picha

Suratul-takaathur (102) imeteremshwa makkah Ina aya nane

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Kumekughafilisheni (katika) kutafuta wingi (wa mali na jaha na watoto na kujifakharisha kwayo).
  2. Hata mmeingia makaburini (mmekufa kabla ya kufanya kheri yeyote).
  3. Sivyo hivyo! Karibuni hivi mtajua (kuwa sivyo hivyo).
  4. Kisha (nasema) sivyo hivyo karibuni hivi mtajua (kuwa sivyo hivyo).
  5. Sivyo hivyo! Lau kama mnajua ujuzi wa yakini (kuwa sivyo hivyo msingefanya hivyo).
  6. Hakika mtauona moto wa Jahiym.
  7. Kisha (nasema) mtauona (moto) kwa yakini.
  8. Kisha kwa hakika mtaulizwa siku hiyo juu ya neema mlizopewa (mlizitumiaje).

 

Mafunzo kwa Ufupi.

  1. Pupa katika kutafuta anasa za dunia ndizo hupelekea mtu kumuasi Mwenyezi Mungu (s.w).
  2. Kuchuma mali na kuhangaikia watoto sio jambo baya, bali lisitusahaulishe katika kumtumikia Mwenyezi Mungu (s.w).
  3. Kuwepo siku ya mwisho ni jambo lisilo na shaka ili kila mtu akaulzwe juu ya jinsi alivyotumia neema alizopewa.
  4. Kutumia vibaya neema na vipawa tulivyonavyo hupelekea kumuasi Mola wake na hivyo kustahiki adhabu.
  5. Neema na vipawa tulivyonavyo ni dhamana kwetu na tutaulizwa siku ya Kiama.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/20/Thursday - 02:07:46 am Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1408

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 web hosting    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Makundi ya Id-ghamu katika usomaji wa Quran Tajwid

Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu.

Soma Zaidi...
Utofauti wa Quran na hadithi Al Quds

Has utakwenda kujifunza utofauti was Hadithi Al Quds na Quran

Soma Zaidi...
Hukumu ya Ikhfau katika tajwid

Ikh-fau ni moja ya hukumu za nun sakina na tanwin kwenye hukumu za Quran tajwid

Soma Zaidi...
Quran na sayansi

3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran??

Soma Zaidi...
Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum

SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s.

Soma Zaidi...