Suratul-takaathur (102) imeteremshwa makkah Ina aya nane
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
- Suratul- Takaathur (102): Imeteremshwa Makkah, Ina Aya Nane.
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
- Kumekughafilisheni (katika) kutafuta wingi (wa mali na jaha na watoto na kujifakharisha kwayo).
- Hata mmeingia makaburini (mmekufa kabla ya kufanya kheri yeyote).
- Sivyo hivyo! Karibuni hivi mtajua (kuwa sivyo hivyo).
- Kisha (nasema) sivyo hivyo karibuni hivi mtajua (kuwa sivyo hivyo).
- Sivyo hivyo! Lau kama mnajua ujuzi wa yakini (kuwa sivyo hivyo msingefanya hivyo).
- Hakika mtauona moto wa Jahiym.
- Kisha (nasema) mtauona (moto) kwa yakini.
- Kisha kwa hakika mtaulizwa siku hiyo juu ya neema mlizopewa (mlizitumiaje).
Mafunzo kwa Ufupi.
- Pupa katika kutafuta anasa za dunia ndizo hupelekea mtu kumuasi Mwenyezi Mungu (s.w).
- Kuchuma mali na kuhangaikia watoto sio jambo baya, bali lisitusahaulishe katika kumtumikia Mwenyezi Mungu (s.w).
- Kuwepo siku ya mwisho ni jambo lisilo na shaka ili kila mtu akaulzwe juu ya jinsi alivyotumia neema alizopewa.
- Kutumia vibaya neema na vipawa tulivyonavyo hupelekea kumuasi Mola wake na hivyo kustahiki adhabu.
- Neema na vipawa tulivyonavyo ni dhamana kwetu na tutaulizwa siku ya Kiama.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Madrasa kiganjani π4 kitabu cha Simulizi π5 Dua za Mitume na Manabii π6 Kitabu cha Afya
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Madrasa kiganjani π4 kitabu cha Simulizi π5 Dua za Mitume na Manabii π6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Hukumu za mim sakina na tanwinkwenye hukumu za tajwid
Hukumu za kim sakina na tanwin ni idgham shafawiy, idh-har shafawiy, na Ikhfau shafawiy
Soma Zaidi...Aina za Madda twabiy kwenye usomaji wa Quran
Madda zimegawanyika katika maeneo makuu mawili ambayo ni madda twabiy na madda fariy
Soma Zaidi...HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA
SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina iβrab ( Ω Ω).
Soma Zaidi...Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r.a)
Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r.
Soma Zaidi...Dai kuwa Muhammad (s.a.w) alitunga Qur-an ili kuleta Umoja na Ukombozi wa Waarabu:
(vii)Dai kuwa Muhammad (s.
Soma Zaidi...