauzito)

Post hii inahusu zaidi viti vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid, ni jumla ya vitu vyote vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid.

Soma Zaidi...